Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Mkataba wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Ugaidi ya Mwaka 2004

Hon. Joseph Michael Mkundi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukerewe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Mkataba wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Ugaidi ya Mwaka 2004

MHE. JOSEPH M. MKUNDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kupata fursa hii. Nianze kwa kumpongeza Mheshimiwa Waziri kwa kuwasilisha Itifaki hii ambayo ni muhimu sana kama walivyotangulia kusema watangulizi. Nimpongeze Mwenyekiti wa Kamati yetu mimi kama Mjumbe wa Kamati, kwa uwasilishaji wake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Itifaki hii ni muhimu na hasa kwa kupata mustakabali mwema wa maendeleo ya kiuchumi na kijamii katika Taifa letu. Sisi Tanzania kama moja ya nchi ambazo siyo kisiwa tunachangamana, tunashirikiana katika nyanja mbalimbali na mataifa mengine yanayotuzunguka, hatuna namna yoyote tunayoweza kutafuta maendeleo ya Taifa letu kama kuna shida ya usalama kwenye Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa miaka ya karibuni kumekuwa na shida ya usalama hasa kutokana na matukio ya kigaidi. Jambo ambalo limepelekea jumuiya mbalimbali kujipanga ili kukabiliana na matukio haya. Inapoletwa Itifaki hii leo katika Bunge lako Tukufu, niombe Waheshimiwa Wabunge kwa umoja wetu tuweze kuliridhia Itifaki hii. Kwa sababu kupitia Itifaki hii, itafanya Taifa letu liweze kushirikiana na mataifa mengine kudhibiti lakini na kukabiliana na matukio ya kigaidi, lakini na kuzuia matukio ya namna hiyo vilevile. Leo tupo kwenye harakati za kujenga misingi imara ya kiuchumi ya Taifa letu. Hatuwezi kunufaika na misingi hii kama kutakuwa na shida ya usalama kwenye Taifa letu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namna pekee ni kushirikiana na wenzetu katika kukabiliana na matukio hayo. Tuweze kutambua ni angle zipi ambazo wahalifu kupitia ugaidi wanaweza kuzitumia na ni namna gani tunaweza tuka-train watu wetu kushirikiana na watu wengine katika kukabiliana na matukio haya. Yote haya hatuwezi kuyafanya sisi kaka Taifa tukiwa tumejitenga, ni lazima tushikamane, tushirikiane na mataifa mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kama ambavyo Mwenyekiti wa Kamati yetu amesoma taarifa yetu, tumechambua Itifaki hii, ni Itifaki muhimu na ya msingi sana Bunge letu kuweza kuridhia ili sasa kama mataifa mengine tuweze kushirikiana kudhibiti, lakini na kuhakikisha usalama wa watu wetu na mali zao unakuwepo ili sasa tuweze ku-concentrate kwenye kushughulikia mafanikio katika uchumi kwenye Taifa lakini na kwa mwananchi mmoja mmoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo kwa uchache, niombe Waheshimiwa Wabunge wenzangu, kama ambavyo sisi taarifa yetu tumeiwasilisha kama Kamati, tuungane kwa pamoja kuridhia Itifaki hii ili sasa nchi yetu iwe nchi ya 22 kuridhia Itifaki hii, kuungana na mataifa mengine kushughulikia na kudhibiti matukio ya kigaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, nashukuru na naunga mkono hoja. (Makofi)