Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Dr. Stephen Lemomo Kiruswa Mamasita

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Longido

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuchangia hoja iliyopo mezani ya taarifa hizi zilizoletwa na Kamati zetu. Nikijielekeza kwenye Kamati ya Nishati na Madini, nitumie fursa hii kuwapongeza sana Wanakamati kwa kazi nzuri mno na ripoti nzuri ambayo wametuletea sisi kama Serikali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika taarifa waliyoileta wameleta mapendekezo na maoni yao mbalimbali. Nitumie fursa hii kusema kwamba sisi kama wizara tumeyachukua yote na tutakwenda kuyafanyia kazi na tutaleta mrejesho unaoeleweka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kwenye mapendekezo ya taarifa hii ya Kamati masuala mbalimbali yamejitokeza. Kwa mfano, wameelezea suala la STAMICO kwamba STAMICO ijikite katika uwekezaji wa mambo machache lakini yenye tija. Hili sisi tunalichukua kama Wizara tutaenda kulifanyia kazi kwa sababu tayari STAMICO ni moja ya taasisi zetu muhimu sana katika kufanikisha ukuzaji wa sekta ya madini. Hivi sasa STAMICO wanaendelea kujikuza kuongeza mitambo ya kisasa zaidi, kuongeza ujuzi zaidi na wameleta hata kuwekeza katika kutafuta mitambo ya kuwasaidia wachimbaji wadogo. Kwa hiyo, hili tunalibeba kwa uzito wake na tutalifanyia kazi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kulikuwa na suala lingine la mambo ya PPRA kwamba Kamati kweli imeona umuhimu wa STAMICO kuongeza kasi ya utendaji iweze kuwa shindani katika soko; maana yake kuna kampuni za binafsi pia zinafanya kazi za uchorongaji, utafiti, ni kweli na sisi tunalipokea hili na kama Wizara tutaendelea kuijengea uwezo na kwa sababu mfumo wa PPRA unahusika na ununuzi wa umma procurement, nadhani hili ni suala nyeti ambalo tutahitaji kukaa na wenzetu wa Wizara husika tuangalie namna ambavyo watawasaidia STAMICO nao waende kwa kasi. Maana procurement zingine zinachukua muda na wanapitwa na kandarasi ambazo zingewaongezea mapato na Shirika letu la STAMICO liendelee kuonekana kama ni shirika la kibiashara.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia taarifa ya Kamati tunapokea tu yale ambayo wameleta tutayafanyia kazi nataka tu wajue kwamba tumeyapokea yote, lakini kwa upande wa utitiri wa tozo mbalimbali, ada zinazotozwa hasa kwa wachimbaji wadogo. Sisi tumelipokea hilo na Wizara tayari imeweka mikakati madhubuti ya kuhakikisha kwamba tutakaa na wenzetu wa Wizara ya Fedha na Mipango pamoja na taasisi yao TRA tuangalie ni tozo zipi, kodi zipi ambazo zinakwenda kukwamisha ukuaji wa sekta ya uchimbaji wa madini hasa wachimbaji wadogo. Hilo pia tumelipokea kwa uzito wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mfano tu wa kwamba Serikali inasikiliza. Katika awamu iliyopita kabla mimi sijaingia kwenye nafasi hii, kuna wakati hata baadhi ya kodi ziliondolewa, kama ile VAT ya asilimia 18 kwa wachimbaji wadogo iliondolewa, ikaondolewa pia kodi ya zuio, withholding tax ya asilimia tano na kuna utitiri wa kodi nyingine ambazo bado tutakwenda kuendelea kuzifanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kupokea hii Taarifa ya Kamati walipendekeza kwamba Tume ya Madini iendelee kuongezewa uwezo au tuseme tu taasisi zote za Wizara ya Madini maana tuna Tume ya Madini, STAMICO, TEITI, Geological Survey of Tanzania – GST na hawa wote wana changamoto za upungufu wa wafanyakazi, kuna watu wanaokaimu, wanahitaji kuongezewa bajeti. Haya yote tumeyachukua na tunakwenda kuyafanyia kazi na taarifa ya Wizara itatoka na hoja za Waheshimiwa Wabunge zitajibiwa kikamilifu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine muhimu ambalo limejitokeza ni hili la TASAC. TASAC kwa sababu ni Taasisi ya Uwakala ambayo ndiyo inayopitishiwa madini yanayokwenda nje ya nchi. Ni kweli taarifa ya Kamati imethibitisha kwamba watu wanapokuwa wametoa madini yao kule migodini wanakuwa wameshalipia kodi nyingi nyingi inapofika kwenye port of exit iwe ni uwanja wa ndege, bandarini basi unakuta wanalazimika tena kulipia kodi. Hili nalo tumelichukua na tutakwenda kulifanyia kazi. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana.

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana na naunga mkono hoja. (Makofi)