Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Simon Songe Lusengekile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru nami kwa kunipa nafasi kuchangia Mpango wa Bajeti 2022/23.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kipekee sana nimshukuru Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama yetu Samia Suluhu Hassan, kwa kazi kubwa anayofanya kwa ajili ya Watanzania. Kipekee pia nimshukuru kwa fedha ambazo ametupatia hivi karibuni kwenye majimbo yetu, trilioni 1.3 katika sekta mbalimbali. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze kwa kuchomekea hapo eneo la elimu. Ni kweli kuna kazi zinafanyika kubwa kwenye Majimbo sasa, madarasa yanajengwa, tunamshukuru sana. Lakini ukweli lazima tukubaliane kujengwa kwa madarasa lazima kuwe directly proportional na upatikanaji wa Walimu. Kwa hiyo mimi niishauri Serikali ije na mpango katika Bajeti ya mwaka 2022/23 wa namna gani tunakwenda kuajiri walimu ili wakabiliane na wanafunzi wengi ambao wanakwenda kutumia madarasa haya. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo tunavyokuwa tunamshukuru Mheshimiwa Rais kwa kutupatia madarasa pia tunamshukuru kwa sababu ni imani yangu kwamba tunakwenda ku-create ajira kwa ajili ya Watanzania na Walimu ambao bado hawajapata ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichangie maeneo machache sana ya mpango huu. Taarifa ya Kamati ya Bajeti pamoja na taarifa ya Mheshimiwa Waziri imeonesha kwamba mwenendo wa Shilingi yetu ya Tanzania unazidi kuimarika. Lakini niseme tu kwamba ili shilingi yetu iendelee kuimarika zaidi ni lazima tufikirie ku-export final product kuliko kuwa na importation kubwa ya raw material kwa ajili ya viwanda vyetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kwa nini tunazungumza hivi? Ni lazima tuimarishe viwanda vyetu vya ndani na kuendelea kujenga viwanda mbalimbali ambavyo vitatoa final product kutokana na malighafi ambayo sisi wenyewe tunatengeneza hapa, malighafi nyingi zipo zinatokana na kilimo. Tuchukulie mfano kule kwetu Mkoa wa Simiyu na Mikoa ya Tabora, Mara na Mwanza, tunalima sana pamba, lakini pamba bado haina thamani kwa sababu hatutengenezi final products zinazotokana na pamba, isipokuwa tunafanya exportation ya material ambayo kule wenzetu wanakwenda kutengeneza final product.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ningeishauri Serikali, kuna andiko lilishaletwa Wizarani, Wizara ya Fedha na Wizara ya Viwanda, kujenga kiwanda Mkoa wa Simiyu ili uweze kuhudumia Mikoa ya jirani, na kiwanda hiki kitakuwa cha vifaatiba vitokanavyo na pamba. Tunajua tunaweza tukapata gozi, tunaweza tukapata mashuka. Tutaokoa fedha nyingi za kigeni ambazo tunakwenda kununua vifaa hivi nje, vitaendelea kupatikana kwenye nchi yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kiwanda hiki pia kitatoa ajira kwa Watanzania, zaidi ya Watanzania 1,000 wataajiriwa kupitia viwanda hivi. Kwa hiyo tunapokuwa tunazungumza habari ya viwanda tunazungumza habari ya ku-maintain fedha yetu ili isiendelee kushuka thamani yake bali iendelee kupanda kwa kuwa na products ambazo zinapatikana kwenye nchi yetu. Mfano umeutoa, hata hivi vyuma ambavyo vinatengeneza reli tungekuwa tumetengeneza kupitia Liganga huko wataalam wanasema wala tusingekuwa na haja ya kuagiza. Maana yake fedha yetu ingeendelea kuimarika zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini kwenye kuimarika kwa fedha mimi huwa najifikiria swali moja, sijui wataalam wanasemaje, lakini huwa nawaza kwa nini mimi niko kwenye nchi yangu Tanzania ninakwenda hotelini naambiwa charge ni dola 200. Sasa nawaza kwa nini naambiwa dola 200 kwenye nchi yangu, si niambiwe tu laki nne ya Tanzania nijue? Kwa nini, kwa sababu demand ya dola itakuwa kubwa kuliko supply na demand ikiwa kubwa maana yake fedha yako ya Tanzania ina-depreciate.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa najua wataalam haya wanashauri na mimi naomba niseme kama ambavyo amepiga marufuku Mheshimiwa Simbachawene hivi karibuni kutupa pesa chini wakati wa kutunza vikundi mbalimbali, kuna haja sasa Mheshimiwa Waziri kuja na sera ya kukataza charges zozote ambazo wana-charge katika fedha za kigeni. Hakuna sababu ya kwenda kwenye hoteli ukaambiwa dola, maana yake itabidi ukatafute dola ili uende ukalipe hiyo charge ambayo utakuwa umeambiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nilikwenda siku moja paleā€¦

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, taarifa.

MWENYEKITI: Kabla ya taarifa, Wasukuma mtaipata, mlizoea kutupatupa hela chini sasa mtakamatwa wote. Taarifa inatokea upande gani? Mheshimiwa Ester.

T A A R I F A

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nampa taarifa Kaka yangu, jirani yangu pale Mbunge wa Busega, kwamba ukienda nchi zingine ukifika airport lazima utabadilisha dola ili uweze kutumia kwa pesa za nchi husika, kwa hiyo ni jambo zuri.

MWENYEKITI: Unapokea taarifa Mheshimiwa Lusengekile.

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, naipokea kwa mikono miwili kwa sababu nilienda hoteli moja hapa Dar es Salaam nikanywa soda nikaambiwa dola moja, yaani nikawaza kwa nini naambiwa dola moja, si aniambie tu elfu mbili nijue. Lazima tuheshimu fedha yetu, tukiheshimu fedha yetu itakuwa na thamani, hakuna sababu ya ku- undermine fedha yetu. Mheshimiwa Waziri wa Fedha liangalie hili. (Makofi)

MWENYEKITI: Kwa hiyo Musukuma wewe unakwenda kwenye hoteli hujui hata malipo yatakuaje? Endelea mtani. (Kicheko)

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, issue hapa siyo kujua ni shilingi ngapi, issue hapa ni kuniambia anani-charge kwa dola hiyo ndiyo issue yangu. Mimi hata kama angesema 5,000 sina tatizo mtani, lakini shida ni kuni- charge kwa dola. Kwa hiyo, nataka tuimarishe shilingi yetu kwa namna ya pekee sana ya kuiheshimu fedha yetu. Mtu akifika airport pale ana dola zake atafute benki ilipo abadilishe achukue fedha zetu za ndani aende akaanze kutumia, hapo tutaimarisha shilingi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la riba, tumeona kwenye taarifa ya Kamati ya Bajeti. Wastani wa riba za mabenki kwenye kukopesha sekta binafsi tumeona ni asilimia 16.6. Ni kweli riba hizi ni kubwa na tunatamani mabenki yetu yapunguze riba.

MWENYEKITI: Kengele ya pili hiyo Mheshimiwa.

MHE. SIMON S. LUSENGEKILE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana.