Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Prof. Sospeter Mwijarubi Muhongo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Musoma Vijijini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru sana kwa kupata hii nafasi. Kwanza kabisa nitoe pongezi kwa Serikali nzima ikiongozwa na Rais wetu kwa kazi nzuri na kutupatia Mpango wa kujadili. Pili, kwa sababu, hapa sipaswi kuongea mambo ya jimbo sana na Ndugu zangu wa Musoma Vijijini wanajua mambo yetu yanaenda vizuri kasoro barabara zetu ambazo nimeongea na TANROADS watabadili mbinu tuweze kupata lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mengi yameongelewa, tunapaswa kutoa ushauri. Hapa napenda kutoa ushauri wangu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nayaongea haya ikiwa kama wahusika watapendezwa wataona yana uzito, basi wanaweza wakayaingiza kwenye mpango ambao wametuletea; kwanza kabisa wakati tunajadili hivi tujue hii ni sehemu ya Mpango ambao unatuelekeza mwaka 2025 tutakuwa tunakamilisha miaka yetu ile mitano ya Mpango wa Maendeleo wa Miaka Mitano ambacho ni kikubwa sana tukifika 2025 tukiwa watu milioni 70 pato letu la Taifa linapaswa kuwa karibu zaidi ya bilioni 210 ikiwa kama pato la mtu mmoja mmoja kweli litafika dola 3,000 kwa mwaka, ndio malengo yetu hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa ili tufike huko kwa kupitia huu mpango mimi nilitaka kwanza mpango wetu watakavyoenda kuutekeleza uwe na malengo. Malengo hasa ni nini tukiwa tunaelekea 2025 na hii ni transit period?

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, tunachotaka kuona kinawekwa msisitizo ni ukuaji wa uchumi, lengo kubwa hilo, growth. Tumeshuka nne, tutaenda tano, sasa tujitahidi kama tunataka kuondoa umasikini nchi hii tujitahidi uchumi uvuke asilimia saba na wanasema ukiwa asilimia nane duniani kote ndio umaskini unapungua. Ukiwa chini ya nane Ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge tujue umasikini bado una sisi. Tukitaka kwenda vizuri sana mpango tuuelekeze kwenye ukuaji wa asilimia 10 na zaidi ndio tutasema sasa uchumi unaenda vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la pili ni kuwafanya wananchi waishi kwa neema yaani wealth creation sijui kiswahili chake lile ni lengo la pili la muhimu sana. Lengo la tatu, kwenye huu Mpango ni suala la ajira tulipaswa kuelezwa ajira ndani ya mwaka huu mmoja tutatengeneza ajira ngapi? Na tunakoelekea 2025 tunadhani tutakuwa tunatengeneza ajira ngapi kila mwaka? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, la nne, ni huduma kwa jamii hayo sasa ni maji, umeme, barabara, hizo ni community service huu Mpango unapaswa kutueleza hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ambacho sikukiona sijakisikia lengo letu tunataka shilingi yetu iwe kubwa, tuna gold refineries mbili mpya tumesema tuanze kuwa na akiba ya dhahabu gold reserve naomba huu Mpango nao useme kwenye huu mwaka unaokuja tutaanzaje? Tutaendaje kwa sababu sasa tuna refineries ambazo zinaweza zikasafisha dhahabu kufikia zaidi ya asilimia 99.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, hayo ndiyo maeneo ambayo tunategemea yawe kwenye Mpango. Lakini nini cha kufanya kutekeleza hayo malengo nini cha kufanya cha kwanza kabisa kimeongelewa na kila mtu ni suala la kilimo hicho ndicho cha kufanya sasa wengi wameyaongea sitaki kurudia huko tena kilimo. Lakini tukisema kilimo tunachukua maana ya mifugo, uvuvi yote hiyo tunaweka kwenye kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, cha pili ni suala la elimu Taifa lote duniani kote hata mataifa yaliyoendelea kila mwaka yana mpango wa elimu na sisi tunataka tufate huu mwaka mmoja tutakuwa na shule ngapi mpya tutaajiri walimu wangapi tutakuwa na vyuo vitatoa wangapi? Mpango wa elimu lazima ujulikane uwepo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine ni afya tunajenga vituo vya afya tunajenga zahanati lakini kwenye Mpango useme kwamba kwa huu mwaka tunakuwa na zahanati kadhaa, vituo vya afya kadhaa, hospitali za rufaa kadhaa. Kingine ni miundombinu ambayo tumesema kamati ya bajeti naishukuru kwa staili ya kilometa tano tano, tatu tatu kila mkoa hiyo siyo mbinu nzuri ya kujenga barabara zetu. Lakini Mpango utueleze utashughulikaje na mambo ya miundombinu hasa mabarabara ya vijijini ambayo yanaenda kuleta mazao kutoka vijijini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na cha muhimu zaidi Mpango uongelee mambo ya mazingira na tabia nchi ni vitu viwili tofauti environment and climate change ni vitu viwili tofauti mazingira na tabia nchi. Mpango sidhani kwamba umejieleza dunia inasema tushuke chini ya nyuzi 1.5 lakini sehemu zingine za Tanzania temperature raise inafika mpaka three degrees celosias kwenye Indian ocean imeshavuka 1% celosias mpango ueleze.

