Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

Hon. Edward Olelekaita Kisau

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala na Serikali za Mitaa kuhusu Shughuli zake kwa Mwaka 2021

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa nafasi, na nimpongeze Mwenyekiti wa Kamati ya Katiba na Sheria na Wajumbe wote wa Kamati kwa kazi kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na kwa sababu ya muda, niwapongeze Mawaziri wote ambao wanakuja kwenye Kamati yetu, wote, kuanzia Ofisi ya Waziri Mkuu, Chief Whip, Attorney General, Waziri wa Sheria, Ofisi ya Waziri Mkuu mambo ya Ajira, Muungano – wote kwa ujumla wenu, kwa kazi kubwa ambazo kwa kweli mmefanya kwa utekelezaji wa kazi katika Wizara zenu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kamati ya Katiba na Sheria kwa muda wa mwaka mmoja imeweza kufanikiwa kurekebisha sheria karibu 58, siyo kazi ndogo sana; utungwaji wa sheria siyo kazi ndogo sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwenye sheria hizo, kati ya sheria maarufu sana ambazo tumebadilisha ni kuruhusu Kiswahili kitumike kwenye mahakama zetu na kutafsiri sheria zetu ziende kwa Kiswahili. Kwa kweli kati ya sheria ambazo nazikumbuka na mabadiliko mazuri sana kwa Watanzania ni kuruhusu Kiswahili kianze kutumika ili watu waanze kufuatilia mashtaka kwenye kesi za mahakama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kinachonifurahisha zaidi ni kwamba Ilani ya Chama Cha Mapinduzi baada ya sisi kusema kwamba tubadilishe sasa sheria ziende kwa Kiswahili, Wizara ya Katiba na Sheria walitakiwa kwa mujibu wa ilani yetu wawe wametafsiri sheria 157. Lakini kwa kasi yao wamerekebisha na kutafsiri sheria 208; hongereni sana. kasi hii ikiendelea mtakipa Chama Cha Mapinduzi heshima kubwa sana kule. Kama ilivyo kwenye ilani, ukurasa wa 167. Na ninaomba ninukuu: -

“Kuongeza uelewa wa wananchi kuhusu sheria mbalimbali kwa kutafsiri sheria 157 kutoka Lugha ya Kiingereza kwenda Kiswahili”

Mheshimiwa Mwenyekiti, big up. Ninyi mmevuka lengo. Najua mna kazi kubwa sana, kwa sababu hata mnatakiwa kutafsiri subsidiary legislation na zile nyingine karibu 39,000; mtakuwa na kazi kubwa sana. kwa hiyo, naamini Wabunge watawaelewa wakati wa bajeti, mkileta bajeti hapa mpewe pesa nyingi muendelee kuchapa kazi kubwa zaidi. Kwa hiyo kwa miaka mitano ninyi mmeshaturahisishia kazi. Sheria zile principal zipo karibu 449, ninyi meshavuka kabisa; hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini Wizara ya Katiba na Sheria ilitakiwa, kwa mujibu wa Ilani yetu, kuboresha majengo ya mahakama. Wajumbe wa Kamati ya Katiba na Sheria tulipata nafasi ya kutembelea mikoa mbalimbali kuona miradi ya mahakama; tumeanzia Kongwa, tumekwenda Morogoro, tumekwenda Njombe, tumekwenda Dar es Salaam, tumekwenda Arusha na leo tumekwenda Dodoma kuona jengo kubwa la mahakama, Judiciary Square ambayo inasadikiwa litakuwa jengo bora kuliko Central and Southern Africa, na Waheshimiwa Wabunge tunawakaribisha. Wizara ya Sheria wanatuambia mwaka huu Desemba, watafungua hili jengo. Jengo zuri halijawahi kutokea; hongereni sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mabadiliko mengine ambayo ni muhimu sana ni mabadiliko ya kuwaruhusu mawakili kwenda kwenda kwenye mahakama za mwanzo. Hii siyo tu inafungua fursa ya ajira lakini inawafanya wananchi wapate huduma za uwakilishi kwenye vijiji vyao; excellent.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kati ya sheria zilizobadilika ni kuweka break ile nolle prosequi na amicus curiae kwenye mambo ya sheria, itaongeza, na itapunguza mashtaka yale ambayo yanawasumbua wananchi sana. na vilevile kusema upelelezi ukamilike ndiyo tuendelee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimalizie kwa kusema hivi…

MWENYEKITI: Malizia sentensi ya mwisho Mheshimiwa Olekaita.

MHE. EDWARD O. KISAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, sentensi moja. Na kwa kuwa Wizara ya Katiba na Sheria mna kazi maalum ya kufanya, naomba niseme Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, tarehe 29, alipokuwa akihutubia UN, na mimi nasema he for she; alisema yafuatayo: -

“Aware that being passionate about gender equality is not sufficient, my government is reviewing policy, legal framework in order to come up with actionable, measurable plans to ensure economic empowerment for women but also aspects pertaining to gender equality and gender parity.”

Mheshimiwa Mwenyekiti, mlete sheria hizi tuzibadilishe. Nakushukuru sana, naunga mkono hoja asilimia 100; ahsante sana. (Makofi)