Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

NAIBU WAZIRI WA AFYA: Mheshimiwa Spika, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuchangia, nijikite kwenye ripoti ya Kamati kwenye eneo la Bohari ya Dawa. Kwanza niwashukuru kwa sababu wameonyesha kwamba hali ya dawa imeboreka na hasa baada ya Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kupeleka bilioni 333.8, lakini kuweka utaratibu ambao kila mwezi bilioni 15 zinakwenda Bohari ya Dawa na sasa hali inaendelea kuwa nzuri.

Mheshimiwa Spika, vile vile wamezungumzia kutokuwepo na viwanda vya kuzalisha dawa. Kwa rekodi nzuri ya Bunge kwa hii miezi ambayo Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan amekuwepo madarakani tumekwenda sasa kujenga Kiwanda cha Kuzalisha Dawa kule Njombe na kimefikia asilimia 70 ya ujenzi na kitaenda kuzalisha vidonge vya kutosha nchi nzima kwa siku mbili. Pia kinajengwa kiwanda cha kuzalisha gloves ambacho kitakidhi 85% ya nchi nzima.

Mheshimiwa Spika, Kiwanda chetu cha Keko kimeenda kufufuliwa na sasa kinafanya kazi na kinazalisha zaidi ya dawa 12 kwa sasa. Wakati huo huo kimeanzishwa Kiwanda cha Kuzalisha Mionzi Dawa ambacho kiwanda hicho kwa Afrika Mashariki ni sisi peke yetu tutaenda kuwa nacho na kwa Afrika kuna nchi tano tu ambazo zinamiliki kiwanda hicho. Maana yake ni nini, tulikuwa tunaagiza dawa kutoka Afrika Kusini, sasa tutakuwa tunapata dawa hapa hapa Tanzania na Nchi za Afrika Mashariki zitakuwa zinaagiza hapa nchini kwetu.

Mheshimiwa Spika, wamezungumzia suala la deni la MSD, ni kweli kulikuwa na deni la bilioni 281 na kulikuwa na kazi inayoendelea ya kuhakiki deni hilo. Kwa sababu kila wakihakiki wanakuta kuna kiasi kikubwa cha fedha ambacho kilikuwa siyo halali, kimeshahakikiwa kama milioni 90 na tayari zimelipwa bilioni 39. Wakahakiki tena bilioni 126 wakakuta kuna madeni feki bilioni 4.7 na hii bilioni 126 sasa inaenda kulipwa ambazo zimehakikiwa tayari.

Mheshimiwa Spika, ukizungumzia eneo la Bohari ya Dawa kwa maana nyingine huwezi kuzungumzia bila kuzungumzia uwajibikaji na utendaji mzuri kuanzia juu mpaka kufika chini. Nakumbuka Wabunge tuliripoti hapa kwenu na tukawaeleza jinsi ambavyo kulivyokuwa kuna upotevu wa dawa kwenye maeneo yetu. Tukitaka kweli tufike mahali dawa zipatikane kwa wingi, ni muhimu sana hili suala la kusimamia dawa liwe ni shirikishi, maana yake sasa tunatakiwa twende kujua vyanzo ambavyo vinafanya dawa zipatikane kwenye hospitali zetu za halmashauri na sehemu zingine na vyanzo kuna basket fund, kuna own source na MSD.

Mheshimiwa Spika, sasa wakati mwingine tulivyowaelezea upatikanaji wa dawa hapa kwetu jinsi tulivyoibiwa, tulichotaka ni kwamba tunataka tushuke mpaka chini Baraza la Madiwani na hata vituo vyetu kule chini watendaji na Wenyeviti wa Vijiji na Madiwani wawe ni sehemu ya kusimamia uadilifu huo na kupata ripoti zote zinazotokana na dawa ili tuweze kusimamia kwa umoja wetu.

Mheshimiwa Spika, nafikiri kwa upande wetu hayo ndiyo ambayo yalikuwa yanatuhusu sisi na majibu yake ni hayo. Niseme tu kwenye eneo hili la kuzalisha dawa maana yake tiba mionzi, Kamati yetu ya Bunge ya Huduma za Jamii iliomba ikifika asilimia 80 ya ujenzi wa hicho kiwanda watembelee na asilimia 80 ya hicho kiwanda imefika na tumeshaandika barua kwako kwa ajili ya Kamati ya Bunge kutembelea kukiangalia kile kiwanda.

Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. (Makofi)