Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Philipo Augustino Mulugo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia wasaa nami niweze kuchambua hoja, lakini mimi nijikite kwenye mambo makubwa mawili hasa sekta ya elimu, nami ni mdau wa elimu hapa nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Wabunge mnisikilize. Lipo jambo linaendelea kwenye mashule yetu nchi nzima ambalo jipya mno halijawahi kutokea toka tumepata uhuru. Jambo hilo linaitwa utekelezaji wa Kalenda mpya katika mtaala uliopo hapa nchini. Jambo hilo limetolewa mwezi wa Kwanza na Ofisi ya TAMISEMI, kitu ambacho hakijawahi kutokea TAMISEMI akatoa miongozi ya implementation za curriculum. Anayetakiwa kutoa masuala yote ya kitaaluma nchini ni Mtaaluma Mkuu kwa suala la elimu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kisheria, Mtaaluma Mkuu Tanzania hii ni mmoja tu na yuko Wizara ya Elimu. Sasa TAMISEMI leo wamevaa utaaluma wa kutoa maagizo kwenye shule zetu zote, tena wanaingilia mpaka kwenye shule za private. Jambo hili ni gumu na limeshindwa kutekelezeka.

Mheshimiwa Mwenyekiti, TAMISEMI wametoa mwongozo, ninao hapa nitakuletea kwa sababu upo kwenye simu, lakini kesho naweza nikauchapa vizuri nikakuletea. Nchi nzima, mashule yote binafsi na mashule ya TAMISEMI wameagizwa wafuate Kalenda ya Utekelezaji iliyotolewa na maafisa wa secondary ya primary pale TAMISEMI kwamba kuanzia mwaka huu shule zote nchini zifuate kalenda hiyo kwa vipindi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama shule hii haina somo la mwalimu wa physics, basi wanaachwa wanakwenda kwenye somo lingine, ndiyo wanakuwa hawawezi kutekeleza ile kalenda. Shule ambayo imeshapata mwalimu wa physics na wanafundishwa, basi wasiende mbele mpaka wasubiriane kwa huyu mwalimu ambaye hakuwepo. Sijawahi kuona jambo kama hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hali imeharibika mashuleni. Ukiwauliza wanasema maagizo yametoka juu. Yametoka juu kwa nani? Ukiwauliza Wizara ya Elimu wanasema yametoka TAMISEMI, ukiwauliza TAMISEMI wanasema Wizara ya Elimu haiwezi kutuingilia mambo kama haya. Jamani tunakwenda wapi katika nchi hii? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, leo Mheshimiwa Profesa hapa amezungumza jambo kubwa sana, hebu tutafute regulator wa elimu ni nani hapa nchini? Kwa sababu kama nilivyosema mwaka juzi, TAMISEMI wana shule zao, wanatakiwa wawe na mikakati yao namna ya kuendesha vipindi mashuleni na kufaulisha. Shule za Seminari zina utaratibu wao na shule za private zina utaratibu wao. Haya mambo yanatokea wapi? Leo hii wanasoma katika ile Kalenda yao, maana yake hakutakuwa na revision za topics. Maana wameacha wiki moja kabla ya mtihani wa mwisho kwa mwanafunzi wa Darasa la Saba ama wa Form Four ama wa Form Two ama Form Six maana yake nchi nzima hakutakuwa na revision katika masomo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hata kama ni somo gumu la hesabu, hakutakuwa na topic ya kufanyia revision kwa sababu Kalenda ile inamtaka mwanafunzi asome hiki na kile, hata kama shule inakuwa kwenye mfumo wa michepuo; kwa mfano, shule niliyosoma mimi O’level, Mbeya Sekondari, ina 15. Masomo kama ya cookery yako pale, masomo ya dini yako pale na masomo mengine na vile vile masomo ya sayansi na ya biashara. Pia kuna shule za Kata kule Kapalala ina masomo nane mpaka tisa, unakuja kuwawekea ratiba moja katika mwaka mzima kwamba wataenda Pamoja; haliwezekani jambo kama hili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naiomba Serikali isitishe jambo hili, ni baya. Siyo kwa shule za private tu, hata kwa shule za Serikali jambo hili ni baya, haliwezekani. Wanatuvurugia elimu nchini. Kila mtu akiamka, anakuja anasema hili. Umekuta mtu anasema kwenye TV; mara, kuanzia leo hakuna likizo za wanafunzi. Yaani mtu anaamka tu anakuja kuongea jambo kama hili. Elimu ni shirikishi. Watushirikishe wadau, tuwe tunaongea masuala ya elimu. Hakuna mtu ambaye amezaa mtoto wake peke yake hapa. Wote wamezaa watoto hapa, twendeni kwa pamoja. (Makofi)

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. PHILLIPO A. MULUGO: Mheshimiwa Mwenyikiti, naunga mkono hoja. (Makofi)