Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Eng. Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa nafasi ya kuchangia.

Awali ya yote nimshukuru Mwenyezi Mungu mwenye enzi na Utukufu kwa kunijaalia kusimama mahali hapa muda na wakati kama huu. Lakini kipekee kabisa nimpongeze mtekelezaji mkuu wa malengo ya nchi yetu mama yetu Samia Hassan Suluhu kwa ubunifu mkubwa anaoufanya katika kuongoza Taifa letu. Kipekee kabisa nimpongeza kwa hizi shilingi trilioni 1.3 ambazo kwa hakika miradi yote imekwenda kuwalenga wananchi wa chini moja kwa moja. Anastahili pongezi na tumuombee kwa Mwenyezi Mungu aendelee kufanya kazi zake kwa umahiri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kuchangia Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo naomba kuishauri Serikali katika biashara ya bandari. Ametangulia kuzungumza mwenyekiti wangu wa kamati lakini naomba na niseme yafuatayo. Serikali imeboresha miundombinu ya bandari zetu kubwa lakini kiukweli Serikali haijajipanga kukamata soko la land locked countries. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kule Mashariki ya Kongo kuna shehena nyingi sana ambazo zinatupita Serikali sasa ianze kufanya makubaliano ya kufanya joint operation katika bandari ya Kalemi eneo la Kalemi au bandari ya Kalemi kuna reli ambayo inatuunganisha moja kwa moja mpaka Zambia. Kwa hiyo, tukifanya joint operation katika bandari ya Kalemi maana yake tunaweza kuzipata shehena zinazoingia na kutoka katika bandari ya Kongo Mashariki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala zima la kufanya joint operation katika bandari za wenzetu siyo suala la ajabu tulishawahi kufanya joint operation katika Port Bell Bandari ya Uganda, na sasa hivi ninavyozungumza tayari Durban imeshafanya makubaliano na DRC na Zambia na Malawi ili kuweza kupata soko lile la Mashariki ya Kongo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini disadvantage ambayo Durban wanayo hawana direct contact ya maji moja kwa moja na DRC. Lakini sisi Mwenyezi Mungu ametujaalia tunayo direct contact na DRC lakini hatujaamua kuitumia fursa ile ipasavyo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa niishauri Serikali au niishauri Serikali kupitia Mamlaka ya Bandari waanze sasa mazungumzo na nchi ya DRC ili tuweze kupeleka mitambo yetu katika bandari ya Kalemi na tuweze kuli-win soko lile katika Mashariki ya Kati. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, labda kwa taarifa zilizopo tayari wenzetu wa nchi Jirani wanalimendea soko lile la Kongo Mashariki tayari meli yao ya SGR inaelekezwa kule ili ku-win mizigo ile inayoingia na kutoka Kongo Mashariki sasa ni wakati wetu sahihi wa kuamua kufanya mazungumzo ili tuweze kuli-win soko lile. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumefanya matengenezo bandari ya Tanga lakini sasa ili bandari ya Tanga iweze kuleta faida na tija inayotarajiwa ni lazima mambo yafuatayo yafanyike. Kwanza reli ya Tanga mpaka Arusha ambayo imeshakarabatiwa iweze kufanya kazi. Serikali imetengeneza kilometa 470 Tanga mpaka Arusha lakini reli ile mpaka sasa haifanyi kazi sasa ili bandari ya Tanga wapate wateja wa Kilimanjaro na Arusha ambao wanakimbilia Mombasa reli ile ni lazima ifanyekazi. Serikali ijipange sasa katika mwaka unaokuja wa fedha bandari ile ya Tanga iweze kuunganishwa na soko la Arusha na la Kilimanjaro.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile reli ile ya Tanga mpaka Arusha ikiweze kusogezwa mpaka Musoma ambapo kuna bandari kule pia tutaweza kuli-win soko la Uganda kupitia kule Victoria. Lakini vile vile reli ile ikiweza kufika Arusha na tayari barabara ya Tanga, Handeni Kibirashi mpaka Singida imeanza kujengwa maana yake tutalivuta soko la Rwanda kwenda Tanga ni karibu zaidi kuliko kukimbilia kwenda … mjini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunapofanya investment kubwa vile vile Serikali ifanye simultaneous mambo mengine bila kuchelewesha delay ya return of that investment. Lakini umuhimu wa barabara ya Handeni Kibirashi mpaka Singida sasa hivi pia umuhimu wake ni rahisi mno kusafirisha mitambo pamoja na vifaa vingine vya ujenzi vinavyokwenda kujenga bomba la mafuta. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo niiombe Serikali kilometa 20 ambazo zimetengwa kufanywa wakati huu ziongezwe barabara ile iweze kuisha kwa haraka kwa maslahi mapana ya Taifa hili. Naomba kuzungumzia suala zima la utekelezaji wa miradi yetu kupitia force account na nalisema hili kwa mapenzi makubwa kwa nchi yangu. Kuna usemi unasema kwamba if you think education is expensive then try ignorance na mimi nasema if you think…

MWENYEKITI: Hapo Mheshimiwa inabidi u-declare interest umo haumo?

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, haya na-declare the interest kwamba na mimi ni mkandarasi mdogo mdogo lakini vile vile nazungumzia professional liability ambayo kwenye force account haipo. Lakini vile vile ninacho kiangalia ni ubora wa vinavyozaliwa kwenye force account.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niseme kwamba halmashauri zetu ambazo sasa force account ndiyo imekuwa inatekelezwa kwa kiwango kikubwa hazina wahandisi na tunapokwenda kununua material ya ujenzi kwa kutumia zile Kamati za Manunuzi zilizoundwa hawafanyi test za material nondo hata kama unakwenda kuinunua kwenye hilo duka nondo lazima ui-test kabla ya kuipeleka site. Kuna test ambazo zinatakiwa kufanywa kwa nongo kama bending test, tensile strength test zinabebwa na kupelekwa site bila hizi test kwa sababu hakuna wahandisi halmashauri. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile tunaponunua hata kokoto kuna test zake ambazo zinatakiwa zifanywe kabla ya kusema kokote hii itaenda kutumika mahala fulani sisi tunabeba tunapeleka site ni liability kubwa sisi tunaamini tuna-save lakini naomba sana tufanye tathmini ya kina katika majengo yote ambayo yamejengwa na force account ili tuone kweli kuna saving? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakwambia hakuna saving kwa sababu gani Mheshimiwa CAG amesema kuna baadhi ya halmashauri nyingi zimeshindwa kufanya retirement baada ya kununua manunuzi hii maana yake ni nini? Serikali imeweka mwongozo wa kufanya kazi kupitia force account. PPRA wametengeneza guidelines lakini guidelines ile haitumiki ndiyo maana wameweza kununua moja kwa moja bila ya kutengeneza framework contract ili uweze kushindanisha bei kati ya supplier mmoja na mwingine lakini wewe unakwenda direct kwenye duka kwenye kiwanda unanunua wakati hakuna framework contract otherwise kusingekuwa hakuna retirement ya materials.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nikwambie kitu kimoja kule Dar es Salaam kuna jengo lilidondoka pale Chang’ombe tunaliita Chang’ombe village Mhandisi aliyesimamia lile jengo alifungwa lakini katikati ya Jijji kuna jengo lilidondoka Mhandisi aliyesimamia lile jengo alifungwa lakini katika force account hakuna professional liability…

MWENYEKITI: Nimeambiwa kumbe ya pili tayari.

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru naomba kutoa hayo kwa ajili ya manufaa ya nchi yetu. (Makofi)