Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

Hon. Simai Hassan Sadiki

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nungwi

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Sheria Ndogo kuhusu Uchambuzi wa Sheria Ndogo zilizowasilishwa katika Mkutano wa Tatu wa Bunge na Mkutano wa Nne wa Bunge pamoja na Kanuni za Uvuvi za Mwaka 2009

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na mimi kuweza kunipa fursa ya kuchangia jioni hii ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sheria zimetungwa kwa ajili ya ku-regulate human conduct sasa kwa kawaida sheria yeyote inakuwa inaongoza matendo halisi ya mwanadamu, sheria nazo katika utungwaji wake zimekuwa zimekuwa zimewekewa misingi maalum itakayoongozwa katika uandishi wake au maandalizi yake. Sheria Ndogo inapokuwa inaenda kinyume na utaratibu wa Katiba, sheria inapokuwa inaenda kinyume na utaratibu wa Sheria Mama maana yake sheria hiyo inakosa uhalisia katika matumizi yake. Sheria inapokosa uhalisia katika matumizi yake moja kwa moja itakuwa ni batili na haina uhalali wowote kisheria katika kuitumia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maana yake nini, siyo kitu cha busara kwa changamoto zinazojitokeza katika utunzi na uandaaji wa Sheria Ndogo kuletwa hapa Bungeni kila mara na kuweza kujadiliwa. Matatizo haya na changamoto hizi zinazojitokeza takribani Mabunge ya miaka yote kasoro zinazojitokeza ni zilezile. Kamati ya Sheria Ndogo inachukua jitihada za msingi kuisisitiza Serikali juu ya kuzidisha umakini kabisa wakati wanapoandaa hizi sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala linalosikitisha zaidi katika utungaji wa sheria hizi siyo halali kwa Bunge hili kutaka Sheria Ndogo hizi kuingizwa hapa kabla ya kuanza kutumika huko hii ni kwa mujibu wa Tafsiri ya Sheria (The Interpretation of Law Act), Kifungu Namba 37 na 38 (1) maana yake sheria inapokuja hapa Bungeni kuijadiliwa kwanza inakuwa tayari imeshatumika huko kwa wananchi kama wananchi kuumia tayari wameshaumia sana, sasa tutakapokuwa tunakosa u-serious wakati tunapoandaa hizi sheria maana yake nini, moja kwa moja tunaenda kuangamiza wananchi ambao ndio walengwa halisi zinazokoenda kuwasimamia katika utumikaji wa hizi sheria.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatizo la Sheria Ndogo kukosa uhalisia ni tatizo moja kubwa sana. Nakupa mfano sheria nyingi zilizokuja Bungeni kipindi hiki cha Bunge la Mkutano wa Tatu na la Bunge la Mkutano wa Nne zimekosa uhalisia katika matumizi. Nakupa mfano, kuna Sheria Ndogo ya kudhibiti ombaomba ya Wilaya ya Chunya iliyotungwa mwaka 2021 ukisoma hiyo sheria tafsiri yake inaweka wazi inatafsiri ombaomba kwa kumtambua kama mtu ambaye kaanza na ulemavu kitu ambacho ni kinyume kabisa na utaratibu wa Katiba. Katiba yetu ya Jamhuri ya Muungano inahamasisha umoja, mshikamano na usawa kwa binadamu, lakini ukiisoma hiyo sheria kwa undani zaidi utakuja kubaini kwamba ubaguzi ni sehemu inayopewa kipaumbele. Nakupa mfano, ukiangalia Kifungu cha 10 katika hiyo sheria kinasema wazi kwamba Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ana mamlaka ya kumfukuza ombaomba kumrejesha Wilaya alikotoka na katika Mkoa alikotoka kwa kumkabidhi kwa Katibu Tawala wa Mkoa husika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ukiangalia mantiki ya hicho kifungu ni nini, unaweza kujiuliza hivi Mkurugenzi anapopata mamlaka ya kumrejesha ombaomba kwao hivi maombaomba wote wanaoenda Chunya maana yake Chunya hakuna ombaomba au sehemu nyingine