Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kuongeza Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kuongeza Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi ili niweze kuchangia Itifaki hii ya kuongezea Mahakama ya Afrika ya Mashariki nguvu ya kisheria ya kuanza kusikiliza kesi za biashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpongeze Waziri wa Katiba na Sheria na Mheshimiwa Naibu Waziri na timu yao yote kwa kazi ambayo wamefanya. Kazi ambayo Bunge imepewa ifanye sasa ni kwa mujibu wa Katiba wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa mujibu wa Ibara ya 63(3)(e) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasema hivi na naomba ninukuu:

“Kujadili na kuridhia mikataba yote inayohusu Jamhuri ya Muungano na ambayo kwa masharti yake ni lazima inahitaji kuridhiwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania”. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, tunafanya kazi ya kikatiba kabisa ya Bunge na niwapongeze Mawakili Wasomi wale ambao wameanza mjadala, Mheshimiwa Mwinyi ambaye kwa kweli hili ndiyo eneo lake la kujidai Afrika Mashariki na Mheshimiwa Zainab Katimba, Mheshimiwa Jerry Silaa na Wakili maarufu sana hapa Bungeni Mheshimiwa Thadayo. Kwa kweli sasa napata wakati mgumu kusema baada ya hao wote kusema. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mahakama ya Afrika Mashariki sisi kama Taifa, kwanza ni faida kubwa kwetu kwa sababu Makao Makuu ya Mahakama hii ya Afrika Mashariki ipo Arusha Tanzania. Kwa hiyo, tayari kwa wenzetu wale Mahakama hii kuwepo kwetu ni faida. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama walivyosema wengine hizi Itifaki za Common Markets, Monitoring Union na Customs Union tayari zimeshapitishwa lakini kwa integration ambayo inaenda vizuri sana, mkishaanza kuingia kwenye Itifaki hizi za Common Markets, Customs Union na Monitoring Union ni lazima mtarajie kwamba disputes zitatokea na kwa mujibu Treaty hii ukisoma article 5 and 6 imeeleza kabisa misingi ya Treaty hii kwamba ni lazima tumekubaliana tusuluhishe migogoro yetu kwa namna ya kisheria nzuri na hakuna namna bora zaidi, zaidi ya kwenda Mahakamani. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, ili Wanachama wa Afrika Mashariki waweze kufurahia protocols hizi za Monitory, Customs Union na Common Market lazima kuwe na Mahakama ambayo likitokea jambo, yeyote kati ya wale anaweza kwenda Mahakamani na akapata haki yake. Kwa hiyo, ni muhimu kabisa na hata nje ya dunia wakitaka kuangalia kama integration yetu ni nzuri sana, wataangalia kama kuna mechanism kwamba jambo likitokea unaweza kwenda Mahakamani na ukapata redress. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hii jurisdiction kwa kweli wamefanya kazi nzuri sana. Labda nimtoe wasiwasi dada yangu aliyekuwa anazungumza hapa, nilikuwa naangalia hii protocol yenyewe article 3 kwamba hainyang’anyi haki za Mahakama zetu kusuluhisha migogoro hii. Ukisoma hiyo article 3(2) inasema hivi naomba ninukuu: “The extension of jurisdiction under paragraph 1 shall not preclude the exercise of jurisdiction conferred upon other bodies by the Treaty or the relevant laws of the Partner States”.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo hakuna confusion hapo. Hii ni option tu kwamba party anaweza kwenda Mahakama hii ya Afrika Mashariki kama ni jambo linalohusiana na mambo ya customs union, common market ama monitoring union. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata ukisoma Treaty yenyewe imeeleza kabisa kwamba, mtu anaweza kwenda kwenye Mahakama zetu na akaomba Mahakama zetu zitoe tafsiri ya Treaty hii ya Afrika Mashariki. Kwa hiyo hakuna confusion. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nagusia alichosema Mheshimiwa Tadayo. Unajua wakati wa Supreme Court of Kenya wakati kesi hizi zinaendelea, kati ya messages nyingi tulizozipata tunaulizwa hivi huku kwetu tuna wanasheria wazuri kama wale ambao tulikuwa tunawaona kwenye TV? Jibu ni ndiyo. Kabisa! (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, lakini ni kweli, lazima tujiandae kwa sababu Afrika Mashariki ni competitiveness. Ukishakuwa competitive ni lazima soko sasa litafunguka. Kwa hiyo, niwatoe wasiwasi tu, wako Wanasheria wazuri sana, hapa kwetu tu ni minus TV ndiyo maana hamuwaoni, lakini kesi zikiwa live mtawaona, tena wako wazuri sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Waziri, lakini ni kweli, tuendeshe elimu nzuri sana ili watu wetu wajiandae kabisa namna ya kushirikiana na wenzetu wa Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nguzo kuu ya Afrika Mashariki ni kitu kinaitwa widening and deepening of integration. Kwa hiyo, hii ni stage moja wapo ya sisi kuendelea ku-widen scope ya Afrika Mashariki na kui-deepen. Kwa hiyo, kila wakati kumbuka to widen and deepen the integration kwa sababu tuliamua. Hii ni uchumi na kwa kweli kwa nchi zote za Afrika Mashariki na sasa nchi nyingine zinaongezeka, ziko Saba sasa, nchi yetu iko strategically positioned kuwa mnufaika mkubwa sana wa integration ya Afrika Mashariki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Kamati imefanya kazi nzuri sana. Ninaomba tulishawishi Bunge hili likubali kupitisha Itifaki hii bila kuchelewa ili Mheshimiwa Waziri na timu yake wakaendelee kufanya kazi nzuri sana. Na sisi kwa kweli we are Leaders in the region, lazima tuoneshe leading role kwenye vitu kama hivyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya, nakushukuru. Ahsante sana naunga mkono hoja. (Makofi)