Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

Hon. Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi, namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunijaalia uzima leo nikaweza kusiamama mbele ya Bunge hili tukufu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naanza kwa kumpongeza sana Jemedari wetu Mama Samia Suluhu kwa jinsi anavyochapa kazi na kutuongoza vizuri na mambo yetu yanaenda vizuri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo nawapongeza Mawaziri ambao wanatuongoza kwenye Wizara zetu hasa hii yetu ambayo tunashughulika nayo moja kwa moja kuanzia kwa Waziri Mkuu na Waziri wa Katiba na Sheria. Kwa kweli tumekuwa tunafanya kazi kwa mashirikiano na masikilizano makubwa, naweza kusema ni Kamati ambayo tunajiona kama tunafanya kazi heaven on earth, tunafanya kazi peponi katika dunia jinsi tunavyoweza kufanya kazi na ku-deliver.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nianze kwa kupongeza sana Wakala wa Usalama na Afya Sehemu za Kazi. Kwa kweli wakala huu umeweza kufanya kazi vizuri sana kwa mujibu wa sheria iliyoianzishwa ya mwaka 2003; kwanza jambo la muhimu sana lile la kupunguza tozo na kuwaondolea wadau kero, halafu urasimu wa kupata huduma kwa kutumia nyenzo hizi za kisasa kwa matumizi ya TEHAMA.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine waliloweza kufanya watu hawa ambalo ni la heshima sana ni lile la kusimamia kumaliza jengo la Wakala na Usalama Sehemu za kazi hapa Dodoma. Jengo la uhakika lenye viwango lenye kutimiza masharti yote, lenye kurahisisha watu wa aina yoyote kuweza kutumia, kwa hivyo wale wote walioweza kusimamia katika kazi nzuri hii nawapa kongole zao.

Mheshimiwa Mwneyekiti, ziko changamoto katika OSHA nayo ni uhaba wa watumishi, sijui kwa nini; kwa sababu tunaona huko nje tunaona wamezagaa ma-graduate, mechanical engineering, ma-electrical engineering, watu wa afya na nini, sielewi inakuaje mpaka watumishi ikawa tabu kuchukuliwa kwenye Wizara hiyo kwenda kufanya hiyo kazi. Kwa upande wa OSHA nawapongeza sana na waendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sehemu yangu ya pili ninayotaka kuzungumzia ni hii ya Wakala wa Usajili wa Vizazi na Vifo; hii nayo imepiga hatua kweli kweli kwa sababu zamani ilikuwa shida kidogo, lakini wameweza kuongeza vituo kutoka 139 ambayo ilikuwa kwa kupitia kwa Mkuu wa Wilaya hadi vituo 8,817 katika vituo vya tiba, huko kote watoto wanaandikishwa. Kwa hiyo hii imewapunguzia wananchi usumbufu na vilevile Watoto wanaweza walokuwa chini ya miaka mitano wanaandikishwa bila ya kutoa ada yoyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia zipo changamoto ambazo RITA imewakabili ni zile za kushindwa kuandikisha watoto wanaozaliwa nje ya nchi, kwa sababu bado sheria haijatoa mamlaka kwa RITA kutekeleza hiyo. Sasa ninaushauri na ushauri wangu kwa Wizara ya Katiba na Sheria kwa kushirikiana na Wizara ya Mambo Nchi za Nje, waje na mpango mkakati wa kutatua changamoto hii haraka iwezekanavyo ili hili jambo liweze kufanyaika na watu wapate vyeti vyao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na vilevile liko jambo moja ambao linawasonenesha sana, ni hili watendaji wa RITA kuwa wanakaimu miaka kadhaa, yuko mwanadada pale tangu tumeingia sisi Bungeni hapa yeye anakaimu, kaimu, kaimu, sasa kama hafanyi kazi vizuri huyu kwa nini mnamuacha na sisi tunaamini anafanya kazi vizuri kwa sababu ripoti zinapokuja kwenye Kamati yetu tunaona anafanya kazi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niiombe mamlaka husika dada huyu apewe nafasi yake kwa sababu anaweza kufanya kazi vizuri. mwisho utamkuta anastaafu yupo pale pale, sasa hivyo ndio nini mnafanya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo langu lingine ninachotaka kuzungumzia sasa hivi ni kuhusu dawati la kuwasaidia kwenye sheria. Kuna watu wanapata taabu sana, sasa imetolewa huduma na Wizara hii ya kuwapa watu training wakawasaidie watu kuanzia Mahakama ya Mwanzo mpaka Mahakama ya mwisho. Wasiwasi wangu kama hawa watu waangaliwe vizuri isijekuwa tunatengeneza vishoka vyengine kwenye Mahakama. Wapate training nzuri ili waondolewe, kwa sababu wananchi wengi wa Tanzania hawana uwelewa mzuri wa mambo ya kisheria, kwa hivyo nifurahie kwa hili na ninaunga mkono na ninaomba Serikali izidishe iwaondolee wananchi shida zao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hayo ninaunga mkono hoja hii, ahsanteni. (Makofi)