Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

Hon. Dr. Advocate Damas Daniel Ndumbaro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Songea Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa hii. Nichukue nafasi hii kumshukuru sana Mwenyekiti wa Kamati Mheshimiwa Rweikiza; Makamu Mwenyekiti, Mheshimiwa Ridhiwani na Wajumbe wote wa Kamati ya Sheria Ndogo kwa michango yao kwa mawazo yao, kwa maelekezo yao ambayo wameitoa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda niongelee eneo moja linalohusu zuio au katazo kwa askari wetu wa Jeshi la Uhifadhi wa Wanyamapori na Misitu wasiweze kufanya shughuli nyingine. Hili ni moja kati ya Jeshi Jipya ambalo limeanzishwa mahususi kabisa ili kulinda rasilimali ambazo tunazo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Tanzania ni nchi ambayo inasifika sana kwa kuwa na rasilimali za maliasili bora kabisa duniani. Rasilimali hizo zinapaswa kuendelea kulindwa na ndiyo maana Serikali iliona umuhimu wa kuanzishwa kwa Jeshi la Uhifadhi wa Wanyamapori na Misitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulichokifanya kwenye Kanuni hiyo ni kujaribu kuimarisha utendaji na nidhamu ya Jeshi, kwa kuondoa uwezekano wa kuwepo kwa mgongano wa kimasilahi. Kwa sababu, askari hawa ambao wanafanya kazi katika maeneo ya maliasili na utalii, wasije wakashawishika na wao kujiingiza katika shughuli zinazofanana na maliasili na utalii. Tukiruhusu hilo, baada ya kulinda rasilimali hizo watakuwa wao wanazitumia kupitia shughuli zao za ziada wanazozifanya. Kwa hiyo, hatuwazuii kufanya shughuli nyingine kama za kilimo au biashara nyingine yoyote ili mradi isiingiliane na masuala ya uhifadhi na utalii na isiwe na mgongano wa kimasilahi na mwajiri wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunashukuru kwa Kamati kuibuka na hoja hiyo. Tumejadili na Kamati na tumewaeleza kwamba nia ya Serikali siyo kujaribu kuwakomoa askari hao; siyo kujaribu kuwatoa kabisa na kuwaongezea umasikini, la hasha, ni kuleta nidhamu na kuondoa uwezekano wa kuwepo mgongano wa kimasilahi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tufahamu kwamba askari hawa wanapewa silaha, wanakabidhiwa kulinda hayo maeneo. Sasa ukiwaruhusu wafanye shughuli za kibiashara, kwenye maeneo ambayo wamekabidhiwa kulinda, kwanza wata-take advantage dhidi ya private sector nyingine, kitu ambacho tutakuwa tunakwenda kuua private sector yetu; na pili, kutakuwa na uhujumu wa rasilimali hizo kwa sababu anayelinda unamruhusu pia aweze kuzivuna au kuzitumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa hoja na kuwasilisha. Ahsante. (Makofi)