Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa nafasi ya kuchangia. Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu mwenye enzi na utukufu. Nami nitachangia kwenye Kamati hii ya Miundombinu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Rais wetu kwa kazi kubwa anayofanya kuhakikisha miradi yote aliyoikuta inakamilika. Ni juzi tu tumeshuhudia Waziri wa Fedha akiingia mkataba wa mkopo nafuu kwa ajili ya barabara za miradi inayokwenda kasi, karibia Euro milioni 178, ni mkataba ambao umeingiwa kwa ajili ya kujenga barabara zile; nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa jitihada kubwa anazofanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi naomba nichangie pia kuhusiana na bandari. Nazungumzia Bandari ya Mwambani. Kuanzia mwaka 1975 Bandari ya Mwambani Jijini Tanga ilishawekwa msingi ikitajwa kwamba ni miongoni mwa bandari zenye kina kirefu cha asili Nchini Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na eneo lenye hekta 174.2 lilishatengwa, na bilioni 2.59 zilishalipwa kwa wananchi kupisha eneo lile la ujenzi wa bandari, na tayari Mamlaka ya Bandari ilipeleka Serikalini andiko kwa ajili ya ujenzi wa Bandari ile ya Mwambani kwa ajili ya kumpata mwekezaji na kujenga under PPP (Public Private Partnership).

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ni miaka mitano sasa imepita Serikali iko kimya kuhusiana na Bandari ile ya Mwambani. Ninaiomba sasa Serikali iweke wazi mipango yake kuhusiana na Bandari ya Mwambani Jijini Tanga. Je, zile bilioni 2.59 zilizotolewa Jijini Tanga maana yake kwamba zingewekezwa sehemu nyingine Mkoani Tanga zingeweza kuleta tija vilevile.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini Serikali iko kimya mpaka sasa kuhusiana na ujenzi wa Bandari ya Mwambani? Mwekezaji kweli amekosekana kujengwa under PPP? Lakini, je, Serikali imeshatenga kiasi gani kwa upande wake wa public tujue mwekezaji ameshindikana vipi kupatikana?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaomba sana kuishauri Serikali iipe kipaumbele Bandari ya Mwambani kwa sababu tunashindana na Bandari ya Mombasa na Bandari ya Mwambani eneo lile ni potential, tangu mwaka 1975.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuchangia kuhusiana na mradi wa barabara ya mwendokasi. Tumejenga miradi ile na inakwenda vizuri, lakini mpaka sasa mfumo wake wa tiketi hauruhusu wananchi kuweza kulipa as per distance travelled. Anayetoka Kimara kwenda Kariakoo na anayetoka Kimara kwenda Ubungo wote wanalipa bei moja.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunaiomba Serikali iboreshe mfumo ule wa tiketi za kielektroniki kuweza ku- accommodate uwezo wa mwananchi kulipa as per distance travelled. Ndivyo tunavyoona kwenye nchi za wenzetu; mtu anakwenda ana-punch kila anaposhuka ili kulipa as per distance aliyotembea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na hii yote inatokana na nini; kwenye ujenzi wetu mwanzoni hatuku-accommodate dart ambazo zinaruhusu mifumo mingine ya umeme kuingia chini. Tumejenga vituo, tumejenga barabara, lakini zile conduit darts ambazo zinakubali mifumo ya umeme na fiber kuingia kwenye vituo vyetu haikuwekwa. Na ndiyo sababu baadhi ya vituo vyetu usiku vina giza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunaomba tukiwa tunaelekea kwenye phases nyingine za miradi hii, likumbukwe hili, kwamba we need to provide darts katika primary structuring za miradi ile kuhakikisha kwamba tunaweza ku- accommodate mifumo mingine kuruhusu efficiency katika mradi mzima ule.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niendelee kuchangia kuhusiana na mfumo mzima wa single window system kuziwezesha bandari zetu kuweza kufanya kazi kwa ubora zaidi. Serikali yetu naomba iharakishe kumaliza mfumo huu ambao umefika hatua za mwisho ili bandari zetu ziweze kutoa mizigo kwa haraka. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante.

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)