Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

Hon. Felister Aloyce Bura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kwa Mwaka wa Fedha 2016/2017

MHE. FELISTER A. BURA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa muda mchache sana. Nimeangalia katika hotuba ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuangalia fedha za zahanati, sikuona mahali popote ambapo kuna fedha za ujenzi wa zahanati na Wizara ya Afya pia sikuona fedha za ujenzi wa zahanati.
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba utumie Kiti chako, Kamati ya Bajeti irudi ikapange fedha za zahanati nchi nzima. Tukitaka mafanikio katika kazi zetu ni lazima tufuate utaratibu uliowekwa.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Bima ya Afya, Mkurugenzi aliyekuwepo Mr. Humba alistaafu mwaka 2013, akakaimishwa Miss Mdee akatolewa, akakaimishwa mwingine Mr. Mhando akatolewa. Bima ya Afya haina Bodi, jamani tunategemea ufanisi hapo kweli! Hatuwezi kupata ufanisi! Wale watumishi kila mtu anaogopa kutumbuliwa! Mheshimiwa Waziri amteue Mkurugenzi Mkuu wa Bima ya Afya, Bodi ya Bima ya Afya iko chini ya mamlaka yake.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali ya MOI aliyeko anakaimu, tunategemea ufanisi kutoka wapi? Taasisi ya J. K. Kikwete, taasisi ile aliyeko Profesa Janabi anakaimu. Tunategemea ufanisi kutoka wapi? Kuna kazi gani au kuna kazi gani kuwateua wale kama wanafaa? Hakuna Bodi ya Muhimbili. Mkurugenzi wa Muhimbili anakaimu. Tunategemea ufanisi kutoka wapi?
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali yetu ya Mirembe ina Manesi 89 kati ya Manesi 700. Jamani wale wana-deal na watu wasio na akili timamu. Siku moja Nurse, tena mwanamke, aliniambia mgojwa wa akili alitaka wafanye ngono. Nurse anafanya kazi tangu saa 1.00 mpaka saa 12.00 anawahudumia wagonjwa 20 kwenye wodi moja. Wagonjwa wenyewe hawana akili timamu.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Ummy nampenda sana, lakini ataniambia ni lini atawapeleka wafanyakazi Mirembe? Bodi ya Mirembe haipo! Kwa hiyo, hata ufanisi mkubwa hauwezi. Wale watu wanafanya kazi katika mazingira magumu sana. Hebu awafikirie watu wa Hospitali ya Mirembe.
Mheshimiwa Mwenyekiti, Hospitali yangu ya Mkoa wa Dodoma aliitembelea Mheshimiwa Waziri wiki iliyopita na tukamwonyesha jengo ambalo lipo mbele yake, lile jengo la wodi ya wazazi lina vitanda 180, wodi inayotumika sasa hivi ina vitanda 18 tu, wanawake waliozaa wanalala wawili wawili. Siyo haki!…