Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kudumu Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu shughuli za Kamati hizo kwa Mwaka 2021

Hon. Elibariki Emmanuel Kingu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Magharibi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa za Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii na Kamati ya Kudumu Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama kuhusu shughuli za Kamati hizo kwa Mwaka 2021

MHE. ELIBARKI I. KINGU: Mheshimiwa Spika, kwanza kabisa nami niungane na Wabunge wenzangu kukupongeza wewe binafsi kwa nafasi ambayo Wabunge tumekuchagua kwa kishindo. Hongera sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Taifa hili la Tanzania bado nina imani kwa dhati ya moyo wangu kwamba mambo mema na ya msingi ambayo Taifa letu yameyarithi toka kuanzia zama za Waasisi wa Taifa letu, it is my trust kwamba kizazi hiki cha leo kikiamua kwa dhati na kwa dhamira ya kuangalia maslahi ya nchi mbele na maslahi ya vizazi vinavyokuja, tuna uwezo kabisa wa kulilinda Taifa hili tukafanya maamuzi Taifa hili likabaki moja, Taifa hili likabaki kuwa la mshikamano, Taifa hili likaendelea kuwa la upendo na likadumisha tunu za umoja na mshikamano ambazo ndizo zimekuwa asili ya Taifa hili ambalo limekuwa likipigiwa chepuo kwa mifano duniani bila kuleta migogoro. Tumekuwa na sifa hiyo ya Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Watanzania tumekuwa na sifa ya kutatua matatizo yetu wenyewe na kuliacha Taifa likiwa moja na likiwa na mshikamano. Naomba niseme maneno mafupi yafuatayo: -

Mheshimiwa Spika, demographic projection ya Hifadhi ya Ngorongoro kwa miaka 35 inayokuja, naiona Ngorongoro ya miaka 35 inayokuja ikiwa na population ya zaidi ya watu 800,000 mpaka 900,000. Naiona Ngorongoro ya miaka 40 inayokuja ikiwa na viwanda ndani ya hifadhi, naiona Ngorongoro inayokuja ikiwa na mitambo ya mashine kwa ajili ya ku-cater for population ambayo itakuwa pale.

Mheshimiwa Spika na ndugu zangu Wabunge, naomba nizungumze haya kwa dhati ya moyo wangu, nikitanguliza maslahi ya Taifa langu mbele na kuweka ubinafsi wangu nyuma. Nataka niwaambie Watanzania, na naomba Bunge linisikilize kwa makini. Haya mambo tunayozungumza habari ya heritage ya dunia kwa Ngorongoro hatuzungumzii tu heritage ya dunia kwa sababu inaleta revenue zinazolisaidia Taifa letu, lakini tunazungumzia misingi ya historia ambayo Taifa hili Mungu amelipatia tuvirithishe vizazi vya wajukuu zetu na wajukuu wa wajukuu zetu kwa nature ya utajiri ambao Mungu amelipatia Taifa hili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nayasema hayo kwa sababu na nitakuwa mtu wa hovyo sana kama nitatanguliza mambo ya ukabila kuzungumza sijui Umasai, kwangu mimi hoja siyo Mmasai aliyeko Ngorongoro, kwa sababu wale ni Watanzania, raia wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Hoja ninayoizungumza; je, Taifa hili la kizazi cha sasa hivi tuko tayari kuona heritage ambayo Mungu ametupatia kama nchi ikipotea bila kufanya maamuzi? Hiyo ndiyo hoja ya msingi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukienda kwenye hoja hiyo ya msingi wote kwa pamoja tutarudi kama Taifa, tutatengeneza resolutions za kwenda ku-approach lile eneo. Nataka nikuhakikishie jambo hili litamalizika kwa amani na utulivu na maslahi ya Taifa hili yatakuwa yamelindwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, ndugu zangu, nataka niwaambie kitu kimoja; ukiachilia mbali habari ya mifugo tunayoizungumza, lakini kuna taarifa ambazo kama siku moja ukiniruhusu nitazileta mezani kwako kama ushahidi. Kuna taarifa ambazo zinaonesha, sitaji kwa jina, mataifa ya jirani kuna hujuma kubwa inafanyika katika Hifadhi ya Ngorongoro. Kuna idadi ya wanyama wengi wanaletwa na mataifa jirani na lengo lake ni vita vya kitalii kupambana kati ya Mataifa ya East Africa. Sisi kizazi cha leo we are not ready kuona Ngorongoro inatufia katika mikono yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nayasema haya kwa uchungu mkubwa kwa sababu haya yanayofanyika kule ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro ukiachilia mbali modernization ya housing ambayo inaendelea kule ndani, lakini ninachotaka kusema ni kwamba population ya watu kutoka mwaka 1959, watu 8,000 na kwa kweli huwezi kuzuia watu walikuwepo mle kwa mujibu wa sheria, lakini tujiulize swali; sheria ile iliundwa wakati ule ilikuwa imelenga nini kwa wakati ule? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kama sheria tulikuwa tumeiunda sisi wakati ule Bunge hili ndicho chombo peke yake cha Kitaifa chenye mamlaka ya Kikatiba ya kubadili sheria na kutunga sheria zinazolinda maslahi ya nchi na kulinda maslahi ya vizazi vinavyokuja katika Taifa letu.

