Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Tauhida Cassian Gallos Nyimbo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. TAUHIDA C. GALLOS: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa fursa hii kuweza kuchangia. Kwanza kabisa, nianze kwa kukupongeza wewe mwenyewe binafsi kwa kuteuliza na chama chako, Chama cha Mapinduzi, lakini vilevile kuweza kupata kura za kishindo kwa Wabunge. Sambamba na pongezi hizo nimpongeze Naibu wako ambaye ni msaidizi wako kwa kuchaguliwa pia naye na Wabunge kwa kura nyingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mchango wangu nitajielekeza kwenye matumizi ya miradi ya halmashauri. Halmashauri imekuwa na kipindi cha utekelezaji wa fedha. Kulikuwa na mambo kadhaa sugu ambayo yanaisumbua halmashauri. Kwanza, tulikwenda na tulipita kwenye awamu ya Wanasheria ambao walikuwa wakisababisha matatizo makubwa ndani ya halmashauri zetu. Tulipotoka hapo tukaja na ugonjwa wa Mfuko wa asilimia 10 ambao haukuwa na usimamizi mzuri; kwa sehemu haujapona moja kwa moja, lakini kwa sehemu kidogo kuna unafuu si asilimia 100 lakini asilimia zaidi ya 60 kidogo mabadiliko yapo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kuna ugonjwa ambao kwa sasa unasumbua Halmashauri zetu. Ugonjwa huo ni matumizi mabaya ya fedha; kuchukua fedha za Halmashauri kuwekeza kwenye majengo na kutokuyamaliza. Ugonjwa huu umekuwa tatizo ndani ya Halmashauri zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, fedha nyingi za wananchi zinazokusanywa kwa kodi zinaenda kutengenezwa miradi ambayo haiishi, inakaa zaidi ya miaka mitatu mpaka mitano bila ya kumalizika. Nitoe mfano kama wa Halmashauri Tatu ya toka mwaka 2012; kuna Bwalo la Chakula, Chamwino; mradi wa Babati Mjini - nyumba za Waganga; mradi wa ukumbi - Mpwapwa. Hiyo ni baadhi ya miradi ambayo ndani ya Halmashauri zetu zimetumia fedha nyingi lakini miradi haikumalizwa.

Mheshimiwa Spika, kuna aina za miradi ndani ya Halmashauri zetu; kuna miradi ya Serikali, kuna miradi ya wananchi na miradi ya watendaji. Miradi ya Watendaji mara nyingi huwa haiishi, kwa sababu huwa na miradi yenye fedha nyingi ambayo haiihitajiki na wananchi, siyo malengo ya wananchi, siyo mtazamo wa Serikali; nao huianzisha miradi ile iwe ni njia au kichochoro cha kufanikisha mambo yao. Zinachukuliwa fedha kwa mamilioni lakini bado unakuta zimeenda kutumbukizwa sehemu toka mwaka 2012 na ipo miradi mingine zaidi ya mwaka 2012 haimalizwi.

Mheshimiwa Spika, imebidi sasa tuiwekee mkazo. Mheshimiwa Rais wetu amekuwa mfano kwenye miradi. Tuchukulie mfano wa reli ambao sasa hivi unamaliziwa na Mheshimiwa Rais na bado anapeleka fedha kumaliza miradi hii. Kama ni miradi ambayo ina malengo na inahitajika kwa wananchi sielewi kuna tatizo gani la Halmashauri kila mwaka wanatenga fedha kuanzisha miradi mipya na miradi mingine kuendelea kubaki ikiwa ni miradi ambayo haifanyiwi kazi na pesa ya wananchi inapotea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, miradi mikubwa inayohitajika kwa wananchi ni hospitali, shule; hiyo ndiyo miradi wanayoihitaji wananchi. Leo unaenda kuchukua fedha unaipeleka Mpwapwa unaenda kuweka hall unategemea mtu wa Mpwawa kumkodisha hall akafanye shughuli kwa shilingi milioni tatu, itaingiza wapi fedha hizo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, chukulia inaenda kujengwa nyumba ya Mganga vyumba vitatu, inachukua miaka minne bila kwisha, lakini fedha ya wananchi ipo pale tayari imeshakaa. Tunaishauri Serikali kuondokana na matumizi mabaya ya fedha ambapo wananchi wanazihitaji na wanahitaji zifanyiwe kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naomba kuchukua fursa hii kuunga mkono hoja ya Kamati yetu ya LAAC. (Makofi)