Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Nicodemas Henry Maganga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbogwe

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Ninakushukuru kwa kunipa nafasi hii na mimi nichangie mpango huu kwa siku ya leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niliusoma mpango na nimeuona lakini mimi kwenye kipengele cha miundombinu tumekuwa na adha kubwa. Barabara zetu zinajengwa kwa


kiwango cha lami kwa pesa nyingi lakini baada ya muda mfupi barabara zinakatika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilishauri hapa kwenye Bunge lililopita lakini nashauri tena kuwe kuna miundombinu ya mifereji pembeni. Barabara hizi zinakatika kutokana na maji hakuna miundombinu ya mifereji. Nilikuwa ninaomba kuwe kuna miundombinu ya mifereji wakati wa kuweka hizi bajeti ili barabara zetu ziwe salama.


Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kipengele cha miundombinu kuna kipengele ambacho hakijaguswa, kipengele hiki ni cha majitaka. Kuna adha kubwa ambayo inakuja adha hii ikoje. Kwenye kipengele cha majitaka mtandao wake ni mdogo mno ni mdogo nilizungumzia katika Jiji la Dar es Salaam, lakini sasa tunakwenda kwenye Miji na Majiji yanayokua kwa kasi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukieleza suala la maendeleo ya watu ni lazima uoanishe na miundombinu thabiti. Nikisema hivyo ninaainisha Majiji yanayokua sasa hivi mfano, mtandao wa majitaka katika Mikoa ya Mwanza ni asilimia 3.1 na Jiji lile linakua kwa kasi. Mtandao wa majitaka katika Mji wa Moshi ni asilimia 5.8 ule Mji ulivyo mkubwa unakua kwa kasi. Iringa asilimia 11, Mbeya asilimia 0.6, Songea asilimia 3.7, Tanga asilimia 9.3, Tabora asilimia 0.1, Arusha asilimia 7.0 lakini inakuja Dodoma asilimia 11 ambako ndiko Wabunge wapo, huu ni mtandao siyo wa kuwafikia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninaweza kutoa mfano wa Jiji la Dodoma, Jiji hili linakua kwa kasi ya ajabu, linakua kwa maana ya watu, majengo na viwanda vidogo vidogo. Huwezi kutenganisha maisha ya binadamu na masuala haya ya majitaka. Athari hii itakwenda mbali zaidi kama tutaendelea kulifumbia macho wakati Dodoma mtandao wa majitaka ni asilimia 10 tu ya watu wote waliounganishiwa mtandao huu. Je, kesho yetu ikoje, kwa nini tunahangaika kuagiza madawa nje kwa ajili ya malaria, kwa ajili ya magonjwa ya typhoid, kwa ajili ya kichocho na magonjwa mengine


yanayosababishwa na maji, kipindupindu kwa nini ni kwa sababu hatujaweka miundombinu thabiti ya majitaka. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nawiwa kusema hili kwa sababu naangalia Dodoma inavyokwenda kulipuka kila mtu anakimbilia hapa. Sasa, watu wa DUWASA kupitia research wanasema hawana bajeti ya kujenga miundombinu mipya na kukarabati ya zamani hawana hiyo bajeti. Kesho yetu iko wapi? Ni kwa nini sasa mtandao huu haupo? Haupo kwa sababu ni gharama kubwa. Mtandao wa majitaka katika hili Jiji na Majiji mengine kwa mita 10 ni shilingi 100,000 ili uunganishiwe kutoka kwenye mfumo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukioanisha unapata kilomita Moja ni Shilingi 1,000,000/= mtu kama mimi mpiga kura wa kawaida, mtu aliyeko kijijini, mtu ambaye analia na msiba wa mazao hayajauzika, wamachinga wanapiga kelele wanapata wapi Shilingi Milioni Moja ya kuunganishiwa huu mtandao? Lakini ukiangalia ni asilimia 30 tu ya watu wote waliounganishiwa kwenye huu mtandao, kwa hiyo asilimia 70 tupo tuna-hang tu. (Makofi)

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, taarifa.

SPIKA: Taarifa Mheshimiwa Njau subiri.

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa
Mwenyekiti, taarifa.

SPIKA: Nimekuona Mheshimiwa.

T A A R I F A

MHE. NICODEMAS H. MAGANGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, Mheshimiwa Mbunge anayechangia kuhusu Machinga namuunga mkono sana, kweli Serikali inapaswa iwaangalie machinga maana sasa hivi wanateseka sana. Ahsante sana. (Kicheko)

SPIKA: Yaani Maganga bwana. (Kicheko)

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ninapokea..

SPIKA: Unajua huyo ni Musukuma ameona tu mtoto mweupe hapa! Mheshimiwa Njau endelea. (Kicheko)

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante ninapokea taarifa hii naendelea. Ni lazima tuweze kutibu haya mambo mapema kwa sababu hiki ni kipele cha cancer. Tunapoendelea kufanya maendeleo tujue kwamba, huku chini kuna vitu vingine vitatakiwa vifanyike ili tuweze kwenda mbele.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikitoka hapo naenda kwenye kipengele cha Wakandarasi. Kipengele cha Wakandarasi imekuwa kama wimbo ni mazoea naomba tutoke kwenye mazoea. Kwa sababu, hili ni janga la Kitaifa tena kubwa. Nikisema hivyo tuna ripoti ya CAG ya Machi inasema miradi minne tu kutokana na kucheleweshwa kwa pesa za ile miradi tozo pamoja na faini ni Shilingi Bilioni 101.98 miradi minne. Tunakwenda wapi kama Taifa? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama wataalam wapo ambao wanakaa….

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

SPIKA: Mheshimiwa Halima taarifa.

T A A R I F A

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kumpa taarifa mchangiaji anayechangia vizuri sana, kwamba kwenye ripoti hiyo ya Machi kwenye suala la Wakandarasi CAG amesema taasisi 122 za Serikali zinadaiwa jumla ya shilingi trilioni tatu na zaidi huko. Kwa hiyo, endelea na mchango wako mzuri Mheshimiwa Mbunge. (Makofi/ Kicheko)

SPIKA: Pokea taarifa hiyo Mheshimiwa Felista.

MHE. FELISTA D. NJAU: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea kwa mikono miwili. Nikisema hivi hili suala huwa tunapita tu as if hakuna kitu kinachofanyika, lakini Taifa limedidimia kwa kupoteza pesa nyingi nashawishika kusema hapa kuna kamchezo kanachezwa kati ya mlipaji na mlipwaji. Kwa nini nashawishika, kwa nini huu ugonjwa umekuwa ni endelevu wakati mikataba ipo, kwa nini wanavunja mikataba, kwa nini Wakandarasi hawalipwi? (Makofi/Kicheko)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama Wakandarasi hawalipwi na adha hii inatokea na kila mwaka linatokea, huu ugonjwa umekuwa ni endelevu ifike mahali huu mguu wa cancer ukatwe ili mtu awe salama. Nakushukuru sana. (Makofi)