Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Dr. Hamisi Andrea Kigwangalla

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nzega Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. DKT. HAMISI A. KIGWANGALLA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, awali ya yote nianze kutoa mchango wangu kwanza kwa Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Sita, mama Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea shilingi trilioni 1.3. Lakini pili niseme tu ukweli, nilihamasika kuchangia kwenye Mpango huu, awali sikuwa na mpango huo baada ya kauli yako jana, kwamba hizi shilingi trilioni 1.3 zilizoletwa na Mheshimiwa Mama Samia Suluhu Hassan zimeichangamsha nchi. Ni kwa nini na sisi tusiweke Mpango wetu wenyewe kwenye Bajeti inayokuja wa kutenga shilingi trilioni 1.3 au shilingi trilioni1.5 ya kwetu wenyewe kwenye Bajeti? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, wazo hili kwa kweli lilinifikirisha sana na ndipo nikaona niombe kuchangia, ili kuweka msisitizo kwenye jambo hilo. Maana yake ulilisema juu juu hivi halafu likaishia pale nikasema pengine nitoe mawazo yangu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiukweli nakubaliana sana na hili wazo na ninasema hivi kwa sababu, ninaona kuna haja ya kufanya hivyo kutokana na mambo kadhaa ambayo nitayataja. Mojawapo kwanza ni affirmative action kwamba tutakuwa tuna Mpango mahsusi wa nini tufanye na fedha yetu wenyewe. Kwa ajili ya kusambaza keki ya Taifa kila kona ya Nchi yetu kwa maana ya kwenye majimbo yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini la pili, tutakuwa na sababu mahususi za kitu gani fedha hizi ziende zikafanye. Lakini la tatu, tuna stress kubwa sana kwenye uchumi wetu kutokana na namna tulivyoendesha mambo yetu hapo nyuma. Lakini pia kutokana na kuingiliwa na mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19. Kwa hivyo, uchumi umeathirika sana, uchumi una-undergo stress kubwa sana. Kwa ambao ni wahangaikaji, wajasiriamali wenzangu huko mtaani watakubaliana na mimi, hali si shwari kwenye uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili tuweze kurudi kwenye mzunguko mzuri ni lazima Serikali ifanye mambo kadhaa. Mojawapo kiukweli ni kutoa nafasi za ajira kwa wingi zaidi ili watu waweze kuajiriwa. Ama iongeze mishahara, ama iongeze posho kwa maana ya ku-pump fedha kwenye jamii, ili mzunguko uwepo kule watu waweze kutumia uchumi uweze kukua tena. Lakini uchumi wetu kabla ya Covid na kabla ya miaka hii kadhaa hapa nyuma ulikuwa unakua kwa kiwango cha asilimia 7. Sasa hivi unakua kwa kiwango cha asilimia 4 hivi kwenda kwenye asilimia 5 hapo. Maana yake hatuko vizuri sana kwenye economic growth na ili uchumi uweze kukua ni lazima tufanye juhudi za makusudi kabisa za kusukuma fedha kwa wanachi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo hii inaweza ikawa ni njia mojawapo ya kusukuma fedha kwa wananchi. Lakini mbali na hivyo nimeona kwamba tunaweza tukatumia mradi huu wa shilingi 1.3 trilioni ambao umeingia, kama chachu ya sisi wenyewe kuamka tu na kuanza kutenga fedha kwa ajili ya miradi ambayo inaenda kuwagusa watu. Hususani kufuatia stress ambayo imeufika uchumi wetu na mambo yafuatayo ningependa kushauri yafanyike. Kwamba, katika hizi fedha ambazo tumegawiwa sasa hivi kwenye Majimbo yetu, ni lazima kutengenezwe mfumo mzuri wa usimamizi wa matumizi ya fedha hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lazima kutengenezwe mfumo mzuri wa ufuatiliaji, mfumo mzuri wa tathmini na mwisho wa siku mfumo wa kupima matokeo. Na sasa kuanzia hapo kwa sababu, hizi fedha zitakwenda mpaka mwisho wa bajeti hii tuliyonayo sasa. Kwenye bajeti itakayokuja Serikali ituletee Mapendekezo ya namna ambavyo tutapata pengine shilingi trilioni 1.5 nyingine sasa ambayo tutakwenda nayo kwenye mwaka ule utakaofuata. Na hii itakuwa ni kama vile measure ya ku-stimulate ukuaji wa uchumi baada ya janga la CORONA ambalo limeupiga uchumi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa kama tutakuwa tumeweka mifumo mizuri ya usimamizi, ufuatiliaji na tathmini kutokana na hii shilingi trilion 1.3 tuliyopewa sasa hivi maana yake mwakani tutaendelea tu na Mpango ule. Ambao utakuwa mzuri zaidi kwa ajili ya kutia chachu ukuaji wa uchumi tena na kuhakikisha kuna mzunguko kwenye maisha ya watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo ni lazima tuweke mfumo ambao utawezesha kitu kama pay for performance yaani kama vile performance basic financing. Kwamba, tukiweka vigezo sasa hivi na fedha zimeshakwenda, wale watakaofanya vizuri basi wata-enjoy hiyo shilingi 1.5 trilioni ambayo itakuja kwenye bajeti ijayo. Kwa hivyo mfumo kama huu utapendeza sana kama utafanyiwa kazi, utaandaliwa na hatimaye utatekelezwa. Kwa sababu, linaweza likawa ni jambo la kudumu kwamba, tunatenga fedha kwa ajili ya miradi mahususi kila mwaka kwenye bajeti yetu sisi wenyewe na wala sio kusubiria mikopo ama fedha za wafadhili. Kwa hivyo mfumo kama huu wa kulipa kwa matokeo unaweza ukafikiriwa kutumika kwenye matumizi ya hizi fedha. