Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ili niweze kuchangia kwenye hoja zilizopo hapo mezani. Kwanza kabisa niungane na wenzangu kukupongeza kwa nafasi hii ya kuwa Spika wa Bunge pia nimpongeze Naibu Spika. Lakini kwa namna ya pekee nizipongeze oversite committee zote kwa maana ya PAC na LAAC kwa presentation ya Wenyeviti wake wamefanya presentation nzuri sana niwapongeze sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, leo nitajikita kuchangia hasa kwenye benki zetu za Serikali nataka nielezee going concern ya benki zetu za Serikali. Serikali kuwa na benki zake yenyewe ni jambo muhimu sana, lakini kuanzia mwaka, 2017 Serikali ilichukua uamuzi wa kuunganisha benki zake. Kwanza, ilianza kuichukua TWIGA kuiunganisha na Benki ya Posta; baadaye ikaja kuchukua Benki ya Wanawake ikaiunganisha mwaka, 2018 na Benki ya TPB. Shida kubwa hizi major mbili hazikuwa na tatizo kubwa shida kubwa ilikuja pale ambapo, Serikali iliamua kuchukua benki ya TIB Corporate na kuiunganisha na Benki ya TPB ili kuunda Benki ya TCB ambayo ni Benki ya Biashara ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lengo lilikuwa ni zuri labda tulikuwa tuna-revert will yetu ya kubinafsisha Benki ya NBC ili tuwe na Benki ya Biashara ya kwetu ya Serikali, lakini kitendo cha kuileta TIB Corporate tayari ilikuwa na mikopo chechefu ya Shilingi bilioni 130, hii imekuja kuharibu mizania ya vitabu vya, Benki hii ya TPB ambayo ilikuwa tayari ipo kwenye top ten ya benki zinazofanya vizuri hapa nchini. Kwa sababu, tuna benki sasa zaidi ya 50 lakini benki yetu ya Serikali ya TPB ilikuwa ina- perform vizuri. Kuleta kwa mikopo chechefu na pia ikaleta mzigo wa wastaafu kwa maana ya staff management team ile ambayo ilikuwa na mishahara mikubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, mpaka leo kutokana na ofisi ya Treasurer kuto-solve huu mtanziko pale ndani ya benki ni kama kuna management mbili. Kuna wale waliotoka TIB Corporate ambao wage bill yao kwa mwezi inakwenda, 1.7 billion shillings ambao kazi kubwa inayokwenda pale ni kusoma magazeti. Unalipa shilingi 1.7 billion kwa mwaka fedha za walipa kodi hawajapangiwa majukumu, sasa inaonekana Serikali kupitia Ofisi ya Msajili wa Hazina hawakujipanga wakati wanafanya hii merger. Ilitakiwa watumie approach ile waliyofanya wakati wanabinafsisha ile Benki ya NBC, walichukua madeni na mali zile ambazo, wale makaburu hawakuzitaka, wakaunda Shirika pembeni tanzu la CSC kwa ajili ya ku-deal na yale mambo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa huku approach ilikuwa wakapeleka madeni mabaya Shilingi bilioni 130 na Treasurer aliji-commit kwamba huu mzigo nitaubeba. Tangu Juni, 2020 ameweza ku-recover Shilingi bilioni tatu tu, kwa hiyo itamchukua zaidi ya miaka 40 ku-recover ile mikopo chechefu. Ile mikopo mingi, ukiiona haina future yoyote, mikopo ile yote yawezekana hata Serikali isiweze ku-recover zile fedha. Sasa, naomba kuishauri Serikali kuna approach mbili ambazo unaweza kutumia kuisaidia benki hii, ambayo ina matawi 83 na ina wakala wa benki zaidi ya 3,500 nchi nzima na ni benki ambayo tunaitegemea kama Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, jambo la kwanza; wakubali kuchukua ile mikopo iondoke kwenye mizania ya vitabu vya Benki ile ya TCB. Pili, hawa management ambao wanalipwa Shilingi 1.7 billion na wapo tu wanasoma magazeti, watafutiwe sehemu nyingine ndani ya Serikali, kuna mamlaka nyingi, wakafanye kazi, kuliko kutumia fedha za walipa kodi hawafanyi kazi yoyote. Hii contradiction tu ni basi tu katika making decision, ilitakiwa siku ile tu ya merger wawe wameamua hili jambo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatu, tuna benki yetu nyingine kubwa kabisa Benki ya Maendeleo ambayo ni TIB Development katika nchi yoyote ile kwa mfano China Development Bank. Hii China Development Bank ndio ina- finance miradi yote mikubwa ya kimkakati ndani ya nchi ya China, lakini sisi hii TIB Development alipoianzisha Mwalimu Nyerere mwaka 1970 alikuwa na nia njema. Kukaingia ulaghai na ujanja ujanja mpaka ninaposema leo hii mikopo chechefu imefika Shilingi bilioni 327 na kila mwaka wakijitahidi wanakusanya labda shilingi bilioni mbili au tatu. Maana yake hata benki hii leo hii ukienda wame-stop lending hawakopeshi, kwa sababu, fedha ina liquidity crisis maana yake ni nini kinachoweza kutokea hapo?

Mheshimiwa Spika, wamesema watatoa non cash bond. Noncash bond ni kwenda tu kuweka mizania ya vitabu ikae vizuri, lakini hai-address tatizo la mtaji la benki hii. Ina mtaji wa Shilingi bilioni 38, lakini requirement ya Benki Kuu inatakiwa Benki aina ile ya TIB Development iwe na mtaji wa shilingi bilioni 50. Sasa, leo hii unakwenda kufanya non cash bond ambayo pia inakwenda na impact kwenye deni la Taifa, tayari hata TCB wanasema, wanakwenda kuweka non cash bond, yes ni initiative ya kuweka mizania ya vitabu, isome vizuri, lakini hai-address matatizo ya benki zetu hizi za Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, Serikali kama inataka kweli twende mbele kwenye financial sector na hapa sijaongelea Benki ya Maendeleo ya Kilimo nayo hali ni hii hii. Maana yake sisi ndio tuna-prove failure; Benki Kuu inasema asilimia tano ya non-performing loan against assets zako ndio inatakiwa, lakini sisi kwa mfano, TIB leo mikopo chechefu ni zaidi ya asilimia 50 wakati inatakiwa iwe asilimia tano, tunakwenda wapi tumeamua kuua benki zetu wenyewe. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa sababu ya muda niishie hapa. Ahsante sana. (Makofi)