Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

Hon. Santiel Eric Kirumba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

MHE. SANTIEL E. KIRUMBA: Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote napenda kukushukuru kwa kunipatia nafasi hii ya kuchangia katika hii Kamati ya Sheria Ndogo nikiwa kama Mjumbe. Kuna mambo madogomadogo, kwanza katika sheria hizi zinazotungwa ni sheria ambazo zinaweza kutuingizia mapato sisi katika halmashauri zetu na sheria hizi zinagusa mwananchi directly. Kwa hiyo tunapozitunga lazima tuangalie sheria hizi zinaendana na uhalisia wa maisha ya mwananchi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapenda kuishauri Serikali iwe inapitia kwa karibu sheria hizi kabla hazijafika mbali na kabla hazijaanza kutumika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kuzungumzia suala moja; katika GN ya tarehe 9, Julai, Na. 589 ya The Wildlife Conservation, sheria hii kifungu cha 12(4) hakimpi mamlaka Waziri kutunga sheria na badala yake kinakinzana na sheria mama ambayo imemruhusu katika Kifungu cha 121(a) ambayo Waziri anapewa mamlaka kutunga sheria zozote ambazo zinamhusu. Kwa hiyo tunapenda kama Waziri husika afanye marejeo anapotunga sheria zake, aangalie kifungu hicho mama kinamwelekeza nini ili aweze kufanya kazi yake hii kwa ufasaha. Hata hivyo, ni watu ambao wanafanya kazi vizuri na tumeshirikiana nao vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika hiyohiyo GN ya Julai 9, 2021 Na. 589, hili ni jambo lingine la kushangaza, The Wildlife Conservation Act inaelezea kwamba mtu yeyote aliyeajiriwa katika Jeshi Usu haruhusiwi kufanya kazi nyingine yoyote, unapomaliza kazi uende ukapumzike. Wanaelewa kabisa hawa watu tulivyowaajiri vipato vyao ni vidogo, unapomwambia asijihusishe na kazi yoyote, ile sheria uliyotunga inakinzana na sheria mama ya Labour Act, unless uwe na conflict of interest katika lile jambo, lakini hakuna, unamwambia anapomaliza kazi yake asiende kufanya shughuli yoyote, sidhani kama hili liko sawa. Wabunge wanaelewa vipato vyetu ni vidogo, uambiwe usijihusishe na jambo lolote au na shughuli yoyote, unapomaliza shughuli zako za Bunge uende ukapumzike; kweli itaweza kufaa?

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba Mheshimiwa Waziri arudie tena hiki kifungu, akipitie. Unless kama haipingani, haina conflict of interest, awaruhusu hawa watu waweze kuendelea kufanya kazi zao nyingine. Kwa sababu mnaelewa hawa Jeshi Usu mishahara yao jinsi ilivyo midogo. Tukiendelea kufanya sheria ambazo zinawabana wananchi wetu wasijiingizie kipato, wasifanye shughuli nyingine, hiki kitu ni changamoto sana. Halafu kingine, inatengeneza hali ya uchonganishi na Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vitu ambavyo vinaongeleka, ni vitu ambavyo vinasaidika na ni vitu ambavyo vinawezekana. Naomba Mheshimiwa Waziri na Naibu Waziri wako hapa na tulikuwa nao kwa pamoja, waipitie hii kanuni ya 24 iweze kuwapa uhuru hawa Jeshi Usu kufanya kazi nyingine. Naelewa wanaelewa kazi ngumu ambayo wanaifanya na hawa watu wanafanya kazi ngumu sana, lakini kama haiathiri sheria zao, naomba waruhusiwe hawa watu kufanya shughuli nyingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ya kwangu ni hayo, nashukuru sana. (Makofi)