Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

Hon. Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Hotuba ya Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania wakati wa Kufungua Bunge la Kumi na Moja

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, wale watu ambao walikuwa hawalipi kodi, lakini Mheshimiwa Rais wetu amethubutu kufanya kazi hiyo na matokeo yameonekana na kodi sasa zimeonekana mpaka hatimaye sasa watoto wetu wameweza kwenda kusoma bure
kwa sababu ya mambo mazuri ambayo Rais wetu alituahidi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, hapa ni kazi, mimi nitaendelea. Kuna kazi ambayo tunatakiwa tuifanye na Serikali inatakiwa iangalie kwa makini kuhusu Halmashauri zetu upande wa Wakurugenzi pamoja na Watendaji. Kuna sehemu nyingine watendaji
wanakaimu na kama Mkurugenzi mara nyingi anakaimu siyo Mkurugenzi kamili inakuwa kazi kufanya kazi ya maendeleo katika maeneo husika. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, unakuta sehemu nyingi kuna miradi mbalimbali ambayo Serikali iliainisha ili iweze kufanyika. Katika maeneo mengi miradi hiyo haikuweza kukamilika kutokana na utendaji. Ukienda pale anasema mimi Kaimu, Mkurugenzi kasafiri siwezi kufanya
jambo lolote. Hilo limekwamisha sana miradi yetu tuliyokuwa nayo.
Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kazi inaendelea, kuna Wakurugenzi wengi wamesimamishwa kutokana na majipu, lakini bado kuna maeneo mengi ambayo uaminifu ni mdogo. Naomba kazi hiyo iendelee, tuweze kusafisha ili fedha za maendeleo tukipanga bajeti
ziweze kufikia malengo yale tunayoyatarajia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende upande wa wakulima na wafugaji. Kifike kipindi sasa Serikali, iainishe maeneo ya wakulima na wahainishe maeneo ya wafugaji.
Limekuwa tatizo kubwa sana kiasi ambacho sasa hivi kuna vitu ambavyo vinaashiria siyo vizuri, wanapigana, wanauana na sisi nchi yetu ni nchi ya amani na utulivu. Naomba Serikali yetu ijipange vizuri kwa ajili ya eneo hilo.
Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru sana Waziri wa Ardhi, ametuandikia barua Wabunge wengi tuainishe migogoro ya ardhi. Naomba nikupongeze sana Waziri wa Ardhi kwa kuliona hilo, tuweze kukusaidia na tuainishe maeneo yote yenye migogoro.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakwenda kwenye reli, watu wengi wamezungumza kuhusu masuala ya reli. Kwangu Mpanda ni kitu muhimu sana kutokana na na hali halisi ya sasa hivi barabara zote hazifai, wananchi wa Mpanda wako hewani, mambo yao hayaendi vizuri.
Namwomba Mheshimiwa Waziri reli hii ya Mpanda hata kesho treni ianze kwenda kwa sababu wananchi wa Mpanda wanapata shida, taabu kwa ajili ya mahitaji yao binafsi. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja kwenye masuala ya uchumi, uchumi hauwezi kukua bila miundombinu. Maeneo ya Tabora, Kigoma, Mpanda ni maeneo ambayo yana uchumi mkubwa, wanalima sana, wana mazao mengi, ambayo yanatakiwa yatoke kwa ajili ya
Watanzania wote, lakini kutokana na miundombinu mibaya, barabara hazifai. Mtu anatoka Tabora kwenda Mpanda anatumia siku tatu, analala njiani, kusema kweli tunasikitika sisi Wabunge tunaotoka maeneo hayo kuwa tumesahaulika muda mrefu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naiomba Serikali, mtuangalie kwa jicho la huruma wale wananchi ni Watanzania kama Watanzania wengine, wanahitaji mahitaji muhimu. Shughuli zao za kilimo, basi waweze kutoa mazao yao ili waweze kupata mahitaji yao binafsi.
Mheshimiwa Naibu Spika, nakuja upande wa polisi, nawapongeza sana polisi wetu, wamefanya kazi nzuri, lakini kuna maeneo mengi nyeti hakuna vituo vya polisi, wananchi usalama wao unakuwa mdogo, maeneo mengi utakuta wana mazao mengi, lakini usalama
wao haupo kutokana na kukosekana kwa kituo cha polisi katika maeneo hayo. Tunaomba Serikali ijipange basi kupeleka vituo vya polisi katika maeneo hayo ili wananchi waweze kupata usalama wao.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niende kwenye mapato tena. Zamani kulikuwa kuna Shirika lilikuwa linaitwa NASACO, Shirika la NASACO lilikuwa linakusanya mapato bandarini, ile mizigo yote inayotoka kwenye meli, lile shirika sasa hivi halipo. Sasa naomba kama kuna
uwezekano Serikalini, lile lilikuwa linasaidia sana mapato yalikuwa hayawezi kupotea ndani ya bandari zetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba basi Serikali ijipangwe vizuri, kuona ni jinsi gani ya kuweza kupitisha makontena ndani ya bandari zetu, maana kuna maeneo mengine hakuna usalama mzuri, watu wanaingiza mizigo bila kulipa ushuru.
Mheshimiwa Naibu Spika, tumeshuhudia Tanga, bandari bubu nyingi, lakini na Mpanda, Kalema kuna bandari, mpaka leo hatuwezi kujua hatima yake itaisha vipi. Kuna sehemu nyingi muhimu, nyeti ambazo zinaweza kuliletea Taifa hili mapato, lakini tumeliacha wazi. Tunaomba
basi na sisi bandari ile ya Kalema ifanyiwe kazi, ina miaka sijui sita sasa hivi, majengo yalianza, Mkandarasi sijui ka-disappear wapi hatufahamu. Tunaomba basi ili uchumi uweze kukua, bandari, reli na barabara ziweze kutengenezwa vizuri kwa kiwango cha lami. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hivi Serikali ijipange, mnapoteza hela nyingi…
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa muda wako umekwisha, tafadhali naomba ukae
MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)