Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. JUDITH S. KAPINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi, awali ya yote ningependa niipongeze Kamati hii, ni mojawapo ya Kamati ambayo inafanya kazi kubwa sana kupitia sheria ndogo nyingi sana. (Makofi)

Kwa hiyo, kwa kweli nimpongeze Mwenyekiti na Kamati nzima kwa kazi kubwa sana ambayo wanaifanya. Inawezekana Kamati hii ikadogoshwa kwa maana inaitwa Sheria Ndogo, lakini niseme ni Kamati ambayo inagusa maisha ya Watanzania kwa kupitia Kanuni na miongozo mingi sana na kuirekebisha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niipongeze Serikali kwa kuleta mabadiliko ya Kanuni mbalimbali ambazo zinasaidia utekelezaji wa sheria mama, lakini pamoja na kuipongeza Serikali ningependa niishauri Serikali, zipo sheria mama nyingi ambazo Kanuni zake zimepitwa na wakati; zipo pia sheria mama nyingi ambazo zinahitaji kutungiwa Kanuni ili ziweze kuendana na nyakati ambazo tunazo sasa hivi. Ningependa nitoe mfano na vilevile niishauri Serikali kwamba kuna Kanuni ambazo ni za umuhimu sana ambazo, tungeshukuru kama zingeletwa kwenye Bunge kupitia Kamati mapema sana ili Watanzania waweze kuneemeka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mfano wa kanuni hizo ni kanuni zinazohusiana na mifumo ya malipo ya fedha kwa njia za mtandao. Kanuni na sheria zinazohusiana na mifumo ya malipo kwa njia ya mtandao zinahitaji, kufanyiwa marekebisho ili yaweze kuendana na teknolojia ambayo tunayo sasa hivi. Mpaka leo ukiangalia sheria na kanuni zetu zinataka makampuni ya nje yanayofanya biashara na wafanyabiashara wanaouza huduma na bidhaa, hapa Tanzania kwenda nje ya nchi kuweza kufanya huduma za malipo ya fedha wakiwa na leseni ya hapa Tanzania (National Payment License). (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo hili ni jema kwa sababu Serikali inalinda mapato, lakini lina changamoto kwa sababu badala ya kulinda mapato tunapoteza mapato. Ningependa niseme kwamba hapa nchini kwetu kuna njia kuu za malipo kwa wafanyabiashara, wanaofanya biashara kwa kuuza bidhaa na huduma nje ya nchi. Njia kuu ambayo imezoeleka ni watu wa nje ya nchi kufanya transfer benki kupitia visa au mastercard, lakini kwa dunia ambayo tunayo leo watu wangependa kufanya transactions hizi wakiwa wana simu zao kiganjani. Vilevile ili uweze kufanya njia hizi za malipo yaani kama wewe ni mfanyabiashara wa Tanzania uweze kulipwa na mtu wa nje, kama sio kwa transfer za benki inabidi ulipwe kupitia application mbalimbali za fedha ambazo zinakusaidia uweze kupata malipo ya moja kwa moja. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa application hizi kwa hapa Tanzania wafanyabiashara wengi hawawezi kuzitumia kwa sababu ili application uweze kutumia makampuni yenye application hizo lazima ziwe zina leseni ambazo zimetolewa hapa Tanzania. Sasa jambo hili ni gumu kwa sababu makampuni haya ni giant companies, wana-own teknolojia kubwa sana, ni mabilionea hawawezi kuja ku-establish hapa makampuni yao kwa urahisi.

Kwa hiyo, sasa kinachotokea wafanyabiashara wengi waliokuwepo hapa wanapata ugumu wa kulipwa fedha, kwa hiyo, sisi tumegeuka wanunuzi. Kwa mfano, mojawapo ya application ni Pay Pal, mimi naweza kumlipa mtu wa nje, kama nauza bidhaa na huduma lakini mtu wa nje hawezi kunilipa mimi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nilipenda niliongelee hili ili Serikali sasa iweze kuona umuhimu wa kutunga/kubadilisha kanuni ili wafanyabiashara wa hapa ndani waweze kunufaika kwa namna moja ama nyingine. Unaweza ukadhani kwamba kwa sababu kanuni haziruhusu ama sheria haziruhusu basi wafanyabiashara hawa hawafanyi hizi biashara, kwa mfano PayPal watu wana account za PayPal, lakini wamezifungulia Kenya. Wanafungua na account za fedha Kenya, kwa hiyo, wanafanya malipo kupitia Kenya, kwa hiyo, fedha zinakwenda Kenya. Kwa hiyo, sasa mwisho wa siku sisi tunapoteza mapato na fedha za kigeni. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, badala ya ku-demand leseni kwa makampuni haya labda ni njia sahihi kwa Serikali kupitia Wizara ya Fedha ama BOT, kuweka kitengo maalum cha ku-scrutinize njia hizi za mifumo ya malipo ya kimtandao na kuweza kuishauri Serikali; ni njia gani kama Taifa na wafanyabiashara wanaweza kuchukua ili waweze kufanya biashara na Serikali itanufaika kupitia fedha za kigeni na itanufaika kupitia kodi ya ongezeko la thamani pale ambapo mfanyabiashara atatoa fedha kwenye application yake kwenda kwenye account zetu za hapa Tanzania. Kwa hiyo, vijana wa Taifa hili wanafanya ubunifu mbalimbali sana na siku hizi huduma za kiteknolojia wapo vijana wanauza online. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, ningependa kuishauri Serikali kama shida ni sheria nimeambiwa shida ni sheria na hizi license watuletee Kamati tuweze kufanya mabadiliko ili Watanzania vijana waweze kuuza biashara zao kwa urahisi. Leo unamuuzia mtu atoke huko nje alipo aende benki afanye transfer badala ya kulipa moja kwa moja kwenye simu yake. Kwa hiyo, hatuwezi kupigana na teknolojia, washauri wetu na wataalam kwenye Wizara watusaidie kuweza kuwaza mbele kuliko kusubiri teknolojia itufuate. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ahsante na naunga mkono hoja. (Makofi)