Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

Hon. Ramadhan Suleiman Ramadhan

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chake Chake

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

2

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

MHE. RAMADHAN SULEIMAN RAMADHAN: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kupata fursa hii ya kuchangia kwenye hoja iliyoletwa mezani leo kutoka Kamati ya Sheria Ndogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, awali ya yote kabla ya kutoa mchango wangu napenda kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kunipa nguvu na uwezo wa kusimama kwenye Bunge lako Tukufu leo kutoa maoni yangu pia nimuombe Mwenyezi Mungu huyo huyo aendelee kumpa nguvu Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassain anapotekeleza majukumu yake ya kitaifa akiwa nje ya nchi muda huu akiwa Misri Mungu ampeleke salama na amrejeshe salama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa wachangiaji waliopita kama watatu kuanzia Mheshimiwa Ridhiwani, Mheshimiwa Advocate Swalle na Kaka yangu Simai umeshaanza kuona picha kubwa ya jinsi sheria ndogo zinavyoleta changamoto. Bahati sijui niseme nzuri au mbaya kwa utaratibu wa kanuni za nchi yetu sisi Sheria zetu ndogo zinaanza kutumika kabla hazijaja kwenye Kamati ya Sheria Ndogo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake zinatolewa kwenye gazeti baada ya kutungwa halafu zinaingia mtaani zinaanza kufanya operation ya matumizi yake halafu baadaye zinakuja kwenye Kamati ya Sheria Ndogo kwa ajili ya uchambuzi ya kuona kwamba yale tuliyoelekeza watunga sheria yameendana na maelekezo ya Bunge? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa shida inapotokea ni kwamba sheria zinaweza zikawa zimeanza kufanya operation mtaani na zimeanza kutumika halafu sisi tunakuja kuona madhahifu yaliyomo mpaka tukiwaambia Serikali wakaribishe baadhi yao tayari zimeshaumiza watu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunapotoa msisitizo wa kipekee kwa Serikali kuwa makini mara mbili zaidi wanapotunga Sheria Ndogo ndiyo tunatakiwa tuweleweke hapo. Kwamba tunatoa msisitizo kwamba sheria hizi zitaenda kutumika kabla hazijapita kwenye Kamati za Bunge kwa ajili ya kuzi- scrutinize, kuzichunguza kwa makini na sisi kutoa mapendekezo ya yale tunayoyaona yanakosewa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunawaomba Serikali kwa sababu wamepewa mamlaka na Sheria za Bunge katungeni Sheria Ndogo kwenye mambo haya. Kwa hiyo, wanakuwa Kamati zao Ndogo wanakaa kwanza, wanakaa na wadau zinaandikwa zinapita kwa Waziri anazisoma, anazisaini kwa hiyo tunawaomba makini mara tatu zaidi ya kuhakikisha kwamba Sheria Ndogo hizo zinakuwa, zinapokuja kutumika kwenye jamii haziji kumi za watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tulikutana na sheria moja ilikuja kwenye kamati yetu kwa ajili ya uchambuzi hii ya uhifadhi wa wanyamapori ni kanuni ya uhifadhi ya wanyamapori ya mwaka 2021. Kwenye kifungu cha 31 cha kanuni hiyo imekuja kuwapa mamlaka hili Jeshi Husu, Jeshi la Uhifadhi la Wanayamapori, mamlaka ya kufanya upelelezi kukamata, kufanya searching za kwenye majumba na watu ku-secure maeneo ya matukio kufanya surveillance kwa watu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wakati tunachambua tulikuwa tuna wasiwasi haya mamlaka kwa mujibu wa criminal procedures yamewekwa kwa vyombo maalum vinavyofanya upelelezi kwa mfano Polisi. Leo tunayachukua mamlaka haya haya tunaenda kuwapa Jeshi Husu wafanye na wao, siyo shida lakini umakini wa kuhakikisha tuna-control behavior za majeshi yetu wakati wa kufanya haya tunatakiwa tuwe makini mara mbili zaidi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sababu wanaenda kuingia kwenye haki za watu, unapopewa haki ya kumkamata mtu na kumfanyia upelelezi maana yeke utakaa naye, utamuoji lakini kwenye criminal procedure utaratibu wa jinsi polisi na vyombo vingine vya upelelezi vimepewa mamlaka kwa kwa mujibu wa criminal procedure na utaratibu mzuri ambao wao wanaufuata na baadhi ya wakati vyombo hivyo vingine vinampaka ma-PGO, wana code of ethics na conduct za kuhakikiha kwamba hawavuki, na hawaharibu haki za watu wakati wakitekeleza majukumu yao. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, moja katika vitu tunavyowaisitiza ni kwamba wahakikishe michakato ya kuwatungia code of ethics iende kwa haraka ili kuhakikisha kwamba hao waliopewa mamlaka sasa haya sasa hawaendi kuya-abuse haiendi kuyatumia kinyume na yanavyotakiwa kutumiwa kwenye sheria zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huo ndiyo ulikuwa mchango wangu naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)