Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Tecla Mohamedi Ungele

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. TECLA M. UNGELE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipatia nafasi ili nami nichangie hoja hii iliyotolewa na Kamati ya Masuala ya UKIMWI, dawa za kulevya, kifua kikuu na magonjwa yasiyoambukiza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote tunamshukuru na tunampongeza Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuendeleza na kuongeza ujenzi wa madarasa katika shule zetu ili kupunguza msongamano wa wanafunzi katika madarasa hayo. Msongamano huo ndio uliokuwa unaleta magonjwa ya maambukizi ikiwa ni pamoja na kifua kikuu na mengineyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mchango wangu nitauelekeza kwenye kifua kikuu na ukoma. Kifua kikuu ni ugonjwa mkubwa na ni tatizo kubwa nchini Tanzania. Tunaona Tanzania ni miongoni mwa nchi 30 ulimwenguni zenye maambukizi makubwa ya kifua kikuu; mwaka 2019 kulikuwa na wagonjwa 137,000. Kikubwa zaidi, kwa kifua kikuu kama mgonjwa hakugundulika mapema na hakupata matibabu mapema basi kuna hatari ya kwenda kwenye kifua kikuu sugu na hatimaye kusababisha kifo. Mgonjwa wa kifua kikuu asipopata matibabu anaambukiza watu wengine 10 mpaka 20 kwa siku. Hilo ni tatizo kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nitachangia kuhusu ugonjwa wa ukoma. Bado ukoma ni tatizo kwenye nchi yetu; na ukoma nao unaambukiza kwa njia ya hewa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, takwimu zinaonesha mwaka 2019 kulikuwa na wagonjwa 1,600 nchini, lakini pia hata kihistoria ugonjwa wa ukoma una asili fulani ya unyanyapaa. Kwa hiyo kuna hatari wagonjwa hawajitokeza. Sasa, ushauri wangu ni kwamba, kuimarisha elimu ya afya katika jamii, lakini pia kutumia kikamilifu kada ya community health workers nchini kwetu. Tumeona sasa hivi wanaajiriwa kama medical attendance, lakini kada hii ilikuwa specifically kwa ajili ya kwenda kwenye jamii na ndiko watakakoshughulika na magonjwa haya sugu, kugundua wagonjwa wa kifua kikuu na maambukizi mengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia nashauri kuwe na mafunzo maalum, iwe short courses ama course za muda mrefu kwa ajili ya kukabiliana na magonjwa ambukizi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naunga mkono hoja.