Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

Hon. Amb. Dr. Pindi Hazara Chana

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

0

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

MHE. BALOZI DKT. PINDI H. CHANA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Nimesimama kwa heshima zote na taadhima kuunga mkono hoja iliyopo mbele yetu ya Kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika. Naunga mkono na ninaomba nianze na historia. Naipongeza sana Serikali, Waziri, Naibu Waziri kwa kutuletea mkataba huu.(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika historia nakumbuka Mwalimu Nyerere ilikuwa ni ndoto yake kuona Afrika ni moja, masuala ya Pan-Africanism. Hivi sasa chini ya AU tumefanikiwa kufanya masuala mengi, kwa mfano tayari tunalo Bunge la Pan-African, pamoja na Bunge hili Mwalimu alitamani sana Afrika iwe moja. Alikuwa anashirikiana na Mzee Mandela na akina Mzee Mugabe na wengine wote. Kwa kweli eneo hili liligawanyishwa na wakoloni. Wakoloni ndiyo walikuja wakafanya kutugawanyisha ili kututawala, lakini sasa wakati umefika wa kuwa na eneo huru la biashara.

Mheshimiwa Naibu Spika, wenzetu Europe wamefanikiwa, European Union, mpaka wamekuwa na fedha inayofanana inaitwa Euro kutumia ndani ya Europe, hawatumii tena pesa za nchi nyingine. Sasa sisi tumefanikiwa katika Jumuiya ya Afrika Mashariki kama ni eneo la kujifunza, wengi wamesema, tulikubaliana kuwa na Common Market, Custom Union, Monetary Union, ultimately tulisema tunakwenda kwenye kitu kinaitwa Political Federation.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo common market hii ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ni eneo zuri la sisi kulielewa vizuri kwa sababu tunapokwenda sasa kwenye eneo huru hapa tunazungumzia masuala ya mahindi, huku ndiko maeneo hasa ya kupeleka mahindi.

Mheshimiwa Naibu Spika, ziko nchi ndani ya Afrika wao kutwa ni kupigana, mara wamefanya mageuzi, mara wanapigana, sisi ni kisiwa cha amani. Kwa hiyo hiyo kwetu sisi tayari ni strength. Na upande ule sasa wana hizo weaknesses ni eneo sasa la kujikita na kuelewa ni namna gani sasa tunatchukua hizo fursa.

Mheshimiwa Naibu Spika, Tanzania tuna watu takribani milioni 60 na sasa tunakwenda kwenye soko la takribani bilioni 1.2, mazao tunazalisha ya kutosha, mambo kama mahindi. Sasa lazima tuone kuwalinda wakulima wetu, wazalishaji wetu. Kwa mfano, tunataka tuagize labda mafuta ya alizetu, lazima tujiulize haya yaliyopo mafuta ya kula tumenunua kiasi cha kutosha? Tunaweka threshold kwamba kabla ya kuagiza ngano au mafuta, lazima ya kwetu tuwe tumechukua a hundred percent ndipo sasa tunaweza tukaagiza vitu vya nje.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo mimi ninaunga mkono hoja hii kwa asilimia mia, na kwa kweli imekuja wakati muafaka, tuchape kazi. Soko hili la pamoja ni letu na bidhaa za kupeleka kwa kweli tunazo. Sisi ni wazalishaji wazuri sana wa mazao (raw materials), sasa tuone namna gani ya kuongeza thamani ili mwananchi anapoenda hata dukani akiona chai ya Tanzania na chai ya nje, akiona bidhaa nyingine aseme hapana sasa nachukua hii ya Tanzania. Wakati mwafaka sasa wa kulinda, kuangalia kodi zote ambazo siyo za lazima tuziondoshe (non-tariff barriers).

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo nimesimama kwa heshima zote kuunga mkono, ilikuwa ni ndoto ya Mwalimu Nyerere, wacha Afrika tufanye kazi kwa pamoja ndipo sasa tutaweza hata kujadiliana na Mabara mengine. Afrika tukiwa pamoja tutaweza kujadiliana na Marekani, tutaweza kujadiliana na Ulaya na nchi zingine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kweli Waziri nakupongeza sana, Kamati imefanya kazi nzuri sana, ninaunga mkono hoja. Tuombe tu TIC wajitahidi kusaidia kuungana na TIC za maeneo mengine tuone namna ya kuboresha.Naunga mkono hoja. (Makofi)