Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Dr. Oscar Ishengoma Kikoyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba kusini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma (PIC) kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. DKT. OSCAR I. KIKOYO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Nami niungane na Wabunge wengine kukupongeza kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ni Mjumbe wa Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma. Katika ripoti yetu tumeangalia mashirika mengi, lakini nasikitika kusema mashirika yetu mengi hayafanyi kazi vizuri. Tatizo mojawapo, katika ripoti yetu tumeainisha, ukosefu wa mtaji ni tatizo kubwa kwenye mashirika yetu na nijikite kwenye TPA.

Mheshimiwa Naibu Spika, TPA kwa uchumi wa nchi yetu na kulingana na jiografia yetu na nchi zinazotuzunguka, kusema kweli ni cash cow yetu. Hata hivyo, ukiangalia mtaji walionao na uwekezaji wetu na jiografia yetu, nchi zilizotuzunguka zinazohitaji huduma yetu, kulingana na ripoti yetu ambayo tumewasilisha hapa, tumesema TPA utendaji kazi wake ni mdogo kwa sababu hawana mtaji wa kutosha.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia vifaa walivyonavyo ni vya karne iliyopita, siyo vya karne hii. Tanzania siyo peke yetu; au Bandari ya Dar es Salaam siyo peke yake katika ukanda huu. Tunazo bandari nyingi ambazo tunashindana nazo. Kama tuna vifaa hafifu ambavyo vina teknolojia hafifu, hatuwezi kushindana na bandari za nchi zilizo karibu kwenye ukanda huu wa Afrika Mashariki na Kusini mwa Afrika. Tutaachwa nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, napendekeza, Serikali i- commit hela ya kutosha kwenye Bandari ya Dar es Salaam ili tuweze kuhudumia mizigo ambayo nchi jirani wanapitisha kwetu. Vinginevyo washindani wetu watatuacha nyuma. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, la pili, bandari hiyo ina upungufu mkubwa wa wafanyakazi. Ikama yao ni wafanyakazi 3,196, lakini waliopo mpaka leo tunapoongea ni wafanyakazi 2,512. Wanao upungufu wa wafanyakazi 1,404 tunashindwa wapi? Kama hiki ndicho kitega uchumi cha uhakika tulichonacho, tukiwekeza vya kutosha, tuna uhakika wa kutengeneza fedha za kutosha kutusaidia kupunguza matatizo kwenye bajeti yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukishakuwa na wafanyakazi wachache, ukawa na mtaji mdogo, madhara yake ni kwamba tunatumia muda mwingi kuhudumia meli na matokeo yake hawa tunaowachelewesha kupakua mizigo yao, tunawalipa fidia na hizo gharama zote zinapelekwa kwa mlaji na matokeo yake ni nini? Bidhaa inayopitia kwenye Bandari ya Dar es Salaam haiwezi kushindana na bidhaa nyingine. Itakuwa ni ya bei ya juu sana. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimalizie na Taasisi inayoitwa TASAC. Wakati Sheria ya TASAC inapitishwa hapa, wengi tuliipigia kelele, lakini tukaipitisha kama Bunge. TASAC anafanya kazi ya udhibiti, lakini wakati huo huo anafanya kazi ya kutoa huduma.

Mheshimiwa Naibu Spika, haiwezekani hii. Kwetu huku tunasema ni sawa sawa na kuchukua rubisi ukachanganya na konyagi, haiwezekani. Kama ni mdhibiti, afanye kazi ya udhibiti na tuunde taasisi nyingine ya kufanya biashara ambayo inafanywa na TASAC. Mdhibiti afanye kazi ya udhibiti na tuwe na kampuni nyingine tofauti na TASAC ambayo itafanya kazi ya clearance, kazi za kusafirisha kidogo kidogo na kutoa mizigo, lakini hizi kazi mbili lazima tuzitenganishe, hatuwezi kuendelea hivi. Vinginevyo tunabaki kama kichekesho tu katika uchumi wa soko. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, naunga hoja mkono. (Makofi)