Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Spika, ahsante awali ya yote niungane na wenzangu kukupongeza wewe kwa kuchaguliwa na Bunge hili kuwa Spika wetu na kwa kweli sisi Wabunge tuna imani kubwa. Tunaomba Mungu akusimamie. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya pongezi hizo ambazo pia zimfikie Mheshimiwa Zungu Naibu Spika, nianze sasa kwa kuchangia hoja au taarifa ya Kamati ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kama ambavyo imewasilishwa na Mwenyekiti wetu, mama Grace Tendega, ikiwa ni hesabu za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali katika Mamlaka za Serikali za Mitaa kuishia mwezi Juni, 2020. Ni ukweli kwamba Serikali imekuwa na juhudi za dhati kabisa kupeleka fedha katika Mamlaka za Serikali za Mitaa, kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ikiwemo sekta ya afya, sekta ya elimu na sekta nyinginezo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pia kumekuwa na utaratibu wa kupeleka fedha kwa utaratibu wa flat rate kwa kila halmashauri, kwa mfano, Serikali imekuwa ikipeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni kwenye shule zetu za sekondari. Hapo awali ilikuwa ni Shilingi milioni 75 na baadaye ikawa ni shilingi milioni 80, lakini kumekuwa na namna tofauti tofauti katika utekelezaji wa eneo hili.

Mheshimiwa Spika, katika baadhi ya halmashauri Shilingi milioni 80 imetosheleza kabisa kujenga bweni moja la wanafunzi kukaa idadi ya watoto 80 ikiwemo facilities za ndani ya bweni hilo, kwa maana ya vitanda, lakini katika baadhi ya halmashauri shilingi milioni 80 hazijatosha na hakuna ambacho kimefanyika na kazi haina viwango. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, katika hili nina maeneo mawili ya kuzungumzia. Eneo la kwanza ni kuwapongeza wale ambao kwa dhati kabisa wamefanya vizuri ikiwemo, halmashauri ya Wanging’ombe ambayo ni Jimbo la Mheshimiwa Festo Dugange. Wamejenga shule, wamejenga mabweni kule katika Sekondari ya Wanging’ombe, wamejenga bweni katika Sekondari ya Wanike kwa Shilingi milioni 75 na imetosheleza hakuna namna yoyote ya harufu ya ubadhirifu wa fedha. Hata hivyo, katika halmashauri zingine shilingi milioni 80 imezama, mabweni hayajakamilika, vitanda hakuna na bado fedha haitoshelezi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hiki ni kiashiria tosha kabisa kuna mazingira ya dalili ya matumizi mabaya ya fedha hizi za umma. Katika hili niseme pia kwamba Serikali imekuwa ikipeleka fedha hizi bila kufanya tathmini ya kina. Katika maeneo mengine ni kweli kumekuwa na dalili za ubadhirifu lakini katika mazingira mengine ambapo facilities zote ikiwemo bidhaa za madukani, zinapatikana kwa urahisi na zile bidhaa ambazo zinapatikana kwenye mazingira halisi ikiwemo mchanga, mawe, kokoto zinapatikana, bado fedha hizi hazijatosha.

Mheshimiwa Spika, sasa niseme tu kwamba wakati Serikali ili kuzipunguzia mzigo wa hoja halmashauri zetu, zinapeleka fedha hizi kwa utaratibu huu wa flat rate, zingefanya kwanza tathmini ya kimazingira ili kujua kila halmashauri na kila maeneo yanahitaji shilingi ngapi? Kwa mfano, katika baadhi ya halmashauri zimekuwa mbali na maeneo ambayo bidhaa za viwandani zinapatikana. Huwezi ukapeleka utaratibu wa flat rate na wakafanya kama vile ambavyo wangeweza kufanya vingine kwa vizuri zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kutoa ushauri huu, niunge mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)