Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. CHARLES J. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nikushukuru kwa kunipatia fursa ya kuchangia taarifa za Kamati hizi mbili kwa sababu ya muda nitachangia taarifa ya Kamati inayoshughulika na sekta ya kiuzalishaji ya kilimo, mifugo na uvuvi.

Mheshimiwa Naibu Spika, hizi ndiyo sekta za kiuzalishaji na kwa mtazamo wangu mimi ni kwamba naangalia ustawi wa ndani ya nchi, uzalishaji wa chakula na naangalia uwezo wa sekta hizi kuuza nje. Tunapata chakula Tanzania, hatujapata njaa kwa miaka sita au saba na watu wanafurahi, lakini nataka niwaambie Watanzania tunakula chakula cha bei ghali, tunazalisha bila tija, tungetegemea watu wale nyama kwa shilingi 5,000 kwa kilo, wale samaki kwa shilingi 3,000.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini nchi yetu ina export thamani ya dola bilioni sita lakini bahati mbaya 2/3 inatokana na madini na zaidi dhahabu, tunapaswa tu export tukitegemea hizi sekta za kiuzalishaji kwa sababu zina nguvu ya kujumuisha, zinashirikisha watu walio wengi. Lakini ukisikiliza wataalamu ikiwepo Wizara husika hizi, hawa watu wakiwezeshwa Serikali ikiwekeza katika sekta hizi tutaweza ku-export zaidi ya bilioni 10 kutoka kwenye sekta hizi, lakini madhara yake ni kwamba wananchi walio wengi watakuwepo wataachana na hizi tabia za kushukuru vitu vidogo vidogo.

Mheshimiwa Naibu Spika, nataka nizungumze kitu kimoja na nimshauri Mheshimiwa Spika aiambie Serikali iletwe semina na Wabunge tukae kama Kamati tujadili hizi sekta mbili kwa kifupi bila kutafuta maneno mimi sijadili pesa walizopewa, hizi sekta hazijapewa pesa yaani Serikali haijawekeza kwenye sekta hizi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, niwape jambo moja la kuangalia, fursa ya samaki wa kufuga world potential ni bilioni 284; hakuna zao tunalima Tanzania kwenye soko la dunia lina kiasi hicho. Lakini ngoja niwaeleze Tanzania sisi tunasifika kwa kuwa na maji mengi, sasa niwaambie aibu, uwekezaji wa Serikali ya Uganda samaki wa kufuga wanauza tani 118,000; sisi tunauza samaki tani 12,000 nasema tani 12,000 lakini nini wenzetu hawa wamewekeza sitaki kuwaletea historia za mzee wangu za Brazil nawaeleza Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, Egypt wana samaki tani milioni 1.4; kwa hiyo ujanja ni kwamba kwa sababu tuna water bodies nyingi Tanzania Serikali muwekeze kule na uzuri wa sekta hizi tatu nilizozungumza ukiweka pesa leo, kama alivyosema Mwenyekiti wa Kamati inalipa na tusitegemee benki zetu za commercial mambo ya CRDB na asilimia tisa au TBBA hakuna, twende tukakope kwenye benki za kimataifa, zinazotoza riba ndogo, tuweke mamlaka za Serikali tuwape Watanzania. Sekta binafsi mnayoisema siwezi kukubali sekta binafsi ya kutoka nje hayo ni ya kumlisha mtoto wa kwale wakati watoto wa kuku wanakufa, tuchukue pesa tuwape watoto wetu Watanzania, tuwasimamie waingie kwenye uchumi. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, mimi kwetu watu wanasema ziwa liliuzwa kwa sababu hawawezi kuvua kama watu wanaokuja na ….technology, sasa watu wangu mimi lazima tuwatengenezee vizimba, tuwatengenezee miundombinu waweze kushiriki.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho nisaidie nizungumze hoja ya Tume ya Mipango; kuna kitendawili kimoja, kuna Wizara ina shughulikia maji ya binadamu, nyingine maji ya kilimo, nyingine maji ya mifugo, nyingine inazuia mafuriko ya miundombinu tungekuwa na Tume ya Mipango hili suala lingeratibiwa kwa pamoja. Lakini unakuta sasa kuna Wizara sita zinashughulika na kitu kile kile halafu mtu anakwambia eti uchimbe kisima unyweshe ng’ombe huo umeme utautumia kutoka wapi? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo tungekuwa tumeratibiwa pamoja tungetengeneza kitu kinaitwa mini leg hawa wa ndugu zangu wa Kaskazini wasingekuwa wanalia, wangekuwa majosho yao.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja. (Makofi)