Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Mkataba wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Ugaidi ya Mwaka 2004

Hon. Selemani Jumanne Zedi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukene

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la Kuridhia Itifaki ya Mkataba wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika wa Kuzuia na Kupambana na Ugaidi ya Mwaka 2004

MHE. SELEMANI J. ZEDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi hii ili na mimi niweze kuchangia kwenye hoja hii ya Itifaki ya Mkataba wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika ya Kuzuia na Kupambana na Ugaidi. Mimi nitajikita kwenye kueleza faida ambazo kama nchi tutazipata endapo tutaridhia itifaki hii ya Umoja wa Nchi huru za Afrika ya Kupambana na Kuzuia Ugaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ugaidi kutokana na nature yake ulivyo ni vigumu sana kwa nchi moja peke yake kupambana nao. Ugaidi ni tukio ambalo ni organized crime na mara nyingi ni cross border. Ni tukio ambalo wanaoshiriki kulifanya wanakuwa ni watu wana mpango mkubwa na ambao unavuka mipaka ya nchi. Sasa nchi moja bila kushirikiana na wenzako ni vigumu sana na almost impossible, haiwezekani kabisa kupambana na ugaidi kwa kuendesha mapambano hayo peke yako tu kama nchi moja kama vile uko kisiwani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, faida kubwa ya kuridhia mkataba huu, itifaki hii; na mimi niwaombe sana waheshimiwa Wabunge wenzangu turidhie itifaki hii kwa sababu faida kubwa ni kwamba itaiwezesha nchi yetu ya Tanzania kushirikiana na nchi nyingine kuweza kupambana na huu ugaidi ambao nimesema kwamba ni organized crime, na nature yake ni matukio ambayo yanavuka mipaka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, gaidi anaweza akafanya ugaidi nchini kwako lakini mipango ya kutekeleza ugaidi huo ameifanyia nje ya nchi yako, na fedha za kutekeleza ugaidi huo zimetoka nje ya nchi yako. Kwa hiyo, kama hushirikiani na wenzako, na nchi nyingine ni vigumu sana na hutaweza kupambana na huo ugaidi. Na kuridhia kwa itifaki hii kutatuwezesha Tanzania kama nchi kushirikiana na nchi nyingine ambazo nazo zimeridhia ili kuweza kupambana na huo ugaidi kwa pamoja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nchi yetu Tanzania tulisaini Itifaki hii mwaka 2004 lakini haikuwa-enforced mpaka pale ambapo angalau nchi 15 ziliweza kuridhia, na ambayo ilikuwa ni mwaka 2014. Kwa hiyo utaona kwamba tangu instrument hii imekuwa-enforced, kuanzia mwaka 2014 mpaka leo ni kama miaka minane. Sasa, ukiangalia hali ilivyo sasa hivi kama nchi yetu tuna umuhimu sana wa kushirikiana na wenzetu ili kupambana na kuzuia ugaidi. Hii ni kwa sababu wote tunafahamu kwamba nchi yetu sasa hivi kwa namna inavyokwenda kuna fedha nyingi sana na uwekezaji zinakuja. amezungumza hapa Mheshimiwa Chumi muda uliopita; kwamba kuna flow ya fedha nyingi za uwekezaji zinakuja nchini kwetu kwa ajili ya miradi mbalimbali ya kimaendeleo na kiuchumi. Sasa, ili kuwapa confidence hao wawekezaji ambao wanaleta fedha zao kuja kuwekeza nchini kwetu ni lazima wawe na uhakika ya kwamba uwekezaji wao hautaathirika na vitendo vya ugaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na njia moja ya wao kuwa na uhakika ni sisi kuridhia Itifaki hii ili tuwemo kwenye orodha ya nchi ambazo zinashirikiana kupambana na ugaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baadhi ya faida za kuridhia mkataba huu zimeelezwa. Kwa mfano Barani Afrika kuna kituo ambacho ni kimoja tu kipo Algiers - Algeria ambacho ndicho kinachotunza taarifa za magaidi wote, mienendo ya magaidi, magaidi ni kina nani, wana mipango gani, taarifa zote zinatunzwa na kituo cha kanzidata ambacho kipo Algiers – Algeria. Sasa ili uweze ku-access taarifa hizo ni lazima uwe umeridhia mkataba huu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, sisi Wabunge tukiridhia mkataba huo maana yake tunaipa nchi yetu uwezo wa ku-access hizo data za magaidi, jambo ambalo litatusaidia sana kupambana na huo ugaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuridhia Itifaki hii kuna faida nyingi na hakuna hasara yoyote. Kwasababu kimsingi kama nchi tulishasaini hii Itifaki mwaka 2004. Kwa hiyo, issue ya kusiani haipo tena, sasa hivi ni issue ya kuridhia. Kwa kusaini maana yake ni kwamba wakuu wa nchi wali-approve, na ndiyo maana nchi kama Tanzania tukasaini. Kwa hiyo, sasa kinachotakiwa ili uweze kunufaika na faida zinazopatikana na Itifaki hii ni lazima uridhie. Kwa hiyo, tunachofanya sasa ni kuridhia tu lakini kusaini tulishasaini. Na tunaridhia ili tuweze ku-access hizo faida.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeona hapa mojawapo ya faida ni kubadilishana uzoefu na utaalam. Hizi nchi tunapishana uwezo wa kukabiliana na magaidi. Kuna nchi nyingine inakuwa na uwezo zaidi na inakuwa na best practice zaidi. Kwa hiyo, ukiridhia Itifaki hii maana yake ni kwamba unakuwa kwenye fursa ya kuweza ku-share best practice na nchi nyingine ambazo zina uwezo pengine zaidi yetu wa kupambana na magaidi. Kwa hiyo, hakuna haja yoyote ya kutoridhia kwa sababu tutakuwa tunajinyima fursa na faida nyingi ambazo zipo kwenye kuridhia kwa Itifaki hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niwaombe sana Waheshimiwa Wabunge wenzangu turidhie Itifaki hii ya Umoja wa Nchi Huru za Afrika ya Kuzuia na Kupambana na Magaidi kwa sababu ina faida nyingi na haina hasara yoyote kwa nchi yetu, ili tuweze kujenga confidence kwa wawekezaji ambao sasa hivi kwa jitihada kubwa zinazofanywa na Rais wetu wa Awamu ya Sita, Mama Samia Suluhu Hassan, fedha nyingi zinakuja, kwa hiyo, ni lazima turidhie Itifaki hii ili wawekezaji wetu wawe na confidence, wawe na amani kwamba mitaji yao haitaathirika na shughuli na operation za kigaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja na ninawaomba Waheshimiwa Wabunge turidhie Itifaki hii. Ahsante sana. (Makofi)