Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa (LAAC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, awali ya yote nianze kwa kukupongeza wewe binafsi kwa kuteuliwa kuwa Spika wa Bunge. Lakini nijielekeze kwa sababu muda ni mchache. Ni dhahiri kwamba maendeleo ya nchi yoyote yanahitaji umeme, ni dhahiri kama tunahitaji kufikia uchumi wa kati ambao tumekuwa tukiusema, tunahitaji upatikanaji usiosuasua wa nishati ya umeme. Wabunge wenzangu wamekuwa wakichangia mara kadhaa hapa wakiongelea changamoto ya umeme. Nitaiongelea hususan kutokana na taarifa ya Kamati ilivyoieleza hasa suala zima la TANESCO. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, TANESCO ina changamoto kubwa ya fedha, inakabiliwa na madeni makubwa, inadai na inadaiwa. Ukisoma taarifa ya CAG inaeleza si tu kwamba inachangamoto ya fedha lakini pia ina mtaji ambao ni negative yaani working capital ni negative. Ukiangalia uwiano nasoma kwenye taarifa Kamati ya PAC na nianze kwa kumpongeza Mwenyekiti mwana mama amewasilisha vizuri sana. Ahsante sana Mwenyekiti wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ukisoma ukurasa wa 26 wanaeleza uchambuzi wa vigezo mbalimbali vya tathmini ya hali fedha TANESCO. Anaeleza uwiano wa mali na madeni ya TANESCO. Anaeleza kwamba uwiano wa mali ambayo kwa kulipa zile fedha ambazo zinaweza kuwa zimeiva current ratio yake, mali ni trilioni 1.4, madeni ni trilioni 2.7. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hiyo ni fedha ambazo zinahitaji kama zikiwiva kwa muda mfupi illipe, kwa hiyo automatic TANESCO haiwezi ku-meet expense zake za mwaka lazima ipeleke mwaka unaofuata au illipe riba au interest. Lakini siyo hiyo uwiano wa ukwasi liquidity. Liquidity ya TANESCO mali za muda mfupi trilioni 1.4, madeni trilioni 2.761 hiyo ni TANESCO.

Mheshimiwa Spika, lakini tunakwenda kwa mtaji working capital, uchukue zile current asset kwamba zile fedha walizonazo fedha zake na mali inakuja ni trilioni 1.27, ije kwenye madeni trilioni 2.76 kwa hiyo, unakuja kupata TANESCO inajiendesha kwa negative trillion 1.296. kwa hiyo tunakata ifanye nini? Tunaweza kuwa na mipango mikubwa ya kuongeza nishati na tumeona juhudi zikifanywa na Serikali lakini shirika ambalo limekasimiwa mamlaka ya kununua na kusambaza umeme kama inajiendesha kwa hasara tujue kwamba changamoto ni kubwa.

Mheshimiwa Spika, siyo hiyo tu, nimepitia nimeona madeni TANESCO inadaiwa na Songas Capacity Agency zaidi ya bililioni 293 ameeleza hapa Mwenyekiti wa Kamati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini siyo hiyo tu na kwa sababu haijalipa kwa wakati hivyo imepigwa riba ya zaidi ya bilioni 62 hiyo hiyo TANESCO ila cha kushangaza TANESCO hiyo hiyo inaidai taasisi mbalimbali za Serikali zaidi ya bilioni 422. Kwa hiyo, yenyewe ipo ina suffer lakini na wadeni wake ambao hawailipi. Kuna taasisi mbalimbali za Serikali ambazo zimekuwa zikitumia huduma na hazilipi kwa wakati. Nitoe rai kwa Serikali, hebu hizo taasisi kwa sababu zinakuwa zinapewa ruzuku walipe fedha ili TANESCO iweze kujiendesha. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama tunataka kuona hayo mabadiliko na mabadiliko chanya ya usambazaji wa umeme tuiwezeshe TANESCO. Tuhakikishe kwamba ina-working capital ya kutosha tuhakikishe kwamba inaweza ku-meet obligation zake za day to day, kwa sababu, mwisho wa siku changamoto kubwa inatokana na riba ambayo imekuwa inapigwa mara kwa mara kwa sababu haiwezi kulipa fedha zake kwa wakati. Hiyo nitaongelea bila kusahau TANESCO na yenyewe imekuwa na madudu yake.

Mheshimiwa Spika, TANESCO iliingia mkataba mwaka, 2007 na Kampuni moja ambayo ni ya Madini ambayo sasa katika huo mkataba TANESCO ilipaswa kuwa inakusanya fedha, kutoka kwenye hiyo Kampuni ya Buzwagi inaweka kwenye a certain account kwa ajili ya kufanya maintenance. Imekuwa haifanyi hivyo for over ten years, ina maana wewe ukaona kwamba mbali na kwamba ina changamoto ya fedha lakini pia, kuna changamoto ya uzembe ambayo TANESCO lazima wasemwe na mamlaka lazima zisimamie kuona inaweza kutimiza vigezo na masharti yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, hayo ni machache ambayo naweza kuyasema na kwa sababu ya muda niongelee kidogo issue ya NIDA.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Muda umekwisha nakushukuru. (Makofi)