Mheshimiwa Spika, ombi langu kwa Serikali na nataka niliseme hili kwa dhati kabisa kwa Serikali; mzigo huu tusiutupe kwa ile jamii ya watu walioko pale Ngorongoro peke yao. Serikali kwa upande mwingine kuna mahali ilikosea, kwa sababu haiwezekani nyumba za ghorofa zinajengwa Ngorongoro inaangalia, modern houses zinajengwa inaangalia, watu walitakiwa kuchukua hatua mapema. Hivi ninavyozungumza naona kabisa yaani kama vile maamuzi haya tulikuwa tuyafanye jana na siyo leo kwa maslahi ya kulinda ile Hifadhi ya Ngorongoro. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naiomba Serikali ya chama changu chini ya Rais wetu shupavu, mama Samia Suluhu Hassan, juzi Rais amefanya royal tour tumeona impact ya ongezeko kubwa la watalii katika Taifa letu. Tumeona impact kubwa ya ongezeko la mapato katika Taifa kutokana na royal tour. Ombi langu, Serikali ifanye engagement ya Kimungu kwa hawa watu walioko katika hifadhi. Imani yangu ni kwamba engagement ya kuzungumza na wafugaji hawa ikifanyika kwa ustaarabu Watanzania ni Taifa la watu wasikivu, tutamaliza mgogoro ule bila kuleta vurugu ambazo dunia inaweza ikatucheka kesho. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa yale yanayoendelea katika Hifadhi ya Ngorongoro nitakuwa Mbunge ambaye nimeweka rekodi mbaya kwa Taifa langu nikisema Serikali msichukue hatua ya kulinda ile hifadhi. Hatua hii ya kulinda hifadhi inatakiwa ifanyike haraka na kwa maslahi mapana ya Taifa, lakini wakati huohuo tulinde mambo yote yanayohusiana na humanity kuhakikisha kwamba watu hawa wanatafutiwa mahali ambapo watakuwa comfortable na shughuli zao za ufugaji, watakuwa comfortable na shughuli zao nyingine za kiuchumi. Lengo ni kuhakikisha kwamba Taifa hili linabaki kuwa moja.

Mheshimiwa Spika, hizo statistics alizokuwa nazisema Mheshimiwa Salome Makamba, mimi nimekwenda mbali, hizo statistics nina orodha kama utaniruhusu naweza siku moja nikakuletea kwenye meza, ya baadhi ya watu ambao ni wafanyabiashara wa mifugo, wamewatumia watu ndani ya hifadhi na kuweka mifugo ndani ya hifadhi na ndiyo hao wamekuwa wakipaza sauti kubwa sana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, wewe jiulize kama statistics za Serikali zinaonesha ufukara ni asilimia 50, inakuwaje watu wawe na mifugo zaidi ya 800,000 au 900,000 wasemekane ni maskini? Hayo ni maswali ya kujiuliza kama nchi.

Mheshimiwa Spika, Waziri Mkuu wetu yuko hapa.

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo, kwa unyenyekevu mkubwa, naunga mkono hoja, ahsante sana. (Makofi)