Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

Hon. Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

MHE. KILUMBE S. NG’ENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nami nachukua nafasi hii kukushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuchangia na nilitaka nijielekeze moja kwa moja katika yale tuliyoyaona kwenye Sheria Ndogo hizi. Wenzangu waliotangulia wameeleza vizuri juu ya tatizo linaloonekana la Sheria Ndogo kuanza kutumika kabla ya kupita kwenye mamlaka ya Bunge na wanataka, mamlaka zinazotunga Sheria hizi ndogo ziwe makini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka kuongeza neno jingine kwamba lazima Bunge lifikirie kubadili utaratibu huu uko mbele na kwamba Sheria ndogo zote ziwe kwanza zinadhibitishwa na ndiyo zinakwenda kutumika. Maana inawezekana umakini wengine wakaukosa na mkazusha malalamiko. Kwa hiyo, huko mbele mpaka sasa Sheria bado inatoa mamlaka ya kutunga kwa Sheria Ndogo na kuanza kutumika lakini huko mbele tunaweza tukafikiria kwamba mpaka ifike kudhibitishwa na kukubaliwa na Bunge ndiyo ianze kutumika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika maeneo tuliyo experience kwenye masuala ya Sheria Ndogo ipo vile vile Sheria Ndogo ya Uhifadhi na Usambazaji wa Madawa yaani The Tanzania Medicine and Medical Devices Good Storage and Distribution. Hapa napo tumekuta kuna tatizo na changamoto, moja ya changamoto tuliyoiona kwamba Sheria hii Ndogo kwanza inampa mamlaka mhifadhi na msambazaji wa dawa yeye mwenyewe kupokea malalamiko ya dawa zinapokuwa na matatizo, na wakati yeye ni mdau katika jambo hilo, wakati mwingine manufacturer wa hiyo dawa yuko nje ya nchi lakini huyu aliyepokea na kuzihifadhi katika uhifadhi na ushasafirishaji dawa inaweza ikapoteza ubora na baadaye ikaenda kuleta madhara yeye mwenyewe Sheria Ndogo ilikuwa inampa nafasi ya kusikiliza malalamiko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hii ni tofauti na Sheria nyingine, leo hii ikifika mahali ambapo kuna malalamiko ya mamlaka za kutoa mawasiliano kama vile vyombo, Voda sijui Airtel na wengine kuna regulatory authority ya kwao ambayo ni TCRA ndiyo itapokea malalamiko. Kwa hiyo, tulitaka mamlaka haya ya kupokea malalamiko ya juu ya storage ya madawa yanayopoteza ubora ya baki TMDA na yasiende kwa wale ambao ni owner wa premises za kuhifadhi. Kwa hiyo hilo ni moja la tatizo tuliloliona. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jingine ni suala la dawa kupoteza ubora wakati zikiwa katika maeneo ya storage na usafirishaji. Na kwamba lazima huko mbele hizi Sheria Ndogo zifikirie kuwe na utaratibu wa ku-recall yaani ambao unaweza ukafika mahali kukawa na utaratibu maalumu wa kuzirudisha dawa zilizoharibika kutoka kwa hawa ambao ni owner wa premises na wale ambao wana- distribute hizo dawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, katika jambo jingine ambalo tume-experience ni kwamba utungaji wa hizi Sheria Ndogo vilevile wakati mwingine unakumbana na changamoto za kiutafiti. Kwa mfano; Sheria za Uvuvi hizi Sheria Ndogo za Uvuvi zimeweka mambo mengi ambayo yanakinzana na hali halisi ya uvuvi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa, lakini unachunguza unakuta Wizara yenyewe ya Uvuvi na Mifugo inapewa bajeti ndogo sana. Kwa hiyo, katika masuala ya utafiti wanapata shida. Kwa hiyo, wanatunga kanuni kwa kuzingatia jinsi ambavyo wao wanavyofikiria zaidi kulikoni kufanya utafiti.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mfano; Ziwa Tanganyika ambalo lina kina cha zaidi ya mita elfu moja na kidogo, lakini eneo la oxygen ambalo linaweza linakaa viumbe kama Samaki ni mita 150. Lakini ukiangalia katika kanuni walizozitunga wanamkataza mvuvi kuvua kwa zaidi ya mita 20. Kwa hiyo, kuna mita 150 nzima ambayo ipo pale ambalo ni eneo linaweza likavuliwa na hao wakapata mazao ya uvuvi na ambalo lina oxygen, lakini kanuni ile wala haifikii mita 20. Sasa hivi ndiyo tulikuwa tunafikiria wafikie mita 20, lakini kanuni ile ilikuwa inataka nyavu ziwe na macho 144 ambayo ni sawa sawa na mita 16. Kwa hiyo, haya ni mambo ambayo tunaona yanakinzana na mahitaji ya wavuvi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, jingine ambalo tuliliona hili si la kiutafiti ni la kimlamlaka tu kwenye suala la uvuvi, wavuvi wameongezewa mzigo sana chombo chenyewe cha uvuvi kinalipa leseni. Lakini mvuvi mmoja mmoja anayeingia kwenye uvuvi naye kwenye kanuni hizi amewekewa leseni kila mvuvi awe na leseni. Na mbaya zaidi wavuvi hawa wanahama kutoka chombo kimoja kwenda chombo kingine akihama kutoka chombo kimoja kwenda chombo kingine ile leseni yake haitambuliki akifika kwenye chombo kingine lazima akate leseni nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tumeona katika utungaji wa Sheria hizi Ndogo kuna maeneo ambayo yanakinzana na hali halisi na kwa maana hiyo yanaleta ugumu katika kupata tija kwa watu wanaofanya shughuli kwenye sekta hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana naunga mkono hoja. (Makofi)