Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kuongeza Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki

Hon. Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ya Kuongeza Mamlaka ya Mahakama ya Afrika Mashariki

MHE. JERRY W. SILAA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi katika kuchangia na kuliomba Bunge lako pamoja na kuunga mkono hoja ya kuridhia kuiongezea The East African Court jurisdiction ili iweze kufanya kazi ya kutoa tafsiri na kutatua migogoro itakayotokana na zile protocol ambazo wachangiaji wengi wamezitaja nami nitazitaja hapo baadaye.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niungane na wenzangu kumpongeza kwa dhati Dkt. Damas Ndumbalo, Waziri wa Sheria na Katiba kwa uwasilishaji wake mzuri wa hoja ambayo imetupa uelewa mpana wa Itifaki hii ambayo tunaenda kuiridhia. Vilevile nimpongeze mdogo wangu Keisha kwa uwasilishaji wenye ueledi mkubwa alioutoa hapa kwa niaba ya Kamati ya Bunge na Sheria ya Katiba. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, niendelee kupongeza; nimpongeze sana ndugu yangu Abdullah Mwinyi, maana yeye leo hakuchangia ametoa lecture na nimemwomba aandae notisi kina Kingu wangependa kuzisoma, zilete uelewa mpana zaidi na ametueleza na tumepata fursa ya kuona Wabunge wa Afrika Mashariki wenye sifa tunaowapeleka kule wanapokuja kuleta tija kwenye Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Nchi yetu ni Mwanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki kwa mujibu wa the East African Treaty tuliyotia saini mwaka 1999 na ilivyoanza rasmi mwaka 2001 kama walivyoeleza wachangiaji wengine. Article 9 ya Treaty hiyo ndiyo inayoanzisha vyombo mbalimbali vya kiutendaji, The East African Legislative Assembly, The East African Court of Justice na ukisoma article ile inaipa mamlaka mahakama hii kuweza kutafsiri mambo yanayotokana na treaty ile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wachangiaji wote wamesema, mwaka 2004 tumeingia kwenye common customs, tumeridhia kuwa na common custom kwa maana ya custom union ya pamoja, rates za forodha na nadhani Mheshimiwa Abdullah ameelezea vizuri zaidi na ndio maana hapa tukiwa tunapitisha bajeti zile custom measures (jitihada) za Serikali za forodha zinakuwa zimeridhiwa na Nchi zote za Afrika Mashariki na sisi kama Nchi Wanachama tunatakiwa tuendane nazo kwa jinsi Mawaziri wa Fedha wa Nchi za Afrika Mashariki walivyokubaliana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwaka 2010 tumeingia kwenye common market na mwaka 2013 tumeenda kwenye single currency ambayo imeelezewa mchakato wake wa kufikia kule kwa kufanya integration ya chumi za nchi zote wanachama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kinachoombwa hapa leo ni nini? Amekisema vizuri Wakili Msomi Zainab Katimba, ni ile article 27(2) ambayo inaipa Nchi Wanachama ya ile East African Treaty tuliyoingia mwaka 1999 uwezo wa ku- extend jurisdiction ya Mahakama hii ili iweze kutoa majibu kwenye hizi protocols nyingine ambazo kabla ya kuomba ridhaa hii, masuala yote yaliyokuwa ya kimgogoro wa protocol hizi yalikuwa yanaamuliwa na Mahakama za partner state na madhara yake ni nini? Madhara yake kila Mahakama ya Nchi Wanachama itatoa tafsiri kwa kadri ya busara ya Mahakama husika kama mhimili unaojitegemea wa Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, suala moja linaweza kujitokeza kwenye nchi mbili tofauti kwa item moja ya common customs, lakini ikapata maamuzi mawili tofauti kwa Mahakama ya Nchi Wanachama na ku-set precedent mbili kwa jambo linalofanana kwa protocol moja. Kwa hiyo, kinachoombwa hapa ni nini? Kinachoombwa hapa ni jambo la kisheria ambalo lipo kwenye treaty la kutaka ku-extend jurisdiction ya Mahakama hii ya Afrika Mashariki ili sasa iwe na nguvu ya kufanya tafsiri na maamuzi wa hizi protocol tatu tulizozieleza kwa maana ya common custom, common market na monitory union na hilo nilishawishi Bunge hili lina faida kubwa katika ule uwanda mpana mzima wa ile nguvu ya kiuchumi tunayoitafuta kama Jumuiya ya Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndiyo maana hata leo tulipokaa hapa Babu Tale hajakaa, tumekaa katika safu moja tu ya kutafuta ile mantiki ya kutengeneza jambo hili kwenye uwanda wake wa kisheria na Mheshimiwa Kingu amekiri kwamba kuna kiti kilikuwa wazi lakini ameshindwa kuja kukaa kwa sababu amesema yeye ameona ajikite na Ole-Lekaita kwenye uchangiaji wa mwisho yeye amejitolea kwenye suala la kupiga makofi. (Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunawashawishi sana Waheshimiwa Wabunge kuweza kuridhia hoja hii iliyopo mezani ili nchi yetu kama wanachama tuliyoridhia ile East African Treaty mwaka 1999, tuweze ku- extend jurisdiction ya Mahakama hii kwa faida pana ya Jumuiya yetu ya Afrika Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa maneno hayo, naunga mkono hoja na nirejee tena kuomba Bunge lako liliridhie protocol hii. Ahsante sana. (Makofi)