Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. ENG. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, namshukuru sana Mwenyezi Mungu kwa nafasi hii niliyopatiwa ya kuzungumza leo lakini nakushukuru sana Mwenyekiti kwa nafasi vile vile ambayo umenipatia kuweza kuchangia kwenye mapendekezo ya mpango huu wa mwaka mmoja 2022/2023. Binafsi nimpongeze sana Mheshimiwa Rais kwa Kazi kubwa anayoifanya na kwa mambo mengi ambayo ameyatoa ikiwemo bajeti ambazo zimekwenda kwenye majimbo yetu matokeo tunayaona tunaamini kwamba kazi inayoendelea kufanya ni nzuri sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini nimpongeze Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwa kutuletea mpango huu mpango ambao tumeupitia na kuusoma unatupeleka mahali fulani kwenye maendeleo tunayoyatarajia, lakini nimpongeze Mwenyekiti wa Kamati ambaye naye alishauri mambo mengi katika hotuba yake ikiwemo sehemu kubwa ambayo nitachangia ya Kilimo. Binafsi ni muhumini wa Kilimo leo na ninaona kilimo bado kuna kazi kubwa ya kufanya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye Kilimo mwaka jana ilitolewa fedha ya bajeti kama bilioni mia mbili na kitu hivi ambayo kwenye hesabu bilioni mia mbili kati ya tirioni karibu 33 ni fedha kidogo haifiki hata asilimia moja na bado nimeona michango mengi mwenyekiti wa kamati anapendekeza ikiwezekana wapewe bilioni mia nne inaweza ikaleta mchango fulani kwenye maendeleo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, siamini kwamba kutoka uhuru sasa tunaingia miaka 60 hivi karibuni baada ya mwezi mmoja tutakuwa tunasherekea miaka 60. Tumekuwa na slogans nyingi Kilimo kwanza, uhuru yaani yako maneno mengi ambayo tumeyasema lakini bado Kilimo hiki kinaonekana hakiendi maana yake ni kwamba hatujaamua kufanya kudhamiria kuingia kufanya kazi kubwa kwenye kilimo hiki. Nami nimependekeze tu kwanza hata kabla sijasema kwamba ni vizuri kabisa kwenye bajeti yetu asilimia kumi ishughulike na kilimo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, inawezekana bahati nzuri ni mhandisi hatuwezi kupanda mlima kwa gear namba tatu lazima tuondoe namba 1 ikiwezekana mahali fulani tuweke hata hiyo gear ndogo ili tuweze kupanda vizuri sasa tumekuwa tukienda tunakwenda kwa mwendo wa pole pole ambao ninaamini hauwezi kututoa. Kwa mfano, tuna hekta ambazo zinafaa kwa umwangiliaji milioni 29.4 sisi kama nchi tuna scheme ambazo zime-cover 0.4 milioni hekta yaani hatujafika hata milioni moja kwenye zile 29 na bado tunajinasibu kwamba watu asilimia zaidi ya 66 wameajiriwa kwenye sekta hii ya Kilimo hatuwezi kufanya kitu, hizi sekta za uzalishaji lazima zipewe fedha za kutosha tudhamirie kufanya hiki kitu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimesikia wenzangu wanachangia wanaogopa hata kukopa na nini, kukopa hatuna haja ya kukopa bado deni letu stahimilivu hatuna haya ya kuogopa kukopa, tukope tuingie kufanya kazi hii ya kilimo ionekane. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna mambo kadhaa ambayo nafikiri tunatakiwa kuyafanya kwa mfano; tunatakiwa kuhakikisha kwamba tunaporesha hafua za mifugo Kilimo na Uvuvi ambazo ni sekta za uzaliishaji lazima ziboreshwe, lakini tunatakiwa tuboreshe hafua zinazo husika na upatikanaji wa vyakula lakini malisho vile vile na maji, tunatakiwa tuboreshe hafua za huduma za afya za mimea, mifugo na viumbe maji, lakini tunatakiwa tuboreshe hafua za huduma za ugani na usafiri na mafunzo kwa hawa watu wanaoenda kushughulika na kilimo, tunatakiwa tuboreshe hafua za usindikaji na masoko kwa maana na masoko na tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini vile vile, tunatakiwa tushughulike kuhakikisha kwamba tunaporesha M and E Monitoring and evaluation ufuatiliaji wa hii miradi. Sasa siku zote tumekuwa tunazungumza tunataka tuweke milioni mia nne je, ukifikiria sekta ya maziwa peke yake mpaka leo ninavyozunguza hakuna tone la maziwa nchi hii zinazouzwa nje ya nchi hata lita moja haiuzi, lakini ndani ya nchi bado yako maziwa yanamwagwa huko maporini kwenye maeneo tunayotoka kwa sababu gani hakuna mahali pa kwenda kuyatunza yale maziwa hayawezi kukaa siku nne wala siku tano na sisi tunasema tutaweka bilioni mia nne mwaka jana tuliweka bilioni 200.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye mpango huu ukifungua mapendekezo ukurasa namba 63 utagundua tulivyokwenda kwenye kilimo tumepima sample 1,858 kwenye nchi nzima unaweza kupima sample 1,858 za udongo halafu unataka kulima utafiti gani huu tunaufanya siyo kwamba wataalam hatuna namna ya kuwawezesha.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nafikiria nisiseme maneno mengi sana tukubali kwamba sasa Serikali inakwenda kukopa fedha na kuingiza kwenye Kilimo Mifugo na Uvuvi. Niwapongeze Serikali wanaonyesha kabisa kwenye ukurasa namba 18 kwenye kipengele namba 15 ambacho ni XXV kwamba kwenye fedha za covid 19 wamekwenda kuweka bilioni 5 kwenda kusaidia wajasiliamali wadogo wadogo kuboresha vibanda vyao sijui kama itakuwa imeonekana vizuri hii, watu wanaona kama wajasiliamali wadogo wameguswa kwenye hii hotuba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hapo napo nataka iongezwe kwa sababu wajasiriamali hawa wadogo ndio wakulima wetu, ndio wanaofanya shughuli zote huko tuliko iwekwe fedha bili uoga ukidhamiria kumsomesha mwanao ukaanza kuogopa kila siku hata maliza shule ndiya sababu tumekuwa na miaka 60 lakini bado sekta hizi ambazo zinatakiwa ziwezeshwe ili uchumi uchangamke bado hauchangamki. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sisi wote ni mashahidi kwamba pato la Taifa linachangiwa kwa asilimia 26.4 na Kilimo. Sasa tunaogopa nini yaani unajua kabisa kwamba huyu ndiye anayeleta maziwa mengi kwanini usimlishe majani ya kutosha ili atowe maziwa mengi wasiwasi wetu ni nini kama Serikali. Hatuna haja ya kuogopa tuingize fedha kwa sababu hii ni production sector tunaamini kabisa fedha ile itarudi kwa sababu hii itakuwa kama biashara. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, niseme wazi kwamba hoja yangu ya leo nataka nijikite hapa tunaanzisha vikundi vidogo vidogo huko tulipo vya wakulima, vikundi vidogo vidogo vya wavuvi, vikundi vidogo vya wasindikaji. Niseme taarifa njema leo nilikuwa kwenye tamasha la wine pale ni NMB wamesema wasindikaji wale processors wote wanakopa kwa asilimia 10 tu humu nasikia wanasema riba itakuwa asilimia 30 wasindikaji imeshatolewa wanakopa kwa asilimia 10 tu. Kwa hiyo tunauwezo wa kufanya usindikaji processing ya kwetu kwa asilimia 10 hiyo. Kwa nini tunakuwa na mashaka, Serikali ikope tuingie huko tufanye hivi vitu. Maziwa yakatunzwe, maziwa yakasindikwe, maziwa yakawe processed tuanze kufanya biashara na soko la nje. Nina amini kabisa tukichangamsha hizi sector za uzalishaji uchumi wetu utaamka na utakuwa mkubwa kuliko ulivyo leo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunisikiliza. (Makofi)