Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kudumu Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu shughuli za Kamati hizo kwa Mwaka 2021

Hon Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

3

Ministries

nil

Taarifa za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kudumu Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu shughuli za Kamati hizo kwa Mwaka 2021

MHE. ALLY J. MAKOA – MWENYEKITI WA KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA ARDHI, MALIASILI NA UTALII:
Mheshimiwa Spika, ninakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuhitimisha hoja. Nawashukuru Waheshimiwa Wabunge kwa michango yao mizuri ambayo kwa kweli imezidi kutuimarisha na ninadhani Serikali imesikia. Ninawashukuru Mawaziri waliochangia lakini kipekee kabisa nimshukuru Waziri Mkuu kwa maelekezo yake mazuri ambayo ameyatoa hapa mbele ya Bunge, ni matumaini ya Kamati kwamba sasa Serikali itakwenda kuyafanyia kazi mawazo ya Waheshimiwa Wabunge.

Mheshimiwa Spika, pamekuwa na hisia kubwa sana kwa upande wa Ngorongoro lakini lazima na Bonde la Kilombero na lenyewe litiliwe mkazo kama jinsi ambavyo Ngorongoro inavyotiliwa mkazo kwa sababu Bonde lile na lenyewe likiachiwa yatakuja kutokea madhara makubwa pengine kama haya yanayoweza kutokea Ngorongoro.

Mheshimiwa Spika, baada ya kuyasema hayo, sasa ninaomba kutoa hoja kwamba Bunge likubali kupoipokea taarifa yetu.

Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja. (Makofi)

MHE. NEEMA W. MGAYA: Mheshimiwa Spika, naafiki.