Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Dr. Alice Karungi Kaijage

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ili nichangie. Nianze kwa kumshukuru Mheshimiwa Rais na Serikali yake kwa kuendeleza mapambano dhidi ya matatizo haya makubwa na ambayo ni mtambuka, masuala ya UKIMWI, kifua kikuu, dawa za kulevya na magonjwa yasiyoambukizwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sote tunafahamu kwamba magonjwa yasiyo ya kuambukiza ni magonjwa yale ambayo tunasema hayana vimelea vinavyosambazwa. Hata hivyo, tafiti zinaonesha kabisa kwamba magonjwa yasiyo ya kuambizwa limekuwa ni tatizo kubwa sana na bahati mbaya niseme kwamba the latest study ni ya mwaka 2016 ambayo imekuwa-reported na Shirika la Afya Duniani (WHO), inasema katika vifo 43 vya mwaka 2016 asilimia 71 vilikuwa ni vya magonjwa yasiyo ya kuambukizwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna study nyingine zinazoendelea duniani, zinasema kufikia mwaka 2050 kutakuwa kuna ongezeko kubwa sana la wazee, wanamaanisha kuanzia miaka 65 kwenye study yao. Wanasema asilimia 68 ya wazee hao itakuwa Afrika, Tanzania ikiwa mojawapo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni suala lisilopingika kwamba magonjwa yasiyoambukiza kweli sasa hivi yanayakuta makundi yote, lakini asilimia kubwa ni wazee na ni magonjwa yanayochukua muda mrefu na tiba yake takriban ni ya kila siku, ni magonjwa ya kudumu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nasema hili ili kuonesha ukubwa wa tatizo. Kwa hivyo naungana na wenzangu waliotangulia, lakini labda niwe specific zaidi. Niseme, Wizara ya Afya inafanya kazi nzuri sana katika kupambana na janga hili, lakini ifikie mahali sasa, kwa sababu magonjwa haya kwa asilimia zote ni magonjwa yanayozuilika, ni kwamba watu tu hawana uelewa. Hata tunapokaa sisi hutakiwi kukaa zaidi ya saa moja, lazima uinuke utembee.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna alimu kubwa ambayo jamii haiifahamu. Kwa hiyo utaona msingi wa matatizo haya ni sehemu ya kuzuia (prevention). Tungeiachia Wizara ifanye suala la tiba, lakini suala la prevention, kama tulivyoshauriana liwekwe chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu na liundiwe tume. Kwanza tukishazuia pia tutapunguza burden kwa Serikali na kwa Wizara. Kwa hiyo tume hii ikiundwa, au chombo hiki kikiundwa, kwanza hawa watu watakuwa dedicated na watakuwa answerable na wataweza kusimamia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunazo sheria nyingi sana, tumezipata humu humu ndani, sheria zisizopungua 60 ambazo zinasaidia kuzuia magonjwa ya kuambukiza. Hata hivyo, sheria zile ni nani anazisimamia? Wizara imeelemewa. Kuna miongozo imewekwa, hata hivi siku za karibuni umetoka mwongozo, umeshaenda kwenye halmashauri zetu zote, lakini, ni nani anazisimamia? Wizara imeelemewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, suala la prevention ya magonjwa yasiyoambukiza na ambayo ndio msingi wa kuzuia magonjwa haya, hebu tuangalie namna ya kulifanya. Wawe watu ambao watakuwa very dedicated, watakuwa na mipango na watatupa taarifa.

Nashauri hivyo, kwamba sasa ifikie mahali tutambue ukubwa tatizo hili, tuishauri Serikali iangalie utaratibu wa kupambana, kwa maana ya kuzuia. Kwa sababu tukizuia, ukitoa elimu, kwa sababu ukishaunda chombo cha kuzuia kitatoa elimu kwa wakati, kitakuwa kina bajeti na kitafanya mambo yote. Ukishazuia na ukishatoa elimu ina maana hakuna matokeo ya ugonjwa kwa ukubwa wake.

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba dakika moja.

MWENYEKITI: Ahsante, Mheshimiwa, hitimisha kwa dakika moja.

MHE. DKT. ALICE K. KAIJAGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba pia nishauri kuhusu kuongeza bajeti kwa Mamlaka ya Kuzuia na Kupambana na Dawa za Kulevya. Huku tunaona operations zao ni nyeti, wanahitaji vyombo muhimu vya maabara, watu wanao-graduate kwenye methadone wanahitaji pia wapate study za kazi; mambo ni mengi sana kwenye mamlaka hii.

Kwa hiyo nazidi kushauri, kama nilivyoshauri mara ya kwanza, hebu tuanglie bajeti ya hawa watu ili kuwawezesha waweze kufanya kazi kwa urahisi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja. Ahsante. (Makofi)