Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

Hon. Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo ya Taifa Unaokusudiwa Kutekelezwa na Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 pamoja na Mwongozo wa Kuandaa Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipatia nafasi, namshukuru Mwenyezi Mungu aliyenijaalia uzima na mimi kuweza kuchangia mpango siku ya leo. Niwapongeze Kamati kwa kazi kubwa ambayo wameifanya Kamati ya Bajeti, wamefanya kazi kubwa sana kwa uzalendo kwa ajili ya Taifa letu, tunawapongeza sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza na matumizi bora ya rasilimali za nchi tulizonazo, nitaanza na Ziwa Viktoria na Ziwa Tanganyika. Maziwa yote mawili tuna-share zaidi ya nchi moja. Pamoja na kwamba ndani ya ziwa kuna vitu vingi ikiwemo maji, ikiwemo samaki, dagaa na vitu vingine vingi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitaanza na mfano wa Ziwa Tanganyika. Ziwa Tanganyika pamoja na kwamba leo kwenye mpango tunazungumzia upatikanaji wa maji mjini malengo ambayo hayajafikiwa toka tulipoanza kutengeneza mipango yetu, lakini kwenye mpango nilitegemea kuona ni namna gani Serikali imejipanga kutumia maji hayo tuliyonayo kwenda kutatua changamoto za maji kwenye Taifa letu, sijaona kwenye mpango, mmezungumza kidogo sana. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, maeneo ambayo fedha inatumika vibaya ni maeneo ambayo watu wanakwenda kwa ajili ya kufanya survey ya kutafuta maji. Zinatumika fedha nyingi wanaacha mashimo tu kule, lakini kuna vyanzo vya uhakika ambavyo ni Ziwa Tanganyika na Ziwa Victoria. Hatujaona mpango ukionesha hasa kwamba wamewekeza fedha kule ili kufikia malengo ya kupunguza changamoto ya maji Vijijini na Mjini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukiacha suala la maji tu kuna suala la uvuvi, kama wanaweza wakatumia Congo, Zambia, Burundi, tunapozungumza namna ya kuongeza Pato la Taifa ni lazima tuwawezeshe wavuvi wetu waweze kuvua kisasa, pamoja na kuwawezesha, lakini bado lazima tuondoe sheria kandamizi zinazowakandamiza wavuvi wetu

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunategemea tunapozungumza kuongezeka kwa pato tutengeneze mazingira rafiki ya watu ambao wanatakiwa kuongeza Pato la Taifa. Leo pamoja na kwamba nia njema ya Serikali ya kuondoa uvuvi unaoitwa uvuvi haramu, tukachoma vile vifaa lakini lengo ni kuongeza pato, tukawachomea vile vifaa walivyokuwa navyo ambavyo walikuwa wanaongeza pato kupitia hivyo vifaa vinavyoitwa haramu lakini tukawaacha bila hivyo vifaa, mkumbuke wale samaki na dagaa hawajui kwamba hapa ni Tanzania au hapa ni Congo. Kwa hiyo, badala ya kuwasaidia wavuvi tumewatia umaskini. Nilitegemea kwenye mpango tuseme tumejipanga namna gani kwenda kuwaondoa wale wavuvi ambao waliondolewa vile vifaa ambavyo vilikuwa vinaitwa haramu, kuwapa vifaa halali ambavyo ni vya kisasa ili tukaingie kwenye competition na nchi hizo nyingine ambazo tuna-share Ziwa Tanganyika.

