Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi hii ya kuchangia, leo nitachangia Ofisi ya Rais, Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali yote nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kusimama mahali hapa muda na wakati kama huu. Lakini pia kipekee kabisa niwapongeze Kamati hii ya Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa kwa mapendekezo yao mazuri kabisa waliyoyatoa hasa kwa asilimia 10 ya fedha zile za Serikali za Mitaa. Kiukweli kabisa ni wakati sahihi sasa kuhakikisha tunakuwa na mfumo madhubuti ambao uta-enhance transparence, ita-enhance accountability ili fedha hizi ziweze kuleta tija kwa makundi yale yaliyolengwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mujibu wa Ripoti ya Hali ya Uchumi iliyotolewa na Wizara ya Fedha ya mwaka 2020 imesema kwamba ili Taifa letu libaki katika uchumi wa kati wa chini au ili tusonge mbele kitu kimojawapo ni kuhakikisha tunatengeneza uchumi shirikishi na kuondoa umasikini, na mimi ninaamini kabisa kabisa kupitia asilimia 10 tunakwenda kufanya uchumi shirikishi na kupunguza umasikini kwa wanawake wa Taifa hili na makundi maalum. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, fedha zinazotoka kwa ajili ya asilimia 10 kwa Tanzania yetu hii ni fedha nyingi, ni fedha ambazo zinapangwa kupangiwa utaratibu mzuri na maalum ili zilete tija na athari chanya kwa makundi yaliyolengwa. Ukiangalia takwimu mwaka 2019/2020 Serikali yetu imekusanya zaidi ya shilingi bilioni 717, inamaana asilimia 10 ni bilioni 71 point, lakini mwaka 2021 Serikali yetu imekusanya kwa Tanzania nzima shilingi bilioni 757, asilimia 10 ni zaidi shilingi bilioni 76; lakini mwaka 2021/2022 Serikali yetu imepanga kukusanya shilingi bilioni 863 inamaana asilimia 10 ni itakuwa shilingi bilioni 86 za Kitanzania, ni fedha nyingi sana ambazo ni lazima tutengeneze utaratibu mzuri kuhakikisha unaleta tija kwa makundi yaliyopagwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiangalia kanuni zetu ambazo zimetolewa kwa ajili ya asilimia 10 zina madhaifu, pamoja na mwongozo ambao ulitolewa Machi, 2020 nao unahitaji maboresho. Kwa mfano katika mwongozo pamoja na kanuni kifungu cha 21(d), imeitaka TAMISEMI iwaelekeze Wakurugenzi wa Halmashauri kufungua akaunti moja tu ya kuhifadhi zile fedha pamoja na marejesho. Sasa fedha za marejesho zile ni fedha nyingi tukichanganya kwenye akaunti moja maana yake tunakwenda kupunguza uwajibikaji na accountability. Nashauri kanuni ielekeze kuwepo na akaunti ya marejesho pamoja na akaunti ya mikopo ile ya makusanyo ili ya asilimia 10. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, vile vile ukiangalia kanuni ya 21 kifungu cha 37(a), kinasema kwamba Halmashauri zote zitoe mafunzo kwa wale wanaopata mikopo. Lakini mafunzo yake yanalenga ujasiriamali, yanalenga uongozi, hayazungumzi namna ambavyo wapewa mikopo watazijua hizi kanuni na taratibu ambazo zimewekwa. Kwa maafisa maendeleo ya jamii wengi na maafisa ustawi wa jamii wengi wana take advantage kwa sababu hawaelekezwi yale makundi maalum namna ambavyo kanuni hizi zinaelekeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano kumekuwa na malalamiko mengi, wanawake wanasema tunaomba mikopo kila mara lakini hatujulishwi kwamba nimepata au nimekosa ninaahangaika nakwenda na kurudi kila mara. Lakini kanuni inaelekeza ndani ya siku saba mpe taarifa mwanamke yule kwamba umepata mkopo au hujapata, inamaana siku saba zikipita mwanamke yule ata assume amepata mkopo. Kwa hiyo, tunaomba sana kanuni hizi zielekezwe kwa akinamama na makundi yaliyolengwa, ili waweze kutumia fursa hii ipasavyo.

MWENYEKITI: Ahsante Mheshimiwa Engineer Mwanaisha.

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, oooh! Kumbe muda umeisha nakushukuru sana ahsante. (Makofi)