Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Dr. Jasson Samson Rweikiza

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. DKT. JASSON S. RWEIKIZA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA SHERIA NDOGO: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi kuja kuhitimisha hoja yangu. (Makofi)

Ninawashukuru Waheshimiwa Wabunge wote kwa jinsi ambavyo wamepokea taarifa hiyo hususani waliochangia kwa kuunga mkono ambao ni Mheshimiwa Judith Kapinga, Mheshimiwa Priscus Tarimo, Mheshimiwa Ramadhan Suleiman Ramadhan, Mheshimiwa Humphrey Polepole na Mheshimiwa Stella Manyanya ametoa taarifa ya kuunga mkono.

Mheshimiwa Spika, kazi tunayoifanya kwenye Kamati ni kuhakikisha kwamba kazi mama ya Bunge ya kutunga sheria haiharibiwi na waliokasimiwa. Kazi ya kutunga sheria iwe ni sheria mama, sheria ndogo ni kazi ya Bunge, lakini Bunge kwa mamlaka yake chini ya Katiba inakasimu mamlaka hayo kwa mamlaka nyingine ziwe Halmashauri, ziwe Wizara na mamlaka nyingine kufanya kazi hiyo.

Kwa hiyo, Kamati hii kazi yake kubwa ni kama watchdog, ni kuangalia kwamba zile sheria ndogo ziko vizuri kwa niaba ya Bunge hili kwa sababu kama nilivyosema mwanzoni kwamba Bunge haliwezi kukwepa lawama iwapo sheria ndogo itakuwa inakinzana na sheria mama au Katiba au sheria nyingine au haitekelezeki, kwa hiyo hiyo ndiyo kazi kubwa ya Kamati.

Mheshimiwa Spika, ni kuweka ustawi wa wananchi ameongea Mheshimiwa Judith Kapinga hapa akasema kuna malipo ya fedha kwa njia ya mtandao ile PayPal na nchi inapoteza mapato. Hilo siyo jambo jema, ninaomba wahusika kama ni Wizara ya Fedha au wahusika wengine wanaohusika na jambo hilo walifanyie kazi ili kusudi nchi isipoteze mapato, ipate mapato ya kutosha na ustawi wa wananchi uweze kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, nimesema hapo awali nirudie kwa ajili ya msisitizo kwamba kuna baadhi ya mamlaka ambazo zimetoza kodi au tozo kwa jambo hilo mamlaka zaidi ya moja. Halmashauri ya Moshi inatoza kwenye kumbi za sinema na starehe kodi ambayo inatozwa pia na Bodi ya Filamu, kwa hiyo mwananchi anaumia analipa kodi mara mbili jambo ambalo siyo zuri, ndiyo kazi yetu kuangalia kwamba halitokei.

Mheshimiwa Spika, ninawashukuru Mamlaka mbalimbali, Wizara na wengine wanaitikia wito haraka na wanafanya marekebisho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu Wabunge wameunga mkono hoja, sina la kuongeza naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. HUMPHREY H. POLEPOLE: Mheshimiwa Spika, naafiki.