Mheshimiwa Mwenyekiti, niombe sana kwenye mpango huu kwa kuwa tunajua kuna fedha zinapatikana kwenye uvuvi, tutafute namna bora, kwanza zikiwemo meli za kisasa kwa kuwa tunashindana, tuko kwenye ushindani. Lazima tutengeneze mazingira rafiki tukiamini kwamba kweli malengo ambayo tunatarajia tumeonesha kwa mifano kuwasaidia wavuvi wetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya ziwa ukiangalia Ziwa Tanganyika ukiacha maji na uvuvi kuna suala la mafuta. Kwenye Mpango hapa nilitegemea nione mmejipanga namna gani kuvuna yale mafuta ya Ziwa Tanganyika ambayo yangesaidia kuongeza Pato la Taifa letu. Tumezungumza kidogo tu na kuna mambo ambayo hatuwezi kuwa na vyanzo vilevile. Kuna rasilimali ambazo tunazo lakini hatujazitumia kama inavyotakiwa. Mungu ametujaalia maziwa kama hayo yapo, lakini hakuna mipango ambayo inaonesha kweli namna gani tumejipanga kutumia rasilimali hizo kuweza kusaidia Taifa letu ikiwemo suala la Ziwa Tanganyika na Ziwa Victoria. Nimezungumza mara nyingi na leo nitaendelea kusema bado hatujatumia inavyotakiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, lakini ndani ya hayo maziwa mawili bado kuna suala la mipaka. Wavuvi wanapoingia ili wakachukue mazao yao yaliyopo mle ndani kwa maana ya samaki, wanaambiwa kuna sehemu ambazo ni za hifadhi. Ukiangalia kwenye mpango hakuna sehemu wamesema wanaweka kiasi gani kwenda kuweka mipaka kwa kuwa hakuna alama yoyote inayoonesha kwamba hapa ni mpaka. Lakini, toka wameanza kusema hayo maeneo ni hifadhi, hatujawahi kuambiwa kwenye hifadhi hiyo, hao samaki wamefika wangapi zaidi ya wananchi kukamatwa na kupewa adhabu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitakwenda kwenye jambo jingine kwa sababu ya muda kuhusu matumizi bora ya ardhi, kabla sijafika huko, tunatambua nia njema ya wale Mawaziri, Tume iliyoundwa kwenda huko kupitia mipaka. Kuna maeneo ambayo leo kwa sababu kwenye mpango hapa Mheshimiwa Waziri ametuambia idadi ya watu inavyoongezeka na kwa neema ya pekee wanawake wanaongezeka kwa asilimia 51 alivyotusomea hapa, lakini ukiangalia kama idadi inaongezeka tulitegemea kwenye mpango watuambie kwa sababu ardhi iko pale pale na idadi ya watu inaongezeka kuwe na Mpango maalum kwa ajili ya kuongeza maeneo ya uzalishaji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna maeneo yamewekwa hayana faida yoyote, hakuna hata mdudu unaweza ukatembea mchana, asubuhi ukakutana nae lakini wananchi wangeozewa hayo maeneo wangeongeza uzalishaji. Kwa hiyo, kuna haja ya Serikali kuwa na mpango maalum wa kupitia angalau kila mwaka kuangalia maeneo ambayo hayana sababu ya kuwa pori tengefu warudishiwe wananchi ili waendelee kuzalisha na waongeze Pato la Taifa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninapozungumza kuna maeneo ambayo yamekuwa na migogoro mara nyingi, hifadhi na wananchi. Pamoja na kuwa hifadhi, lazima tujue hivi wanyama wale wako wangapi, wanaingiza kiasi gani na kama tungeweza kuwapa wananchi wangeingiza kiasi gani kwenye Pato la Taifa. Leo hatuwezi tukawa tunazungumzia mipango ambayo tunathamini pekee wanyama halafu tukaacha wananchi na tunajua kweli idadi inaongezeka na aridhi iko pale pale. Kama kweli tunategemea matokeo chanya ni lazima tuwe na utaratibu maalum wa kuongeza maeneo kwa ajili ya uzalishaji wa Watanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, hapo hapo kwenye matumizi bora ya ardhi, hapo lazima tuzungumze tumepima eneo kiasi gani kwa ajili ya kilimo. Tumezungumza kwamba hapa inasaidia Pato la Taifa asilimia 26 lakini tulitegemea kwenye mpango hapa mtuambie mmetenga kiasi gani kwa ajili ya kwenda kuongeza kwenye Vyuo vya Utafiti, hatujaona hapa! Kwa hiyo, hakuna suala lolote ambalo linaonesha kilimo ni kipaumbele. Ni lazima tuone kwenye mpango hapa kwa sababu huwezi kuboresha kilimo wakati hujaweka fedha kwenye utafiti. Lazima tutafiti tujue. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ukimaliza kwenye utafiti ni lazima fedha itengwe kwa ajili ya kupima udongo. Leo mnatuambia kuna mazao ambayo soko lake ni gumu lakini mnapokuja na mazao mbadala lazima ardhi iwe imepimwa kwamba udongo huu unafaa kwa ajili ya zao hili. Kama hatujapeleka fedha kwa ajili ya kupima udongo hakuna kilimo hapo na lazima mjue kwamba hivi tunaposema kilimo tunazungumza kitu gani. Kuna suala la kupima udongo, kuna suala la pembejeo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru tu kwamba kuna fedha hizo zimetolewa kwa ajili ya kujenga madarasa, ni jambo jema sana, miongoni mwa maeneo ambayo watu wake wameathirika ni pamoja na wakulima wa nchi hii kwa sababu nchi ambazo zilikuwa zinazalisha mbolea na wao walikumbwa na janga hili kwa hiyo, bei imekuwa kubwa ya mbolea. Tulitegemea kipaumbele cha kwanza mngepeleka kuweka ruzuku kwenye pembejeo ili Watanzania na wao waone! Mheshimiwa Waziri huwezi kumpeleka mtoto darasani wakati hajala, lazima ale chakula ashibe ndiyo aende huko darasani. Kwa hiyo, tunategemea kwenye mpango hapa mtuambia mpango wa Serikali pamoja na slogan ya Awamu ya Tano ya Serikali ya Viwanda, lakini viwanda vingekuwepo hapa vingezalisha mbolea. Mbolea ingezalishwa Tanzania bei ingekuwa nafuu na ingeweza kumsaidia mkulima wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mazingira yote haya tunaomba busara ile iliyotumika kwenda kwenye madarasa ni jambo jema na mimi nakubali lakini turudi kwa hawa wakulima ambao hiyo asilimia 26 nikueleze tu ni wakulima wa mkono na kama nia ni njema ya kwenda kumsaidia mtu huyu ni lazima tuoneshe hiyo nia njema ya kumsaidia mkulima wa kawaida kabisa. Ruzuku ni lazima na mimi niseme tu, Serikali iliyopewa dhamana ni lazima muangalie namna ya kuwasaidia hawa wakulima. Hii siyo favor, lazima tujue kwamba tuna dhamana ya kuwasaidia wakulima wa nchi hii. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, lazima tujue athari ya hili jambo, huu ni mwezi Novemba na kama ni Novemba, wakulima wa Nyanda za Juu Kusini zaidi ya Mikoa Saba huu ndiyo mwezi wa kupanda, mbolea haipo! Tutakuja kuingia gharama mara mbili ya kuagiza mazao nje ya nchi badala ya leo kuweka ruzuku kwenye mbolea iweze kuwasaidia Watanzania. Lazima tuchukulie jambo hili kwamba ni jambo muhimu sana na lazima tuone kwamba Watanzania hawa ambao leo tunaamini zaidi ya asilimia 60 tunawapeleka wapi. Wakati nazungumzia hiyo mbolea lazima mjue pia kuna competition ya masoko hao wenzetu na wao hawajalala. Hawa majirani zetu Zambia mfuko wa mbolea ni 65,000 wao wanatoa wapi? Tanzania tunasubiri nini? Lazima tuone yale mambo mazuri ambayo wenzetu wanafanya siyo vibaya kuiga. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. (Makofi)