Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Mrisho Mashaka Gambo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arusha Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, nami niungane na wenzangu kwanza kabisa kukupongeza kwa kuchaguliwa kuwa Naibu Spika, na ninakutakia kila la kheri kwenye kazi zako.

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi nitaongeleza jambo moja tu kwa sababu ya changamoto ya muda.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunafahamu kwamba malengo makubwa tuliyo nayo ni kuhakikisha kwamba tunaongeza ajira kutokana na Ilani yetu ya Uchguzi ya CCM; tuliahidi ajira milioni nane mpaka mwaka 2025, lakini pia kuongeza na mapato. Na kwa kupitia Sekta ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi ndiko kwenye uwezekano mkubwa wa kutoa ajira nyingi zaidi.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini pia ukiangalia, taarifa yam waka 2019 inaonesha kwamba sekta ya horticulture imeweza kuchangia asilimia 38 ya fedha zote za kigeni ambazo zinatokana na mapato ya kilimo. Ukiangalia kwa mujibu wa data zilizopo pia kwa nchi za Tanzania, Kenya na Ethiopia tunaona kwamba Tanzania tunatumia eka zisizozidi 120 kwa ajili ya horticulture, wenzetu wa Ethiopia eka 1,450 na Kenya 2,800; na ukizingatia kwamba sisi kule Arusha tuna mashamba 11 ambayo yamefungiwa, hayafanyi tena shuhguli zile ambazo zilikuwa zimeusudiwa. Mashamba hayo ni kama vile Kiliflora, Meru Flowers na mashamba mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na kufungiwa kwa mashamba haya tumepata changamoto nyingi sana. Changamoto ya kwanza tumepoteza fedha za kigeni kiasi cha dola za Kimarekani 42,450,000, tumepoteza pia ajira kama 4,010, na hizi ni ajira za moja kwa moja, ukiacha nyingine ambazo zinatokana na sekta yenyewe. Tumepoteza pia fursa kutokana na mnyororo wa thamani, kwa sababu kutokana na kilimo kile kuna ambao walikuwa wanauza pembejeo, kuna ambao walikuwa wanafanya biashara za usafiri pamoja na shughuli nyingine. Lakini pia tumeondoa imani kwa wawekezaji, kwa sababu mashamba yale 11 yalikuwa chini ya wawekezaji, kitendo cha kuchukuliwa na Serikali imetoa hofu kwa wawekezaji wengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na changamoto hizo mimi nilikuwa na mapendekezo yafuatayo.

Kwanza, nilikuwa nashauri kwamba kama wawekezaji waliokuwepo wameshindwa kuwekeza na ushahidi upo kwa sababu alikuwa anadaiwa na Serikali kupitia benki yatu ya TIB, lakini bado dhana na tija ya uwekezaji wa sekta ya bustani (horticulture) kwenye yale maeneo bado iko pale pale. Kwa hiyo tunashauri kwamba Serikali baada ya kuchukua mashamba yale sasa watafutwe wawekezaji wengine wakafanye uwekezaji ili tuweze kupata zile fursa ambazo tunazikosa, kama vile ajira pamoja na fursa ya mapato.

Lakini pia tulikuwa tunashauri kuwa…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. MRISHO M. GAMBO: Mheshimiwa Naibu Spika, ninakushukuru sana.