Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Azza Hilal Hamad

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. AZZA H. HAMAD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Kwa haraka haraka, naomba niungane na Mheshimiwa Bura kusema kwamba Wizara ya TAMISEMI siyo rafiki kwa Wizara ya Afya.
Mheshimiwa Mwenyekiti na Wabunge wenzangu, katika kitabu cha TAMISEMI hiki chenye majedwali kina kurasa 81, lakini kuanzia ukurasa wa 33 mpaka wa 81 wanaongelea elimu. Naomba Kamati ya Bajeti ikakae tujue hatma ya Wizara ya Afya ipo wapi kwenye ujenzi wa vituo vya afya na zahanati? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niende kwenye vifo vya mama na mtoto; taarifa inasema wanawake 42 kila siku wanakufa au wanapoteza maisha. Kwa nini wanapoteza maisha? Wanawake hawa wanapoteza maisha kwa sababu vituo vyetu vya afya havina majengo ya upasuaji, havina damu ya kuwaongeza akinamama hawa; akinamama wanapoteza maisha kwa kumwaga damu nyingi na kwa kukosa huduma ya upasuaji. Ndiyo maana nasema, naomba Kamati ya Bajeti ikakae tujue, waje na mpango wa kuhakikisha kwamba vituo vyote vya afya hata kwa kuanzia kila Jimbo tuambiwe watajenga vituo vingapi vya upasuaji katika vituo vyetu vya afya? (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, bila kufanya hivyo, Mheshimiwa Waziri wa Afya na Naibu wake, nawapenda sana, lakini nawaambia hawatafanya kazi vizuri kwa hilo kwa sababu vifo vitaendelea kuwepo na suluhu yake ni kuwepo kwa majengo ya upasuaji na upatikanaji wa damu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, niende katika Mkoa wangu wa Shinyanga. Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga inatakiwa kuwa na watumishi 680, lakini mpaka hivi ninaposimama hapa ina watumishi 341, ina upungufu wa watumishi 155, hiyo ni Hospitali ya Rufaa, lakini ina Madaktari Bingwa watatu tu, ina upungufu wa Madaktari 24. Katika upungufu wa Madaktari waliopo, hatuna Daktari Bingwa mwanamke hata mmoja! Hatuna Daktari Bingwa wa upasuaji hata mmoja! Naomba Mheshimiwa Waziri alifanyie kazi haraka iwezekanavyo. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, nizungumzie kuhusu ujenzi wa hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga. Mkoa wa Shinyanga uliomba shilingi bilioni tano kwa ajili ya ujenzi wa Hospitali ya Rufaa lakini mmetupa shilingi bilioni moja tu. Hivi kweli kuna dhamira ya dhati ya ujenzi wa hospitali hii? Tunategemea hospitali hii tunaijenga kwa shilingi bilioni moja? Hili halikubaliki! Naomba kama Serikali imedhamiria kweli kujenga Hospitali za Rufaa, basi wahakikishe wanatoa fedha ya kutosha, lakini siyo pesa kiduchu ambayo wanatupa, haiwezi kutufikisha popote. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, bado naendelea katika Mkoa wangu wa Shinyanga. Duka la MSD katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga mpaka sasa hivi tunavyoongea halipo. Naiomba sana Wizara, nimwombe Mheshimiwa Waziri, amefika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga lakini sijui hili wanaliwekaje?
Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la dawa ni kubwa, ukienda pale Manispaa ya Shinyanga hata kwa wale wenye Bima ya Afya, ni maduka mawili tu ambayo wanatoa huduma hii. Sasa linakuwa ni tatizo kubwa na inafika mahali watu hawaoni sababu ya kuwa na Bima ya Afya, kwa sababu hata wanapokwenda kutafuta dawa, hawazipati. Naiomba Serikali iende ikafungue duka. Naomba MSD waende wakafungue duka pale Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Shinyanga. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, natumia fursa hii kuipongeza sana Serikali kwa sababu asiyeshukuru kwa kidogo, hata kwa kikubwa pia hawezi kushukuru. Naipongeza kwa nini? Naipongeza kwa sababu Bunge lililopita kila siku tulikuwa tunaimba humu ndani, MSD wanadai, lakini bajeti ya mwaka huu imeonyesha dhamira ya dhati ya kulipa deni la MSD. Kwa hiyo, niseme nawapongeza sana, naomba mkalipe fedha hizo haraka iwezekanavyo, nina hakika tatizo la dawa kwa kiasi fulani litapungua.
Kwa hiyo, nawaomba sana madawa haya yaweze kupatikana. Vile vile naomba sana tunapokuwa…