Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi kuchangia katika taarifa hizi za kamati hizi mbili ambazo zimeletwa mbele ya Bunge lako. Kuna mengi yameongelewa ambayo ni ya kujenga kwa hiyo niendelee kushukuru kwa michango mizuri ya Waheshimiwa Wabunge lakini mahususi kwa kamati hizi mbili ambazo zinaendelea kuhisimamia na kuielekeza Serikali katika kutekeleza majukumu yake mbalimbali.

Mheshimiwa Naibu Spika, yameongelewa mengi lakini kubwa ni kuona namna gani kuboresha au kuziwezesha taasisi ambazo zinatoa huduma katika maeneo tofauti tofauti ikiwemo taasisi yetu ya ABZA CAMATEC, SIDO, TEMDO, TIC na taasisi zingine ili ziweze kutekeleza majukumu yake kwa ukamilifu. Tunachukua mawazo haya ya Waheshimiwa Wabunge lakini kamati hizi mbili kwa umakini mkubwa kuhakikisha kwamba tunatekeleza majukumu hayo ili tuweze kunufaisha Taifa hili kupitia huduma zinazotolewa katika Taasisi hizi.

Mheshimiwa Naibu Spika, imeongelewa suala la utekelezaji wa Blue Print ambalo Mheshimiwa Tarimba amemalizia sasa Serikali inaendelea kuhakikisha kutekeleza hilo lakini tunaangalia na mapungufu mengine ambayo yanaendelea kujitokeza wakati tunatekeleza. Siyo kweli kwamba tunafungia katika kabati lakini tunaendelea kutekeleza hatua kwa hatua na nikuhakikishie Bunge lako liwe na imani nia ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wetu mpendwa Samia Suluhu Hassan ni kuona tunaweka mazingira wezeshi na bora Zaidi ili kuwahakikisha sekta binafsi inakuwa ni kiongozi katika kujenga uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kumeongelewa mambo mengi kuhusiana na miradi ya kimkakati ambayo inatekelezwa chini ya Taasisi zetu. Serikali inaendelea kufanya bidi na haraka zaidi lakini kwa uweledi ili miradi hiyo iweze kutekelezwa kwa haraka lakini kwa tija kwa ajili ya maendeleo ya Taifa. Imeongelewa miradi ya Mchuchuma na Linganga, lakini kuhusu viuwadudu na mengine tutahakikisha tunatekeleza miradi hii kwa uweledi lakini kuona maslahi mabana ya nchi yanazingatiwa.

Mheshimiwa Naibu Spika, sisi kama Serikali tunachukua maoni yote na tuhakikishie Waheshimiwa Wabunge lakini kamati zetu mbili ambazo zinatusimamia kwamba tutatekeleza maoni yao na ushauri wao na tutaendelea kushirikiana nao kuhakikisha wanatekeleza majukumu ya kila siku.

Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuchangia kamati hizi mbili. (Makofi)