Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Humphrey Herson Polepole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. HUMPHREY H. POLEPOLE: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nikupongeze sana kwa kuchaguliwa kwa kishindo na ahsante sana kwa nafasi ya kuchangia. Nipongeze sana Wenyeviti wa Kamati wamesema mambo makubwa sana yaliyonipelekea kubadilisha kidogo mtiririko wa namna ambavyo ningependa kuchangia na ningependa kwanza kusema kama ifuatavyo: -

Kwa maana njema kabisa kama Serikali isiposikiliza mapendekezo ya Kamati hizi mbili kwa umakini, tutaelekea kubaya na mimi ningesema jambo moja ambalo labda linaweza likaonekana lisieleweke, lakini kama tusipoweka dhamira ya dhati kwenye mradi mmojawapo tu wa chuma tunatumia pesa nyingi kuleta chuma hapa na inaathiri kitu kimoja kwenye uchumi kinaitwa balance of payment yaanitunatumia pesa nyingi sana kuagiza bidhaa kutoka nje kuja ndani kuliko ambavyo tunauza bidhaa za ndani kwenda nje, kiuchumi unapokuwa na nakisi kwenye balance of payment si afya kwenye uchumi na ni kitu ambacho kinaweza kikatufikisha siku moja tukashindwa kuwa na fedha ya nje ya kutosha kuweza kufanya majukumu yetu mengine ikiwemo kulipa madeni. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi ningependa niseme katika hili la kuweka nidhamu ya namna ambavyo tunazalisha ndani, ifike pahala tukubaliane kama Taifa yako mambo tuweke sera za ulinzi (protection policies) katika nchi yetu kwamba bidhaa hii na hii hatuta agiza kutoka nje tutaizalisha kutoka ndani.

Mheshimiwa Naibu Spika, nitakupa mfano mafuta ya kula yanatuongezea nakisi kwenye balance of payment, mbolea inatuongezea nakisi kwenye balance of payment, hiyo chuma nimeisema, sukari inatuongezea nakisi kwenye balance of payment, mchele unalimwa hapa Tanzania lakini bado tunaagiza inatuongezea nakisi kwenye balance of payment, ngano/shairi ambayo inaweza kulimwa hapa Tanzania inatuongezea nakisi kwenye balance of payment.

Mheshimiwa Naibu Spika, hii nakisi kubwa nikipitia pitia nyaraka hapa za Wanakamati na nini inaonekana bado ni tatizo baadhi yenu mtafahamu ya kwamba dhamira nzuri ya Mheshimiwa Rais kwenda kukopa kule IMF pamoja na mambo mengine ilikuwa ni kuweza kushughulika na nakisi kubwa inayoongezeka kwenye balance of payment. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, rai yangu kwa Serikali ziko bidhaa ambazo tukiwekeza vya kutosha hapa hapa nyumbani tutajitosheleza na tukijitosheleza fedha nyingi itabaki hapa hapa nyumbani na hapo ndiyo inapokuja kwenye Wizara ya Viwanda na Biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, duniani kote wale wanaitwa micro small and medium enterprises ndiyo wanashika zaidi ya asilimia 90 ya chumi zote. Hapa Tanzania hawa micro small and medium enterprises ndiyo ambao wanashikilia viwanda vingi vidogo na vya kati ambavyo vina jukumu la kuchakata mazao mbalimbali na huduma na bidhaa ambazo zinahitajika hapa nyumbani. Ifike pahala hawa micro small and medium enterprises yaani biashara ndogo sana, ndogo na za kati ziwezeshwe kwa makusudi na Serikali yenyewe, mabenki hayawezi kuweka pesa kule kwa sababu watasema hakuna usalama. Lakini Serikali ndiyo baba yao, ndiyo mama yao na hapa katika Wizara ya Fedha na Mfuko ule wa Uwezeshaji iko mifuko zaidi ya 50 ya kuwezesha wananchi kiuchumi haisomani, haijuani, malengo yake hayashabihiani, sasa unapokuwa una mifuko zaidi ya 50 yenye fedha za mamia ya mabilioni ambayo haisomani nafahamu yaliwahi kutoka maelekezo hapa kwamba mifuko hii ihuishwe, lipatikane fuko moja kubwa la kwetu la ndani ambalo tutalitumia kuwawezesha wajasiriamali wadogo ambao hawa kimsingi ndiyo engine ya uchumi wetu. Tukifanya hivyo hata wigo wetu wa kodi na mapato utaongezeka. Nakushukuru sana. (Makofi)