Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Sita na Mkutano wa Saba wa Bunge pamoja na Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa kwenye Mkutano wa Tatu na Mkutano wa Nne wa Bunge

Hon. Amour Khamis Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tumbe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa Bungeni kwenye Mkutano wa Sita na Mkutano wa Saba wa Bunge pamoja na Uchambuzi wa Taarifa za Utekelezaji wa Maazimio ya Bunge kuhusu Sheria Ndogo zilizowasilishwa kwenye Mkutano wa Tatu na Mkutano wa Nne wa Bunge

MHE. AMOUR KHAMIS MBAROUK: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa fursa hii na mimi ya kuchangia katika wasilisho hili la sheria ndogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunakushukuru kwa kutuchagua pia katika jambo hili au katika Kamati hii ya Sheria Ndogo, tunakushukuru sana wewe na Mheshimiwa Spika kwa sababu Kamati ya Sheria Ndogo kimsingi ndiyo Kamati inayoendeleza Miji, Halmashauri, Vijiji, kuna sheria nyingi hapa ambazo sisi zitatufanya tuelewe kila kitu kinachokwenda ndani ya nchi hii, tunawashukuru sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia nimshukuru Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Samia Suluhu Hassan, mama msikivu, muadilifu, mwenye hekima, mwenye huruma kubwa sana kwa wananchi wake na hii ni kwa sababu anatoka kwenye Chama cha Mapinduzi, chama ambacho kinatekeleza Ilani yake kwa uangalifu na uadilifu sana. Mama huyu ukilalamika tu tozo yeye anaondoa, sijui halmashauri hii haina shule anakuletea, hakuna hospitali mahali analeta, huyo ndiyo Mama Samia kutoka Chama cha Mapinduzi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mpaka Mama Samia anafikia kwenye maamuzi hayo au kwenye sifa hizo ni kwa sababu Tanzania ni nchi tunayoisifu na inayosifika duniani kwamba ni nchi yenye utawala bora. Na nchi hii yenye utawala bora ni utawala wa sheria, na sheria hizi ndiyo tupo kwenye sheria ndogo, sheria zinazoongoza huko vijijini na kwenye halmashauri mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa tunaomba sana wale ambao wamekasimiwa madaraka na Bunge kutunga sheria hizi tunazoziita sheria ndogo basi wawe makini sana kwa sababu hizi sheria tunaziita ndogo, lakini ndiyo zinazowafanya watu wawe jela, ndizo zinazowafanya watu watozwe faini. Kwa hiyo, si sheria ndogo kama tunavyosaini ni sheria hasa za nchi. Kwa hiyo, tunawaomba sana wawe makini sana na hii ni kwa sababu Waarabu wana msemo wao wanasema dawamulhali minalmuhali (mtu hadumu kwa kwa hali moja Maisha) na sheria hizi zinaenda kusimamiwa na watu mahakamani, leo hakimu anaweza kuwa na hasira akatumia sheria ndogo hii hii akamuonea mtu. Kwa hiyo, ili tumdhibiti hasira zake, furaha yake, huzuni yake lazima tuweke sheria ambayo itamuongoza asije akaongozwa kwa hisia zake.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nina mfano hapa wa sheria inayoitwa Electricity Act, Sura 131; kuna sheria ndogo inasema Electrical Installation Services hii imetoa adhabu mbili; adhabu ya kwanza kwa mtu ambaye hana leseni ya kufanya installation ni faini isiyozidi shilingi milioni moja au kifungo kisichozidi miaka mitano au vyote viwili, lakini mtu mwingine anayo leseni, lakini atafanya jambo nje ya leseni yake, leseni imekwambia wewe kazi yako ni kuweka waya tu hautakiwi baada ya waya kuweka meter kwa mfano, kuweka plug, yeye kwa sababu ya ubinadamu wake akapitiwa akaweka vile vitu, kwa hiyo, yeye anatakiwa alipe shilingi 200,000; lakini amefanya kitu ambacho ni nje ya leseni yake maana yake ni kwamba tuna mli- guard kwamba huyu leseni pia hana jambo alilofanya hana leseni, lakini sheria imemfanya kwamba yeye alipe faini shilingi 200,000. Sasa lazima tuwe waangalifu tusiwe na bias kwamba huyu yupo hivi yupo hivi, lazima tufike mahali wananchi wetu wote ni wamoja tuwe na huruma kama alivyo Mama Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, wale tunaomwakilisha lazima tuwe makini katika jambo hilo. Lakini sawa ulishaliona tatizo hili sheria ndogo ilishaona tatizo tumeitana na tunawasifu Mawaziri Mashallah Alhamdulillah, ni wasikivu sana wanalichukua tunakubaliana tunaenda kulirekebisha hasa hiyo kurekebisha hiyo huku sheria ipo mtaani inafanyakazi, lakini hapa muda wa kurekebisha watu wanaumia field, hairekebishwi inatuchukua muda mrefu sana mpaka kurekebishwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, alikuwa ametoa wazo kwamba Bunge hili liazimie kwamba sasa kazi inapotolewa hii ya kurekebisha iwe na muda maalum. Kwa hiyo, tunaliomba sana Bunge lifanye hivyo kwasababu hizi sheria ndiyo zinaumiza watu wetu kule field. Tuwafikirie watu wetu kwamba wao ndiyo wanaumia.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja. (Makofi)