Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

Hon. Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Huduma na Maendeleo ya Jamii kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021 pamoja na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Masuala ya UKIMWI kuhusu Shughuli za Kamati kwa Mwaka 2021

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa fursa na kuweza kuweka mchango wangu katika hoja zilizowasilishwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote naunga mkono hoja. Baada ya kuunga mkono hoja naomba nijikite katika mambo makuu matatu; jambo la kwanza ni afya, hususan katika taasisi ya MSD, jambo la pili nitazungumzia kidogo kuhusu elimu na baadaye nitazungumzia kuhusu Baraza la Michezo Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika taarifa ya huduma na maendeleo ya jamii iliyowasilishwa, moja ya changamoto kubwa ambayo imekithiri ni upungufu wa dawa nchini. Ukifuatilia hata katika ground, huko site, utakubaliana na mimi kwamba, pamoja na upungufu mkubwa wa dawa zipo dawa ambazo katika maeneo yote hazikuwahi kuwa tatizo, dawa hizo ni kama panadol na paracetamol.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siri ya uwepo wa hizo dawa muda wote ni kwa sababu, sehemu kubwa ya dawa hizi zinazalishwa nchini kupitia Kiwanda cha MSD pale Keko. Kupitia kiwanda cha Idofi kule Makambako Njombe ambacho kinazalisha vifaatiba na tayari kinajiwekeza katika kuzalisha dawa zaidi nchini. Tumekuwa na fursa nzuri ya kuweza kupata baadhi ya dawa ambazo zinatosheleza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ni nini maoni yangu katika jambo hili; Serikali sasa iamue kwa dhati kuwekeza kwa nguvu katika kuanzisha viwanda vya dawa nchini. Viwanda vya dawa nchini ndio njia pekee ambayo itatuondosha kwenye kadhia hii kubwa nchini ya upungufu wa dawa kwa binadamu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan, anafanya kazi kubwa sana katika ujenzi wa miundombinu ya kutolea huduma nchini. Tumeona madarasa mengi sana yamejengwa katika eneo la elimu, tumeona vituo vya afya na zahanati zinaendelea kujengwa kwa wingi sana, lakini majengo hayo hayatakuwa na tija ya kutisha kama hatutakuwa na vifaa pamoja na dawa katika zahanati na vituo vyetu vya afya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja ya eneo ambalo linakwamisha sana upatikanaji wa dawa ni namna ambavyo dawa zinaingizwa nchini. Imeelezwa kwamba, dawa mpaka ifike kwa mlaji ikiagizwa kutoka nje inachukua kati ya miezi sita mpaka miezi nane. Kipindi hicho inawezekana dawa nyingine ikawa tayari imeanza kuelekea kwenye kwisha kwa muda wake wa matumizi. Hali hii imesababisha hasara kubwa kwa Serikali kupitia MSD na dawa nyingi zimeangamizwa kwa kupita muda wake wa matumizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuzingatia kwamba, bado tuna upungufu mkubwa wa dawa katika maeneo yetu, ushauri wangu ni kwamba, namna ambavyo tunaweza tukatatua jambo hili ni kuhakikisha kwamba, sasa tunaenda kwa dhati kuwekeza katika ujenzi wa viwanda vya dawa nchini. Hilo liende sambamba na ajira za watumishi wa idara ya afya, hilo liende sambamba na ule Muswada wa kuhakikisha kwamba, sasa tunapitisha huduma ya afya kwa wote nchini. Tukiwezesha hayo, tutakuwa tumetatua kadhia hii ya huduma ya afya kwa wananchi wetu hapa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo lingine ni katika suala la elimu. Kwa kipindi kirefu binafsi tangu nimeingia kwenye Bunge hili nimekuwa nikiuliza maswali, lakini nilikuwa nikichangia ni namna gani Serikali ina-accommodate wale vijana ambao wanashindwa kuendelea na masomo baada ya kuwa wameshindwa mitihani katika level ya darasa la sab ana kidato cha nne au kidato cha sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, namna pekee ya kwenda ku-accommodate vijana hawa ni kutoa elimu ya ufundi kwa mikopo. Nashukuru sana maoni ya Kamati yamelimeweka hili jambo vizuri. Nisisitize, kwa kuwa, Serikali hii ni ya watu wote si ya wale ambao wanafaulu peke yake, Serikali hii inawahusu wale pia wanaoshindwa mitihani, ni vizuri sasa ikaja na utaratibu mzuri wa kuweza kuwa-accommodate hao kupitia vyuo vya ufundi kwa kuwapa mikopo ya kufanya masomo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ajili ya muda suala la BMT nitalizungumza siku nyingine. Naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)