Mheshimiwa Mwenyekiti, huu Mpango sasa ikiwa hayo ndiyo maeneo na malengo, tutoe wapi fedha nadhani hiki ndiyo kitu muhimu sana financial resources cha kwanza ambacho Mpango unapaswa kuegemea kabisa na mapato mengi yatatoka kwenye kilimo na kilimo kama nilivyosema mwezi Februari lazima tuwe na priority hatuwezi kwenda na mazao yote kwa mpigo lazima tuchukue mazao ambayo yanahitajika duniani sasa hivi tuko karibu watu bilioni 8 na watu wanakula mchele kila siku wanatumia ngano kila siku wanatumia mahindi kila siku, wanatumia muhogo hayo mazao manne ndiyo ya muhimu halafu na mazao ya horticulture hayo matunda ma-avocado na nini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mpango huu utueleze tutazalisha mahindi kiasi gani? Ngano kiasi gani? Mihogo kiasi gani? Na hiyo horticulture kiasi gani hatuwezi kuwa tunaongelea avocado hata haujui hauna projection kwamba utazalisha avocado kiasi gani. Chanzo cha pili cha fedha na bahati mbaya sana hakijajadiliwa watanzania naomba nizidi kuwasihi.

MWENYEKITI: Mheshimiwa Professor muda tayari.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Nilikuwa naongelea mambo ya gesi economy, kutumia methyl kutumia helium nilitaka kuongea mambo ya mining kuingia kwenye madini mapya yanayotakiwa sasa hivi duniani especially hii gesi ya helium duniani sisi tukishindwa kuichimba wengine wameweka contracts wanataka kwenda kuichimba mwezini kwa hiyo ya kwetu tunaweza kuwa nayo tunajadiliana itabaki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kingine nilitaka kumalizia hayo huko tunakokwenda ni kutafuta hizi fedha za climate fund halafu vile vile nilitaka kumalizia kwa kusema kwamba Mpango huu kitu ambacho hatujakipata pale ni yard stick tutapimaje tumefanikiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nilitaka kusema ili tujue tumefanikiwa huu mpango utueleze tunapunguza umaskini kwa kiasi gani? GDP per capital inaongezeka kwa kiasi gani? Halafu watu wangapi wamepata kazi? Viwanda vingapi tumevijenga? Yaani hizo naongea kwa ujumla lakini hapa we need facts and figures wakati tutakuja ku-interrogate mafanikio ya mpango huu halafu gold reserve inatia huruma mtu wa kwanza mwenye gold reserve duniani ni Marekani nilishangaa kuona hata Malawi ina gold reserve niki-check Tanzania gold reserve ni zero huu mpango unatuelezaje ndani ya mwaka mmoja tukielekea 2025. (Makofi)

MWENYEKITI: Ahsante sana Professor ahsante sana.

MHE. PROF. SOSPETER M. MUHONGO: Mheshimiwa Mwenyekiti, la mwisho ni kujenga viwanda vyetu vya mbolea Mpango utueleze tunajenga pale Kilwa Mpango haujasema tunajenga na Mtwara, ahsante.