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini jambo la pili ambalo napenda kulizungumzia, kutokana na stress ambayo imeukumba uchumi wetu, ni lazima mbali na hayo ambayo tayari nimekwisha kuyasema Serikali ifikirie kuweka ahueni kwa wajasiriamali na wahangaikaji. Nchi nyingine tumeona makampuni ambayo yamefeli kulipa mikopo either ile mikopo ikichukuliwa na Serikali kupitia special purpose vehicles, ama yanapewa ahueni kwamba malipo ya marejesho kwa kipindi fulani yatasimamishwa ili hizi biashara ziweze kukua ili ziweze ku-thrive tena kufuatia kuanguka kwa uchumi ambako kumesababishwa na Covid-19. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa sisi kwetu tunaweza tukafanya mambo machache kadhaa ambayo napenda kuyasema. Kwa mfano, kwenye sekta ya utalii ili tuweze kuvutia watu kuja hapa nchini Tanzania inasemwa sana kwamba, ni nchi ambayo ina gharama kubwa kuja kuitembelea basi gharama hizo tunajua zinasababishwa na nini. Ni parking fee za ndege, landing fee za ndege, kodi kwenye jet fuels zote hizi tunaweza, tukatafuta namna ya kwenye bajeti inayokuja pengine tukazishusha chini ili kushusha gharama ya watu kuja Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, na tukazitangaza hizi bei mpya mwisho wa siku tukavutia watalii wengi zaidi kuja hapa Tanzania. Lakini pia, tukavutia wawekezaji wengi zaidi kuja Tanzania. Hiyo nayo inaweza ikawa ni njia mojawapo ya kuweza ku-catalyze economic growth kufuatia janga la UVIKO-19.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini pia, ili ku-stimulate pia growth ya biashara hapa nchini ni lazima tu-consider baadhi ya malipo kwa mfano, pay as you earn, skills development levy. Tukayasimamisha kwa kipindi fulani ili kuyafanya makampuni yetu ambayo yana madeni makubwa ambayo yanashindwa kuendesha shughuli zake, kwa sababu, kipato kimeshuka kutokana na mzunguko kuwa duni yakaweza ku- thrive katika kipindi hiki kigumu ambacho tunapitia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, Serikali inaweza ikaangalia katika Mpango wake namna ya kufanya stimulus, kwenye biashara za hapa nchini ili kuvutia uwekezaji. Lakini pia ili kuwalinda wale wawekezaji ambao wanajikongoja katika kipindi tulichonacho.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pia, Serikali inaweza ikasaidia ni namna gani benki za biashara zifanye kwa wale wafanyabiashara ambao pengine wameshindwa kulipa mikopo. Badala ya kufilisiwa na mali zao kuuzwa ama kufunga biashara basi mikopo ile ikasimamishwa kwa kipindi fulani, ikapelekwa mbele ikafanyiwa restructuring. Halafu biashara zile zikaruhusiwa ziendelee na mwisho wa siku zika-thrive zikachangamka na uchumi ukachangamka kwa ujumla wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hivyo, nilikuwa napenda nitoe ushauri huo kwamba, ni lazima Mpango huu ambao umeletwa hapa tuutolee mawazo yetu ukafikiria namna fulani ya kuweka stimulus kwenye economic growth ya nchi yetu. Na jambo la mwisho ambalo napenda kuzungumzia linahusu uwepo wa baadhi ya miradi ambayo inasemekana imekuwa over costed. Kwamba, anakuja mtu ame-tender labda shilingi 100 anaonekana ni tenderer mmoja, sasa na huyo mmoja anashindwa kupewa ile tender wana re-advertise inapotangazwa kwa mara ya pili anakuja tenderer mwingine. anasema mradi ule badala ya shilingi 100 labda yeye ata-tender kwa shilingi 150 anapewa mradi, akishapewa mradi anarudi kumtafuta yule aliyekuwa ame- tender kwa shilingi 100 anampa ile kazi aende akafanye yeye anakula shilingi 50 bila kufanya kazi yoyote ile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kuna kila haja ya Serikali kuichunguza na kuifuatilia sana miradi yetu na namna tender za miradi mikubwa zinavyofanya. Kwa sababu, kumekuwepo na taarifa za over costing ya miradi kutokana na tenderers kupewa miradi kwa style hiyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)