Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Jesca Jonathani Msambatavangu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Iringa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. JESCA J. MSAMBATAVANGU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nashukuru kwa kunipa nafasi. Nitaanza na Wizara ya Miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niishukuru Serikali kwa kazi kubwa inayofanya katika kutujengea miundombinu. Lakini ninaomba tu, tulikuwa tumepitisha hapa mpango wa miaka mitano na tukaomba wenzetu waweke kipaumbele katika kuimarisha miundombinu inayoelekea kwenye miradi ya kimkakati ikiwepo Ruaha National Park.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jamani sisi Iringa tupo tayari kuwajaza dollar, kuwajaza pound sterling, kuwajaza ma-euro, lakini utelezi unatokea Wizara ya Miundombinu. Tunaomba barabara zile zinazoinga Ruaha National Park zifikike, tujengewe kwa kiwango cha lami. Ili tazalishe madola tutatue matatizo mengine ya sehemu zingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naingia Wizara ya Nishati na Madini, nitaanza na Shirika la STAMICO. Tunaomba sana STAMICO tuwapongeze kwa kazi nzuri mnayofanya, na limekuwa ni shirika sasa ambalo linakwenda kujitegemea baada ya kuwa ICU muda mrefu. Lakini sasa tumejitahidi kuweka maafisa madini kwenye kila mkoa, na tumejitahidi kutanua wigo wa ulipaji madini mpaka kwenye madini ya ujenzi, tunasema mchanga, mawe na kokoto.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana kwenye mchanga, mawe na kokoto wamejiajiri vijana wetu wa hali ya chini sana. tuwaombe sana Serikali muangalie namna ya kuwabeba wale vijana wasije tena wakafukuzwa na ma- tycoon halafu vijana wetu wakabaki tena wanahangaika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Shirika la Posta lifanyiwe rescheduling. Shirika la Posta lipambane kutokana na mazingira ya biashara yaliyopo, tuondoe urasimu. Hawawezi kupambana na Vodacom Tanzania wakati wao bado wana urasimu na mautelezi kibao, mlolongo mrefu wa maamuzi, timing inakuwa iko nyuma, wafanyakazi wanalipwa bila kuangalia marupurupu kutoka na kwenye industry. Wajitahidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TANESCO; TANESCO tunaweza tukailaumu sana lakini wafanyakazi wa TANESCO na TANESCO yenyewe siyo kwamba wanawajibika wako kutengeneza umeme kwenye nchi hii. Lazima Serikali iwawezeshe. Tuliwaambia TANESCO wasambaze umeme kwa 27,000 wakati hatujawapa hela yoyote ya kusambazia umeme huo, wakati tunajua vijijini wao wanasambaziwa kwa fedha inayokatwa kwenye mafuta kutoka kwenye REA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TANESCO walijiongeza. Inawekezana fedha za kukarabati mitambo wakatumia kupeleka umeme kwa wananchi. Sasa mitambo imeshindwa kukarabatiwa ndiyo inatokea kwamba umeme unakatika kila wakati. Serikali iliangalie hilo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuna ishu ya Kitengo kinaitwa TEITI. TEITI ni Kamati ya Usimamizi, Uhamasishaji, Uwazi na Uwajibikaji kwenye Sekta ya Madini, Mafuta na Gesi Asilia. Kazi yake kubwa ni kutuweka wazi kupitia mikataba, kuangalia mapato ya madini yanayopatikana kwenye nchi yametumikaje kwa maslahi mapana ya wananchi. Yapo maswali mengi sana kwenye jamii, kila ukitaka kuwaambia jamani tuchangie hiki wanakwambia ninyi mna madini, mna gesi, kwa nini hamuwezi kutumia hizo fedha?

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa TEITI ni kitengo ambacho kinaweza kutusaidia na kipo rasmi kwa ajili ya kazi hiyo. Lakini TEITI ina changamoto, watumishi wa TEITI wako saba wakati TEITI inakitaji kuwa na watumishi 60. Tunategemea hawa wakaangalie uwajibikaji, wakaangalie uwazi kwenye madini, wakapitie mikataba, watuelimishe wananchi mapato tuliyopata kwenye madini, kwenye mafuta, kwenye gesi asilia – watumishi saba. We are not serious. Kwa hiyo tuwasaidie TEITI ili waweze kufanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini na bajeti yao iongezwe. TEITI leo tumewatengea milioni 443, wakati hata watu wa nje wanaotusaidia, wale wahisani, wameona TEITI kazi yake ni nzuri, wamewatengea bilioni moja na milioni 725 na wameshalipa, wameshawapa nusu ya hiyo fedha. Na sisi tumewapa milioni 200.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kupunguza maswali mengine yasiyokuwa na msingi; madini mnatumiaje, mapato ya gesi yanatumikaje, mapato ya mafuta yanatumikaje. Taasisi kama hizi ambazo tumeziunda zifanye kazi. TEITI inatakiwa iwe na wajumbe nane wa kutoka kwenye Wizara wanne, lakini wanaotoka kwenye NGOs wale wanaharakati wa kupigania mapato ya wananchi wawili na wengine wanatoka kwenye makampuni hayo ya mafuta na gesi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo ni shirika la Uwazi ambalo limekubali na sisi tumeridhia kwa Sheria Na. 23 ya mwaka 2015 ambapo tumeungana na mataifa mengine yenye rasilimali hizi za madini, mafuta na gesi ili kuweka uwazi. Sasa basi tuwasaidie TEITI waweze kufanya kazi yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namalizia kwa kusema ndugu zangu, Wizara ya Miundombinu msitupe utelezi. Tunaomba lami tuwajaze madola na mayuro, Iringa tuko tayari jamani. Ahsante.