Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa ajili ya kunipa nafasi ya kuchangia hoja zote mbili. Mashirika mengi ya umma hayafanyi vizuri yote ambayo tumeyapitia hayafanyi vizuri kabisa na hasa katika maeneo yafuatayo. Kwanza mashirika mengi ya umma yanadaiwa yana mzigo mkubwa sana wa madeni.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia mashirika haya hayana uwezo wa kukusanya madeni yao, unakuta shirika linadaiwa lakini pia linawadai watu pesa nyingi sana na mimi nitatoa mfano hapa mmoja Shirika la SIDO. SIDO lina mzigo mkubwa sana wa madeni mwaka 2018/2019 ilikuwa inadaiwa bilioni 4.7 lakini 2019/2020 deni lake limefikia bilioni 8 ongezeko la 77% unaangalia unaona kwamba sasa hili deni wanadai bilioni 5 wao wangekusanya hizo bilioni 5 wangeweza ku- offset hili deni angalau lingekuwa limebaki kidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini hawana uwezo wa kukusanya madeni yao lakini vilevile hawana uwezo wa kulipa madeni yao, na Shirika hili tunalitarajia sana lingeweza kuwa mkombozi wa uchumi wa nchi hii kwa sababu kazi yake kubwa ni ku-support viwanda vidogo vidogo. Lakini kama linaendeshwa katika mtindo huu, haliwezi kuleta tija yoyoe inayokusudiwa. Serikali lazima iangalie sana kwa ukaribu uendeshaji wa shirika hili kupitia ofisi ya msajili. Bila hivyo hii SIDO haitokuwa na maana yoyote Serikali itaendelea kutoa ruzuku na itaendeshwa na itapotea.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano mwaka 2018/ 2019 Shirika lilitengeneza faida ya bilioni 1.56 lakini 2019/2020 limetengeneza hasara ya bilioni 2 sasa unaweza kuona uendeshaji wa namna hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, nilikuwa nashauri sana Mashirika haya yajitahidi sana kwanza yawe na utamaduni wa kulipa madeni yao mara wanapopata huduma au wanapofanya biashara walipe madeni hata kama kwa kidogo kidogo. Pia wawe na mikakati mahsusi ya kukusanya madeni kwa wale wanaowadai hiyo itawasaidia kuendesha mashirika yao vizuri.

Mheshimiwa Naibu Spika, pia matumizi sheria imewekwa ya fedha Na. 16 ya mwaka 2015 ambayo inaweka ukomo wa kutumia mwisho 60% kuna kitu gani mashirika mengi yamepita 60% kuna tatizo gani katika Serikali kuhakikisha kwamba inasimamia hii sheria kila shirika likaenda kama sheria inavyotaka. Kwa sababu kila shirika unaloliona utakuta limevuka hiyo sheria limevuka huo ukomo wa 60% kwa nini Serikali haisimamii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nashauri sana Serikali kupitia Msajili wa Hazina mashirika haya yabanwe yaweze kutekeleza sheria hii ya fedha Na. 16 hii itasaidia hata matumizi yale yasiyo ya lazima yataweza kuepukwa. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pia tuna shida ya miradi mingi kutokukamilika kwa wakati lakini ukiangalia sababu kubwa ziko moja kwanza ni michakato mingi kila wakati shirika liko kwenye mchakato mipango iko kwenye mchakato litaanza yako mashirika tumeyakuta wana miradi imepita hata miaka 10 haijakamilika. Mfano hata mradi wa Liganga na Mchuchuma kila wakati mnaambiwa michakato inaendelea, lakini pia Serikali haitoi maamuzi kwa wakati au haitoi maamuzi mapema kwamba mradi huu uanze wakati fulani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nayo ni shida nyingine kwamba maamuzi hayafanyiki halafu fedha zinaendelea kutumika mradi haujaanza na hizi fedha za wananchi walipa kodi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, lingine hata ile iliyoanza kidogo Serikali haipeleki fedha ili miradi ile iendelee kutekelezwa kwa wakati. Kwa hiyo, tuna tatizo hilo kwamba mashirika yetu tusipokuwa waangalifu hayawezi kutuletea tija tunayoikusudia. Tunategemea kila shirika liwe na uwezo wa kutoa mchango katika mfuko mkuu wa Serikali. Lakini sasa hivi mengi hayana huo uwezo ama yanachangia kidogo sana ama mengine hayachangii kabisa lakini kwa sababu hatujawa serious katika maeneo haya. Mashirika haya lazima tuyasimamie vizuri tukitaka tukuze uchumi wa nchi hii tukitaka tupate tija, tukitaka Serikali ipate gawio ni lazima tuwe na utaratibu wa kuyasimamia kwa karibu. Serikali, TR lazima isimamie.

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo naunga mkono hoja ahsante sana. (Makofi)