Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU, SERA, BUNGE NA URATIBU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa kuwa nami ni mara yangu ya kwanza kuongea kwa kuchangia katika Bunge hili kwa leo, naomba nianze kwa kumshukuru sana Rais wetu, Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, kwa imani kubwa aliyonipa mimi na Naibu Waziri Mheshimiwa Ummy Nderiananga. Tunamuahidi hatutamwangusha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi huu, kwa mara nyingine tena niendelee kumpongeza sana Spika wetu, Mheshimiwa Tulia Ackson, kwa kupita kwa kishindo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesimama kuunga mkono hoja zote mbili ambazo zimewasilishwa kutoka Kamati ya Katiba na Sheria na Kamati ya USEMI. Naunga mkono mambo yote yaliyoandikwa na yaliyochangiwa kwa mdomo. Masuala yote ni ya msingi na niwahakikishie kwamba tutayachukua na kuyafanyia kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya utangulizi wangu huu, ninaomba nizungumze point mbili kwa haraka sana. Kamati ya Katiba na Sheria imezungumzia juu ya suala zima la Sheria ya Maafa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaomba nizungumze pointi mbili kwa haraka sana, Kamati ya Katiba na Sheria imezungumzia juu ya suala zima sheria ya maafa. Tunayo sheria ya maafa sheria hii ya maafa tulikuwa nayo mwaka 1990 ilikuwa ni Sheria Na. 9 na tukafanya maboresho makubwa sana mwaka 2015 Sheria Na. 7 ya maafa na kamati imesema tuendelee kuiboresha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, Bunge lako hili la sasa session hii tutaisoma sheria hii kwa mara ya kwanza inakuja na maboresho makubwa sana sheria ya maafa. Kwa hiyo, nakubaliana kabisa na kamati juu ya maboresho katika sheria ya maafa na maboresho ambayo kamati wamesema kwanza wamesema ni muhimu kuwa na mfuko maalum wa maafa. Mfuko huu utaweka utaratibu wa namna gani ya kuchangia fedha za maafa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia Waheshimiwa Wabunge wamezungumza umuhimu wa kuwa na Waheshimiwa Wabunge ndani ya kamati za maafa. Muundo wa kamati tutakuwa na kamati za maafa ngazi ya Taifa, ngazi ya mikoa, wilaya kata hadi ngazi za vijiji kuona ni namna gani tunaratibu suala zima la maafa. Maana maafa yanatugusa sisi wenyewe ni jambo ambalo linatokea katika jamii zetu. Kwa hiyo, tutakuwa na hizi kamati, kwa hiyo Wabunge watakuwa ni sehemu ya hizi kamati za maafa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo ni muhimu sana kamati wamezungumzia kuhusu elimu juu ya maafa. Nikuhakikishie kwamba sasa hivi katika mitaala ya shule zetu za Msingi, za Sekondari wanatoa elimu juu ya maafa kuna masomo mbalimbali pale katika shule zetu ni namna gani kujilinda na maafa kwa mfano janga la njaa tunafanyaje udhibiti wa mafuriko tunafanyaje kutokata miti namna gani ya kudhibiti namna gani ya kukabiliana na suala zima la maafa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili suala la elimu ni jambo la msingi sana, hadi Vyuo Vikuu kuna taaluma za degree zinazohusiana na masuala ya maafa masuala ya disaster management, kwa hiyo, sasa hivi tumepiga hatua suala hili la maafa linapewa kipaumbele cha hali ya juu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, eneo lingine ambalo kamati pia imezungumza ni suala zima la utekelezaji wa mapendekezo ya kamati. Kamati mara nyingi inatoa maelekezo mbalimbali mapendekezo kwa hiyo, zinatoa kwa niaba ya Bunge na sasa kamati imeshauri kwamba Serikali kupitia Wizara na Taasisi zake kuendelea kupokea na kutekeleza ushauri na mapendekezo mbalimbali ya kamati.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ushauri huu upo katika ibara ya 63 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano ambayo nanukuu “kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano kwamba Bunge ndicho chombo cha kuishauri”. Sasa kwa kuwa kamati hii ya Katiba na Sheria inasimamia pia masuala ya sera, uratibu na Bunge imeshauri kwamba tuone ni namna gani mapendekezo haya yanazingatiwa. Suala hili pia ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais wetu mpendwa Mama Samia Suluhu Hassan.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kweli amekuwa akituelekeza kwamba ushauri unaotolewa na Bunge Serikali lazima tuuzingatie. Utakumbuka bajeti iliyopita kuna ushauri wa aina nyingi sana ulitolewa na Bunge na ushauri ule wote kwa kweli ulikuwa umezingatiwa na Serikali. Kwa hiyo, suala la Bunge kuishauri Serikali katika taasisi na Wizara ni jambo la kikatiba ni jambo la msingi lakini pia siyo tu kutekeleza ule ushauri, baada ya utekelezaji wa ule ushauri pia Serikali tunakuja kutoa majibu ni namna gani imetekelezwa, na ndiyo maana katika kupitisha bajeti kila tunapoenda kwenye kamati tunasema utekelezaji wa maagizo ya kamati unawekwa pale na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hili ni jukumu la kikatiba na kwa kweli tunashukuru na tunaunga mkono suala hili na ni suala ambalo lipo tumekuwa tukifanya hivyo mara kwa mara lakini kamati imefanya vizuri sana kukumbusha kwamba tunaomba tuendelee suala hili kulizingatia na kama nilivyosema kwa kweli ni maelekezo ya Rais wetu mpendwa kwamba suala hili ni lazima tupate kulizingatia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema haya maoni yote ambayo yametolewa na kamati zote mbili tunakwenda kuzingatia na vile vile tunakwenda kufanyia kazi na kama tulivyosema kwenye ibara hii ya 63 na majibu yanakwenda kuwasilishwa kwenye muhimili huu wa Bunge naomba kuunga mkono hoja nasema ahsante sana. (Makofi)