Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Hussein Mohamed Bashe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, kwanza nakushukuru kwa nafasi na pili naishukuru Kamati ya PAC kwa maoni. Specifically, kwenye eneo la kilimo kulikuwa kuna hoja kubwa mbili. Moja ni hoja ya vihenge na pili ni kuhusu NFRA.

Mheshimiwa Spika, Serikali baada ya kuona mradi wa vihenge umeanza kusuasua na kumekuwa sintofahamu, Serikali iliunda Government Negotiating Team na mwaka 2021 mimi mwenyewe nilishiriki; na wakati huo, Mheshimiwa Kitila akiwa Waziri wa Viwanda ndio alikuwa leader wa ile Kamati na mpaka sasa hivi ile Kamati ipo kazini, tumekutana na wenzetu wa Poland, tumekaa kujadiliana nao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nihakikishie Bunge lako Tukufu kwamba kutakuwa hakuna overspending juu ya framework iliyokuwepo awali. Siyo Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wala beneficiary ambaye ni NFRA haaja-violet mkataba kwa namna yoyote. Part ya YUNA, wenyewe wanaendelea na ujenzi. Sites zao tatu zimeshavuka 90%, wanaenda bila matatizo. Theorem ambaye ndio alikuwa na sites tano, alileta demand ya kuongezewa dola milioni 12 kwa sababu mbalimbali alizozitaka. Serikali imemwomba alete justification, ameshindwa, ameleta barua, anataka kujitoa kwenye ujenzi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, niwahakikishie Waheshimiwa Wabunge na Watanzania wote kwamba Serikali haitaenda kuingia additional cost kwenye mradi huu. Huu ni mkataba wa kukopa, hatupewi sadaka. Kwa hiyo, mkopo una framework, nasi tutausimamia kwa maslahi ya nchi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili ni kuhusu NFRA. Serikali ina njia nyingi ya kutoa fedha kuikabidhi taasisi. Moja, wanaweza wakatoa fedha ambazo wamezibajeti na vile vile unaweza ukachukuliwa mkopo. Mkopo wa NFRA ulitolewa under guarantee ya TR, ni mkopo wa Serikali. Ili usiwe mzigo kwa NFRA baada ya ile maturity ya OD kwisha, interest inabebwa na Serikali na wala siyo NFRA. Kwa hiyo, kutakuwa hakuna burden yoyote kwa NFRA kwa ile shilingi bilioni 50.

Mheshimiwa Spika, nasi kama Serikali tumeamua badala ya ile 15 billion ikifikia ku-mature, kuoandoa ile capital mkononi mwa NFRA, Wizara tutakuwa tunatenga kwenye bajeti yetu ile cost of financing, hii 50 million itaendelea kubaki NFRA na kuifanya NFRA kuwa na liquidity, wakati huo tunaiwekea bajeti ya kila mwaka na kufanya uwezo wa NFRA kuwa mkubwa (aggregative). Kwa sababu kuna njia mbili za NFRA anafanya; pale ambapo tunakuwa na dharura kama nchi, NFRA ndiyo ina jukumu la kutoa chakula cha msaada.

Mheshimiwa Spika, pale ambapo wakulima wanapata shida kuuza mazao, tunaitumia NFRA na CPD kama stabilizing instrument kuweza kwenda kuchukua mazao kwa subsidize rate. Kwa hiyo, naomba niwatoe hofu kwamba maamuzi ya Serikali baada ya Bunge kushauri kununua mazao ya wakulima ya mahindi na model iliyochukuliwa na Serikali ni njia sahihi ambayo haina hasara yoyote na ni njia salama ya capitalize taasisi nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nimalizie kusema tunashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa maoni yao, sisi tutapokea ushauri hasa kwenye eneo la mikataba. Mikataba yoyote tunayoingia hasa kwenye sekta ya kilimo niwahakikishie itakuwa ni mikataba kwa maslahi ya wakulima na wananchi na huu ndiyo mwelekeo na maagizo ya Mheshimiwa Rais, lazima kuwe na value for money kwenye any mkataba tunaoingia nao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru na ninaunga mkono hoja. (Makofi)