ndizo zenye kutoa ombaomba na kupeleka Chunya hiyo moja, lakini unaweza kujikuta kwamba sheria hii mantiki yake ya kutungwa ni nini, tunaelewa hypothetically tunajua mantiki yake ya kutungwa ni nini, lakini lazima izingatie mahitaji ya watu kwa sababu suala la ombaomba siyo Tanzania tu, tunapokuja kumtungia sheria kwamba ombaomba, tumeshamuita ombaomba leo hii tunatengeneza sheria tukimkamata tunampiga faini ya Shilingi Laki Mbili maana yake nini, sasa huyu ombaomba au ni mtu mwenye uwezo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ombaomba duniani kote wapo hata kule Marekani, ombaomba wapo tofauti ni majina tu, sisi tunawaita ombaomba kule wanaita nini homeless people! maana yake unga wa ngano, chapati ya unga wa ngano na andazi vyote ni kitu kimoja vinatumia jamii ya unga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu kingine ambacho kinaonyesha wazi kwamba sheria hizi haziendani na uhalisia halisi wawatanzania soma Sheria ya Uvuvi (The Fisheries Regulatory Act, ya 2009) utaona wazi kwamba hii sheria haiakisi mahitaji ya wananchi walio chini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakupa mfano, ndani ya hiyo Kanuni hiyo unakuja kukuta kwamba miongoni mwa sifa ambazo mtu anatakiwa awe nazo wakati anapoamua kusafirisha samaki nje ya nchi, anatakiwa awe na certificate of incorporation sambamba na hilo awe na article na Memorandum of Association ya kampuni. Haya ni masuala ya kampuni ideological tunaimani kwamba once the company is registered become legal entity lakini kuna tofauti uhalali tunaoipa kampuni kutekeleza majukumu ya kibanadamu tunaiweka kwa misingi ya kwamba iwe na uwezo wa kushtaki na kushtakiwa. Lakini hatuwezi tukamchukua binadamu kuwa na hadhi sawa na kampuni vitu hivi ni masharti ambayo hayawezi yakatekelezeka kisheria. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa tunapoweka mazingira haya lazima tuangalie wale watu wa tabaka la chini. Sheria hii imeenda mbali zaidi cha kushangaza zaidi kwamba wavuvi wamewekewa kina maalumu cha kuweza kuvua tuchukulie mathalani Ziwa Tanganyika lina maji ambayo hayatashuka mita 50, kina cha kwenda chini, lakini sheria ile imeweka mipaka mwisho uvuvi kuvua ni mita 20 kitu ambacho vipi nyavu zao zitakuwa zinavuta hawa samaki wa juu juu tu. Katika mita 150 ambazo zinatakiwa zivuliwe, wewe unaweka mita 20 wewe unayeweka mita 20 maana yake umeacha samaki katika mita 130 hizo umeziacha huru sasa hawa samaki wanauwezo wa kwenda sehemu yeyote.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ikumbukwe kwamba lile ziwa Tanganyika sisi tuna-share na wenzetu nchi kama vile Congo, sasa tunaposema tunawaacha wale samaki sisi, tumejitungia sheria ngumu, sheria ambazo haziwezi kutekelezeka, Congo wao wakienda kule wao watawavua, samaki siku zote hasubiri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, samaki kwanza hana passport atakapotaka kwenda Kongo, kwamba aende akakate passport, aende akaonane na uhamiaji ndipo aende kule, yeye ana uwezo wa kwenda hajijui sasa hivi yuko wapi anaingia wakati wowote na kutoka wakati wowote. Sasa tujaribu kuweka sheria ambazo ni rafiki kwa wananchi wa tabaka la chini, kwa sababu siku zote tunaposema tunapomuwekea mtu sheria rahisi basi inakuwa rahisi kuzifuata, lakini ukiamua kumuwekea sheria ngumu utamuona yule mtu adui. (Makofi)

MWENYEKITI: Malizia sentensi yako.

MHE. SIMAI HASSAN SADIKI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri sana kuzingatia mahitaji halisi ya utungwaji wa sheria. Ahsante sana. (Makofi)