Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

Hon. Kunti Yusuph Majala

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Viwanda, Biashara na Mazingira Kuanzia Januari, 2021 hadi Februari, 2022 pamoja na Taarifa ya Shughuli za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji kwa Kipindi cha Januari 2021 hadi Januari 2022

MHE. KUNTI Y. MAJALA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipatia nafasi na mimi niweze kutoa mchango wangu kwenye hizi Kamati zetu mbili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sote tunakubaliana kwamba bila kilimo sisi sote humu tusingekuwepo ndani, kwa sababu tunakula chakula ili tuweze kupata afya bora na akili timamu kwa ajili ya kutekeleza majukumu yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, samahani, kumbe cheo kimebadilika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia kwenye mtiririko wa utoaji fedha kwa Wizara ya Kilimo, Wizara ya Kilimo bado iko chini, Wizara ya Kilimo bado inaendelea kusahaulika, Wizara ya Kilimo bado imetupwa kabisa huko mafichoni ilhali hii Wizara hii ndio tunayoitegemea Watanzania wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, Watanzania zaidi ya 65% ndio wanapata ajira kupitia Wizara hii. Inatulisha na inatoa ajira, lakini Wizara hii ndiyo inayohangaika wakulima wake ambao ni zaidi ya 80% huko vijijini watafute mbegu wenyewe, watafute pembejeo za kilimo wenyewe, mvua wanategemea ya Mwenyezi Mungu, kilimo cha kudra ya Mwenyezi Mungu, lakini Wizara hii Serikali haijawahi kuonesha nia na dhamira ya dhati ya kuisaidia ili tuweze kuliokoa Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tuna Mfuko wa Pembejeo wa Taifa; Mfuko huu pamoja na Benki ya Kilimo, nianze na Mfuko wa Pembejeo wa Taifa; mfuko huu wa pembejeo wa Taifa tulitegemea Serikali itoe feddha za maendeleo kwenye Wizara ili huu Mfuko wa Pembejeo wa Taifa waweze kupatiwa fedha ili wakulima wetu wadogo wadogo kule chini waweze kupata zana za kilimo na waweze kulima kilimo chenye tija.

Mheshimiwa Naibu Spika, lakini Wizara imekuwa ikinyimwa fedha na mfuko huu umeendelea kukosa fedha, matokeo yake mfuko uko pale, watumishi wako pale, hakuna kazi yoyote wanayoifanya; wanaamka asubuhi wanakuja wanasaini, wanapumzika wanasubiri muda ufike warudi majumbani kwao.

Mheshimiwa Naibu Spika, kama Serikali inaona kilimo hakina tija kwenye Taifa hili niombe tuifute hii Wizara ili wakulima wa nchi hii tuendelee kulima kwa namna tunavyoweza kuliko kuwa na Wizara ambayo haina msaada kwa Watanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, Benki ya Kilimo; benki hii tumeendelea kuipigia kelele humu ndani, kila siku story ni zile zile, maneno ni yale yale na imebadilika sasa mmebakisha kufukuza kila siku mnatubadilishia Wakurugenzi; sasa huyu Mkurugenzi haujampatia fedha, unamfukuza, ulitaka afanye nini? Si amekaa tu, fedha hakuna, atamkopesha nini huyo mkulima? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, mimi niiombe sana Serikali; kama kweli tuna nia na dhamira ya dhati ya kuinua kilimo cha Taifa hili na kujenga uchumi wa nchi hii, twendeni tukaongeze fedha kwenye Wizara ya Kilimo ili tuweze kuleta tija katika Taifa letu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Wizara ya Maji; Wizara ya Maji angalau safari hii imepata mkongojo imesogea, lakini changamoto kubwa iliyoko Wizara ya Maji ni miradi mikubwa ya kimkakati.

Mheshimiwa Naibu Spika, tangu nikiwa nje huko sijaingia kwenye jengo hili kulikuwa na mradi unaitwa Mradi wa Bwawa la Kidunda, una zaidi ya miaka 20 leo Bwawa la Kidunda halijakamilika. Sasa sijui shida ni nini kwa Serikali kwenda kutekeleza miradi hii mikubwa ambayo ina tija kubwa kwa Taifa letu? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa natamani sana, tunaitaka Serikali na tumeendelea kuwashauri Wizara pamoja na Serikali, kwa maana ya Wizara ya Fedha, watusaidie hii mikataba wanayoingia na wafadhili kama wanaona haiwezekani hao wafadhili waliokuja wawaondoe watafute wafadhili wengine ili miradi iweze kutekelezeka. Napata hofu sana, Mkoa wa Dodoma leo tuna Mradi wa Farkwa, sasa hivi una zaidi ya miaka sita tunakwenda was aba, tumelipa fidia, lakini suala ni lini tunaanza ujenzi wa Bwawa la Farkwa? Story, kwa hiyo, tukakwenda humu ndani, watakuja, watakuja, watakuja; bado hatujakamilisha mazungumzo, bado watu sijui wanafanya nini? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, maneno yamekuwa ni mengi kuliko utekelezaji na uchukuaji wa maamuzi. Serikali tunaiomba iwe inafanya haraka kwenye suala zima la uchukuaji wa maamuzi ili kupunguza muda wa kuendelea kupoteza mud ana kutokutekeleza miradi hii kwa wakati. Nakushukuru, ahsante. (Makofi)