Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

Hon. Charles John Mwijage

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Muleba Kaskazini

Contributions

nil

Answers

nil

Commettees

1

Ministries

nil

Azimio la Bunge la kuridhia Mkataba wa Uanzishwaji wa Eneo Huru la Biashara la Afrika

MHE. CHARLES J. P. MWIJAGE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipatia fursa ya kuchangia hoja iliyopo Mezani. Awali ya yote na mimi naunga mkono Azimio la Kuridhia huu Mkataba, kazi ambayo na mimi nimeshiriki sana katika kufikisha maamuzi ya Wakuu wa nchi za Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, nianzie kwa madhumuni (objectives) ya makubaliano haya. Lengo kubwa ni kutengeneza soko kubwa la Afrika. Wataalam wanasema kufika mwaka 2050 nchi zitakazokuwa na watu wengi ni China, India na African Continent. Kwa hiyo soko ni wingi wa watu.

Mheshimiwa Naibu Spika, leo tunao watu bilioni moja na milioni mia mbili, kama walivyosema Waheshimiwa Wabunge, lakini kwa takwimu za mwaka 2017 Afrika inaagiza nje chakula chenye thamani ya dola bilioni thelathini na tano. Lakini kufika mwaka 2025 keshokutwa tu, Afrika itakuwa inaagiza nje ya Afrika chakula chenye thamani ya dola bilioni 110, yaani pesa zenye thamani kuliko GDP ya nchi hii leo na itakapofika mwaka 2025. Kwa hiyo, kwa vigezo hivyo sisi hatuna kisingizo chochote, lazima tujiunge na soko kubwa na soko la Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, ukiangalia misingi (principles) katika Article No. 5 ya hii Africa Continental Free Trade kuna suala la nipe nikupe (reciprocity). Kipengele namba 9, watu watakaokuwa wameelewana watauziana wao. Ni kama leo tunahangaika na mahindi lakini ukienda upande wa Nakonde, upande wa Malawi, malori yamejazana Malawi yanasafirisha mahindi kwenda Southern Sudan, sisi hapa tunatafuta soko tunakosa. Kumbe sasa tutakapokuwa sisi hatukujiunga – na ninawaomba tujiunge, hakuna sababu ya kuogopa nitaielezea, tujiunge ili wale watakaokubaliana wasije wakatengeneza kundi la waliokubaliana na sisi Tanzania tukabaki tunalia. Kama nilivyoeleze population inakuja Afrika, sasa unajitoa Afrika uwe mgeni wa nani? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo lingine ambalo nataka kulizungumza ni kwamba hatuna sababu ya kuogopa. Tumejipanga kwa kipindi kirefu na hususan kwa kipindi cha miaka 15. Mpango wa kwanza wa miaka mitano tuliondoa vikwazo na ndiyo ikaja kuzaa blueprint katika mpango wa pili wa miaka mitano.

Mheshimiwa Naibu Spika, imeelezwa wazi mambo ya vikwazo, sasa vikwazo tunavijua, viondoke. Ninataka nirudie tena, Tanzania haina ukosevu wa wajasiriamali. Tanzania haina shida ya sekta binafsi, sekta binafsi ya Tanzania imefungwa minyororo, ina vikwazo vya kutosha. Kwa hiyo, ni suala la kuwaondolea vikwazo kama ilivyoandikwa kwenye Blueprint Regulatory Reform.

Mheshimiwa Naibu Spika, napenda niseme Blueprint Regulatory Reform ni mkakati wa kujitokeza (emergent strategy), ni kwamba watu walibishana wakabishana vikwazo vipo au havipo, wataalam wakakaa chini wakaweza kuonesha vikwazo ambavyo wote tunavikiri kama alivyosema Mbunge wa Biharamulo, kwamba unaona vikwazo hivi. Yaani mtu anakupa faini kwamba nipe lita kumi za damu, nitazitoa wapi lita kumi za damu halafu niendelee kuishi?(Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, ukisikiliza maelekezo ya Wabunge katika Bunge Bajeti la lililopita, Wabunge msiwe na wasiwasi kwamba tutashindwa kushindana. Kama maelezo ya Mheshimiwa Spika ya kufanya mageuzi makubwa katika sekta za kiuzalishaji yatazingatiwa tutakwenda kwenye soko la Afrika tukiwa kifua mbele. Transformation ya productive sectors tunaiweza, hakuna jambo geni. Hatutaki kurudia, hatutaki kubaki kwenye idadi ya ng’ombe wengi, hapana, tunataka kuwa na ng’ombe wengi watakaoweza kutoa maziwa mengi na nyama nyingi na ngozi ya kutengeneza viatu vizuri vya moccasins. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo Watanzania msiwe na wasiwasi. Lakini mjadala wa sekta ya elimu wa kutengeneza elimu inayotufaa, siyo tuitakayo, ni mjadala unaopaswa kwenda haraka sana kama alivyozungumza Mbunge wa Viti Maalum kutoka huko Mbinga, lazima tuwe na watu wabunifu na wanaoweza kuchezea teknolojia. Lazima watoto wetu, siyo kwamba waende darasani, waende darasani wapate maarifa na weledi kwa sababu sasa wanakwenda kushindana katika nchi inayoitwa Afrika.

Mheshimiwa Naibu Spika, hatutengenezi watu wa kushindana Mbeya, Songea na Kagera, tunaandaa vijana wetu tutakuwa tukipigiwa simu sisi tukiwa wazee nyumbani, mtoto anakupigia simu akiwa Ivory Coast, anatoka hapo anakwenda Cairo.

Mheshimiwa Naibu Spika, na hili la Continental Africa linakuja. Juzi Misri wameamua wata-pioneer wao kujenga reli kutoka Cairo kwenda mpaka Durban, itapita Dodoma na Mbeya. Hiyo ndiyo Afrika inayokuja, ukiwa na wasiwasi utaachwa unazubaa.

Mheshimiwa Naibu Spika, naunga mkono hoja, naunga mkono Azimio hili. (Makofi)